Njoo, Unifuate
Februari 17–23. 2 Nefi 11–25: “Tunafurahia katika Kristo”


“Februari 17–23. 2 Nefi 11–25: ‘Tunafurahia katika Kristo,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Februari 17–23. 2 Nefi 11–25,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2020

Picha
Isaya akiandika kwenye hati za kukunja

Februari 17–23

2 Nefi 11–25

“Tunafurahia katika Kristo”

Nefi alifundisha kwamba maneno ya Isaya “ni wazi kwa wale wote ambao wamejazwa na roho wa unabii” (2 Nefi 25:4). Unaposoma, mtafute roho wa unabii kwa kujitayarisha kiroho, kumsikiliza Roho, na kuandika misukumo yako.

Andika Misukumo Yako

Kuandika kwenye bamba za chuma siyo rahisi, na nafasi kwenye bamba za nefi ilikuwa kidogo. Kwa hiyo ni kwa nini Nefi alifanya kazi ngumu ya kunakili kiasi kikubwa cha maandishi ya Isaya katika kumbukumbu yake? Alifanya hivyo “ili wowote … watakaoona maneno haya wangeinua mioyo yao na kufurahia” (2 Nefi 11:8). Kwa namna fulani, mwaliko wa kusoma maandishi ya Isaya ni mwaliko wa kufurahia. Unaweza kufurahia, jinsi Nefi alivyofanya, katika utabiri wa Isaya kuhusu kukusanywa kwa Israeli, ujio wa Masiya, na amani ya milenia iliyoahidiwa kwa wenye haki. Unaweza kufurahia kwamba hata katika siku za “shida, na giza,” wewe “umeona nuru kuu” (2 Nefi 18:22; 19:2). Unaweza kufurahia ya kwamba unaweza “kuteka maji kutoka visima vya wokovu” (2 Nefi 22:3). Hii ina maana, unaweza “kufurahia katika Kristo” (2 Nefi 25:26).

Picha
ikoni ya kujifunza kibinafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kibinafsi

2 Nefi 11–25

Ninawezaje kuelewa vyema mafundisho ya Isaya?

Nefi alikiri kwamba kwa baadhi, “maneno ya Isaya sio wazi” (2 Nefi 25:4). Hii bila shaka inaweza kuwa kweli kwa wale ambao hawafahamu vyema desturi za Wayahudi wa kale na jiografia jinsi alivyofahamu Nefi (ona 2 Nefi 25:6). Lakini Nefi alitupa ushauri kutusaidia kupata maana katika maandishi ya Isaya:

“Linganisha maneno yake” kwako (2 Nefi 11:2).Zaidi ya mafunzo ya Isaya yana maana na matumizi zaidi ya moja. Kwa mfano, maandishi yake kuhusu kutawanywa na kukusanywa kwa Israeli kunaweza kukutia msukumo wa kufikiri kuhusu hitaji lako la kutaka “kukusanywa” tena kwa Mwokozi.

Tafuta “kujazwa na roho wa unabii” (2 Nefi 25:4).Njia nzuri ya kuelewa utabiri wa Isaya ni kutafuta msukumo kutoka kwa Roho. Sali kwa ajili ya muongozo wa kiroho. Huenda usielewe kila kitu kwa mara moja, lakini Roho anaweza kukusaidia uweze kujifunza kile unachohitaji kujua kwa ajili ya maisha yako leo.

Pia inaweza kuwa ya manufaa kurejelea misaada ya mafunzo katika maandiko, ikijumuisha marejeo chini ya kurasa, vichwa vya habari vya sura, Mwongozo wa Maandiko, na kadhalika.

2 Nefi 11:2–8; 25:19–29

“Njia iliyo sawa ni kuamini katika Kristo.”

Nefi alitambulisha na kuhitimisha dondoo yake ya Isaya kwa kushiriki ushuhuda wake wa Yesu Kristo (ona 2 Nefi 11:2–8; 25:19–29). Kipi kinakuvutia kuhusu ushuhuda wake? Unapojifunza wiki hii, fikiria kuhusu tamaa za Nefi “kuwashawishi watoto [wake] … kumwamini Kristo, na kupatanishwa na Mungu” (2 Nefi 25:23), na andika vifungu ambavyo vinakushawishi wewe kumwamini na kumfuata Yesu Kristo.

Inaweza kusaidia kukumbuka ya kwamba mengi ya mafunzo ya Isaya kuhusu Mwokozi yanatolewa kupitia ishara. Kwa mfano, unaweza kumuona Mwokozi katika ishara kama vile Bwana wa shamba (ona 2 Nefi 15:1–7), jiwe (ona 2 Nefi 18:14), na nuru (ona 2 Nefi 19:2). Ni ishara gani zingine za Yesu Kristo umepata katika sura hizi? Ishara hizi zinakufundisha nini kumhusu Yeye?

2 Nefi 12–13

Wenye kiburi na wapenda anasa za dunia watanyenyekezwa.

Nefi alikuwa ameona kwamba kiburi kingesababisha kuangamia kwa watu wake 1 Nefi 12:19). Kwa hivyo sio ajabu kwamba Nefi alishiriki na watu wake maonyo ya Isaya yaliyorudiwa mara kwa mara dhidi ya kiburi. Katika sura ya 12 na 13, tafuta maneno ambayo Isaya alitumia kuelezea kuwa na kiburi, kama vile walio na kiburi na wanaringa. Kisha unaweza kujaribu kurudia maonyo haya kwa maneno yako mwenyewe, kana kwamba ulikuwa unajiandikia ujumbe kuonya dhidi ya kiburi.

Ona pia “Sura ya 18: Jihadhari na Kiburi” (Mafundisho ya Marais wa Kanisa: Ezra Taft Benson [2014], 229–40).

2 Nefi 12:2–5; 21:9–12; 22; 24:1–3

Katika Milenia, watu wa Mungu watafurahia amani.

Unaweza kuona yenye manufaa kujiweka katika nafasi ya Nefi na watu wake. Fikiria umetoroka Yerusalemu kabla tu ya kuangamizwa kwake (ona 2 Nefi 25:10), na sasa wewe ni miongoni mwa kutawanywa kwa Israeli. Ingeibua hisi gani kusoma mafundisho ya Isaya kuhusu kukusanywa kwa Israeli katika siku zijazo na milenia iliyo na amani? Kama Watakatifu wa Siku za Mwisho, tumepewa mwito kusaidia kukusanya watu wa Mungu katika siku za mwisho kwa matayarisho ya utawala wa Kristo katika milenia. Unaposoma mistari hii, tafakari jinsi unavyosaidia kutimiza utabiri ambao waliuelezea. Je, unahisi kutiwa msukumo kufanya nini ili kutoa msaada kwa ajili ya kuwakusanya watu wa Mungu?

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mawazo.

2 Nefi 12:1–3

Kama umeshawahi kwenda hekaluni—“mlima wa nyumba ya Bwana”—unaweza kushiriki pamoja na familia yako jinsi maagano ya hekalu yanavyokusaidia “kutembea katika mapito [ya Bwana].” Kama bado hujaenda hekaluni, kusoma mistari hii pamoja kunaweza kuchochea mjadala kuhusu jinsi mnavyoweza kujitayarisha kwa ajili ya baraka za hekaluni.

2 Nefi 15:18–23

Je, familia yako inaweza kufikiria juu ya mifano ya kisasa ya dhana ovu ambazo mistarii hii inaelezea? Tunawezaje kuepuka kudanganywa na dhana za uwongo kuhusu wema na uovu?

2 Nefi 21

Kama familia yako inahitaji usaidizi kuelewa sura hii (ambayo inafanana na Isaya 11), unaweza kupata umaizi katika Mafundisho na Maagano 113:1–6, ambapo Nabii Joseph Smith anajibu baadhi ya maswali kuhusu Isaya 11. Je, tunajifunza nini kuhusu Yesu Kristo kutoka kwenye mistari hii?

2 Nefi 21:9

Ni nini baadhi ya vitu bayana tunavyoweza kufanya ili kuwezesha kuijaza dunia na “elimu ya Bwana”?

2 Nefi 25:23–26

Ni jinsi gani unaweza kuwasaidia wanafamilia wako “kufurahia katika Kristo”? Pengine unaweza kuwaalika waandike kwenye karatasi nyembamba vitu kuhusu Mwokozi ambavyo vinawaletea shangwe. Kisha, wakati wa jioni za familia nyumbani au wakati wa kujifunza maandiko kifamilia , mtu anaweza kusoma kutoka kwenye karatasi nyembamba. Wanafamilia wanaweza kuongezea karatasi nyembamba kwa mwaka mzima.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Kibinafsi

Tafuta mpangilio. Katika maandiko tunaweza kupata mpangilio ambao hutuonyesha jinsi Bwana anavyofanya kazi Yake. Kwa mfano, katika 2 Nefi 11–25, unaweza kupata mipangilio ambayo inayonyesha namna Bwana anavyoonya na kusamehe.

Picha
Hekalu la Panama Jijini Panama

Hekalu la Panama Jijini Panama. “Nyumba ya Bwana itajengwa kileleni mwa milima, … na mataifa yote yataitiririkia” (2 Nefi 12:2).

Chapisha