Njoo, Unifuate
Februari 24–Machi 1. 2 Nefi 26–30: “Kazi ya Kushangaza na ya Maajabu”


“Februari 24–Machi 1. 2 Nefi 26–30: ‘Kazi ya Kushangaza na ya Maajabu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Februari 24–Machi 1. 2 Nefi 26–30,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2020

Picha
Yesu akimsaidia mwanamke

Atakuongoza Kwa Mkono, na Sandra Rast

Februari 24–Machi 1

2 Nefi 26–30

“Kazi Kuu na Maajabu”

Bwana alisema, “Ninawaamuru wanadamu wote … kwamba wataandika maneno ambayo nitawazungumzia” (2 Nefi 29:11). Kupitia Roho, Bwana atazungumza nawe unaposoma neno Lake. Andika kumbukumbu ya kile unachopokea.

Andika Misukumo Yako

“Nawatolea unabii kuhusu siku za mwisho,” Nefi aliandika (2 Nefi 26:14). Hii ina maana kwamba, alikuwa anaandika kuhusu siku zetu. Na kuna sababu ya kuwa na wasi wasi kuhusu kile alichokiona: watu wakikataa nguvu na miujiza ya Mungu, wivu na mabishano vikienea, shetani akiwafunga watu kwa kamba ngumu. Lakini pamoja na hizi “kazi za giza” katika siku za mwisho (2 Nefi 26:10, 22) zinazoongozwa na adui, Nefi pia alizungumzia “kazi ya kushangaza na ya maajabu” ikiongozwa na Bwana Mwenyewe (2 Nefi 27:26). Na kiini katika kazi hiyo ingekuwa kitabu—kitabu kinachozungumza kutoka mavumbini, ambacho kinafichua uwongo wa Shetani, na kinachowakusanya wenye haki kama bendera. Kitabu hicho ni Kitabu cha Mormoni, kazi ya kushangaza ni kazi ya Kanisa la Bwana katika siku za mwisho, na maajabu ni kwamba Anatualika sisi sote, licha ya udhaifu wetu, ili tushiriki.

Picha
ikoni ya kujifunza kibinafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kibinafsi

2 Nefi 26:20–33

Yesu Kristo anawaalika wote wamkaribie Yeye.

Nabii Joseph Smith alifundisha kwamba, Baba wa Mbinguni, “hana mipaka katika rehema na baraka zake, zaidi ya tulivyo tayari kuamini au kupokea” (Makaratasi ya Joseph Smith,Historia 1838–1856, juzuu ya D-1,” uk. 4 [nyongeza], josephsmithpapers.org). Soma kile ambacho Nefi aliona mbele katika 2 Nefi 26:20–22 na kile alichofundisha kuhusu Mwokozi katika mistari ya 23–33, na uyalinganishe haya na kauli ya Joseph Smith. Unajifunza nini kuhusu rehema ya Bwana isiyo na mipaka? Unaweza kufanya nini kama muumini wa Kanisa la Yesu Kristo kuwa na tabia kama za Kristo katika jinsi unayowatendea watoto wa Mungu?

Ona pia 3 Nefi 18:30–32.

2 Nefi 26–27

Ni kitabu gani kimetajwa katika sura hizi?

Unabii wa Nefi katika 2 Nefi 26–27, ambao unategemea zaidi kutoka kwa unabii wa awali wa Isaya (ona Isaya 29), unatabiri ujio kwa Kitabu cha Mormoni. Unabii huu unaelezea yafuatayo:

Pamoja na Isaya, manabii wengine katika biblia wanadokezea Kitabu cha Mormoni, ingawaje hawakitaji kwa jina. Kwa mfano, Ezekieli 37:15–20 anazungumzia “kijiti cha Yusufu,” ambayo inaweza kuwa ikizungumzia kumbukumbu ya Wanefi, ambao walikuwa wa uzao wa Yusufu. Kumbukumbu hii ingekuwa kitu kimoja na “kijiti cha Yuda,” ikimaanisha Biblia.

Mifano mingine inaweza kupatikana katika Mwongozo wa Maandiko, “Kitabu cha Mormoni” (scriptures.ChurchofJesusChrist.org).

2 Nefi 28

Shetani anatafuta kudanganya.

Wingi wa uwongo na mbinu za Shetani vinafichuliwa katika maelezo ya Nefi kuhusu siku za mwisho katika 2 Nefi 28. Jaribu kuvitafuta (kwa mfano, ona mistari 6, 8, 21–23, 29). Je, kwa nini unahitaji kujua kuhusu uwongo wa Shetani? Utafanya nini wakati adui atakapojaribu kukudanganya?

2 Nefi 28:27–3129

Mungu anaendelea kutoa ufunuo ili kuwaongoza watoto Wake.

Kama Watakatifu wa Siku za Mwisho tumebarikiwa na wingi wa neno la Mungu, kwa hiyo maonyo ya Nefi yanaweza kutufaa sisi: kamwe hatufai kuhisi kwamba “tunayo ya kutosha!” Unaposoma maonyo katika 2 Nefi 28 na 29, tafakari juu ya maswali kama haya:

  • Je, Bwana anataka nihisi na kutenda vipi kuhusu neno Lake?

  • Ni kwa nini watu mara nyingine “wana hasira” kwa ajili ya kupokea ukweli zaidi kutoka kwa Mungu? (2 Nefi 28:28). Je, mimi hujihisi namna hii? Ikiwa ni hivyo, nawezaje kuwa mwepesi zaidi wa kupokea ukweli?

  • Inamaanisha nini kupokea neno la Bwana? Ni jinsi gani naweza kumuonyesha ya kwamba nataka kupokea zaidi ya neno Lake?

Ona pia Alma 12:10–11; 3 Nefi 26:6–10.

2 Nefi 29–30

Mungu alikitayarisha Kitabu cha Mormoni kwa ajili ya siku zetu.

Nefi alijua kupitia ufunuo, hata kabla ya Kitabu cha Mormoni kumalizika kuandikwa, kwamba siku moja “kitakuwa cha thamani kuu kwa watoto wa watu” (2 Nefi 28:2). Ni kwa nini Kitabu cha Mormoni kina thamani kuu kwako? Fikiria kuhusu swali hili unaposoma 2 Nefi 29–30. Ni nini baadhi ya kazi za “kushangaza” ambazo mungu anazitimiza duniani na maishani mwako kupitia Kitabu cha Mormoni?

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mawazo.

2 Nefi 26:12–13

Nefi alifundisha kwamba Yesu Kristo anajidhihirisha Mwenyewe kupitia Roho Mtakatifu. Ni uzoefu gani ambao wanafamilia wanaweza kushiriki na kila mmoja wakati shuhuda zao juu ya Mwokozi ziliimarishwa na Roho Mtakatifu?

2 Nefi 26:22; 28:19–22

Pengine familia yako wanaweza kufurahia somo linalofundishwa kwa vielelezo kuonyesha kile ambacho 2 Nefi 26:22 inafundisha kuhusu Shetani. Unaposoma kuhusu mbinu za Shetani katika 2 Nefi 28:19–22, ungeweza kufunga uzi kwenye vifundo vya mtu fulani kuwakilisha “kamba ya kitani.” Ni jinsi gani kamba ya kitani ni kama majaribu ya Shetani? Inawezaje kuwa kamba imara? Ni jinsi gani tunaweza kugundua uwongo wa Shetani?

Picha
Uzi ulioviringishwa

Nefi alilinganisha majaribu ya shetani na “kamba ya kitani.”

2 Nefi 27:20–21

Bwana anaweza kuwa anamaanisha nini anaposema, “Ninaweza kufanya kazi yangu mwenyewe”? Ukweli huu unashawishi vipi jinsi tunavyotumikia katika Kanisa Lake?

2 Nefi 28:30–31

Je, familia yako inaweza kufikiria juu ya kitu ambacho, kama ufunuo kutoka kwa Mungu, hupokelewa vizuri zaidi kidogo kwa wakati mmoja? Ni kwa nini Mungu anatufunulia ukweli, “mstari juu ya mstari, kanuni juu ya kanuni, hapa kidogo na kule kidogo” badala ya wote kwa mara moja?

2 Nefi 29:7–9

Ni madhumuni gani Bwana analenga kuthibitisha au kuonyesha kupitia Kitabu cha Mormoni?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi.

Shiriki umaizi. Kujadiliana na wengine kile unachojifunza kunaweza kuimarisha uelewa wako. Baada ya kusoma 2 Nefi 29:6–14, unaweza kuhisi kupata msukumo kumuelezea rafiki ni kwa nini tunahitaji Kitabu cha Mormoni.

Picha
Nefi akiandika kwenye bamba za dhahabu

Maandishi ya Nefi yalitabiri “kazi ya kushangaza na ya maajabu” ambayo ingetendeka katika siku za mwisho (2 Nefi 27:26).

Chapisha