Njoo, Unifuate
Machi 9–15. Yakobo 1–4: “Patanishweni na Mungu kwa Upatanisho wa Kristo”


“Machi 9–15. Yakobo 1–4: ‘Patanishweni na Mungu kwa Upatanisho wa Kristo,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Machi 9–15. Yakobo 1–4,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2020

Picha
Mwanamke akiwa amepiga magoti miguuni mwa Yesu

Samehewa, na Greg K. Olsen

Machi 9–15

Yakobo 1–4

Patanishweni na Mungu kwa Upatanisho wa Kristo

Unapoandika misukumo ya kiroho, unaonyesha ya kwamba unataka Roho Mtakatifu akufundishe. Unaposoma Yakobo 1–4, zingatia kuandika umaizi wako.

Andika Misukumo Yako

Wanefi walimchukulia Nefi kama “mlinzi mkuu” (Yakobo 1:10). Aliwalinda kutokana na mashambulizi ya maadui zao, na alikuwa amewaonya dhidi ya hatari za kiroho. Sasa alikuwa hayupo, na jukumu la kuwaongoza Wanefi kiroho lilimwangukia Yakobo, ambaye Nefi alikuwa amemtenga kuwa kuhani na mwalimu wa watu hawa (ona Yakobo 1:18). Kupitia msukumo, Yakobo aliona kwamba watu wake walihitaji kufundishwa kwa kutumia “maneno makali,” kwa kuwa walikuwa “wameanza kutumikia katika dhambi” (Yakobo2:7, 5). Dhambi hizi zilikuwa sawa na zile ambazo watu wanapambana nazo siku hizi: kupenda mali na uasherati. Na huku Yakobo akihisi kwamba ilimbidi kushutumu uovu huu, moyo wake pia ulihuzunika kwa ajili ya waathiriwa, ambao mioyo yao ilikuwa “imedungwa na vidonda vikubwa” (Yakobo 2:35). Yakobo alishuhudia ya kwamba uponyaji kwa makundi yote mawili—mtenda dhambi na aliyepata kidonda cha kiroho—unakuja kutoka kwa Mwokozi Yesu Kristo. Ujumbe wa Yakobo, kama ule ujumbe wa Nefi aliyemtangulia, ilikuwa ni mwito wa ku “Patanishwa na [Mungu] kwa Upatanisho wa Kristo” (Yakobo 4:11).

Picha
ikoni ya kujifunza kibinafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kibinafsi

Yakobo 1:6–8, 15–19; 2:1–11

Bwana ananitaka niutukuze wito wangu.

Kwa Yakobo, kufundisha neno la Mungu ilikuwa ni zaidi ya jukumu kutoka kwa ndugu yake—ilikuwa “mwito kutoka kwa Bwana,” kwa hiyo alitumikia kwa bidii ku “adhimisha ofisi [yake]” (Yakobo 1:17, 19). Rais Gordon B. Hinckley alifundisha ya kwamba tunaadhimisha miito yetu “tunapotumikia kwa bidii, tunapofundisha kwa imani na ushuhuda, tunapoinua na kuimarisha na kujenga kusadiki kwa haki kwa wale ambao maisha yao tunagusa ” (“Adhimisha Mwito Wako,” Ensign, Mei 1989, 47). Fikiria kuhusu “[miito] yako kutoka kwa Bwana” unaposoma Yakobo 1:6–8, 15–19 na 2:1–11. Kwa nini Yakobo alitumika kwa uaminifu sana? Mfano wake unakutia msukumo ufanye nini ili kuadhimisha miito yako ya Kanisa na majukumu yako nyumbani?

Ona pia “Tekeleza Mwito Wako” (video, ChurchofJesusChrist.org).

Yakobo 2:23–3:12

Bwana anafurahia usafi wa kimwili.

Dhambi ina matokeo kwa watu binafsi na jamii. Akizungumza kuhusu uzinzi, Yakobo alionya juu ya aina zote mbili za matokeo. Utakaposoma Yakobo 2:31–35 na 3:10, tafuta njia ambazo uovu ulikuwa ukiwaathiri Wanefi kama jamii na kama watu binafsi. Ni kwa namna gani njia hizi ni sawa na matokeo ya uovu unaouona katika dunia ya leo? Je, unapata nini katika maneno ya Yakobo ambacho kinaweza kukusaidia kumfundisha mpendwa wako umuhimu wa usafi wa kimwili? Jinsi gani umebarikiwa kwa juhudi zako kubaki msafi kimwili?

Kumbuka kwamba Yakobo alizungumzia pia desturi ya kuwa na mke zaidi ya mmoja. Unapata nini katika Yakobo 2:23–30 ambacho kinakusaidia kuelewa ni kwa nini Bwana, katika hali chache, aliwaamuru watu Wake kuwa na wake wengi? Je, ana hisia gani kwa wale wanaofanya hivyo bila idhini yake?

Yakobo 4

Ninaweza kupatanishwa na Mungu kwa Upatanisho wa Yesu Kristo.

Yakobo aliwaomba watu wake ku “patanishwa na [Mungu] kwa upatanisho wa Kristo” (Yakobo 4:11). Unafikiri hiyo ina maana gani? Je, inaweza kusaidia kutafuta patanishwa katika kamusi? Pengine unaweza kupata maneno au virai katika sura hii ambavyo vinapendekeza kwako jinsi unavyoweza kumkaribia Kristo ili uweze kupatanishwa na Mungu. Kwa mfano, Yakobo alifundisha kwamba sheria ya Musa ilitolewa kwa ajili ya kuwaelekeza watu kwa Yesu Kristo (ona Yakobo 4:5). Mungu ametoa nini cha kukuelekeza wewe kwa Kristo? Ni kwa jinsi gani unatumia vitu hivi ili kumkaribia Mungu?

Ona pia 2 Nefi 10:24.

Yakobo 4:8–18

Naweza kuepuka upofu wa kiroho kwa kufokasi kwa Mwokozi.

Yakobo alipokuwa akitafuta kuwarudisha watu wake kikamilifu kwa Bwana, aliwaonya kwamba wasiwe vipofu kiroho na kwamba wasidharau “maneno yaliyokuwa wazi” ya injili (ona Yakobo 4:13–14). Mzee Quentin L. Cook alionya kuhusu changamoto kama hizo katika siku zetu, “Kuna tabia miongoni mwa baadhi yetu ‘kuangalia zaidi ya alama’ badala ya kudumisha ushuhuda wa misingi ya injili. Tunafanya hivi wakati tunapoweka falsafa za wanadamu katika nafasi ya kweli za injili, kuhusika katika injili isiyo na kadiri, … au kuinua masharti juu ya mafundisho ya injili. Kuepuka tabia hizi kutatusaidia kuepuka upofu wa teologia na makosa ambayo Yakobo alielezea” (“Kuangalia Zaidi ya Alama,” Ensign, Mac. 2003, 42).

Kulingana na Yakobo 4:8–18, tunaweza kufanya nini kufokasi kwa Mwokozi na kuepuka upofu wa kiroho?

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mawazo.

Yakobo 1:6–8, 15–19; 2:1–11; 4:18

Ni maneno na virai gani katika mistari hii vinaonyesha upendo ambao Yakobo alikuwa nao kwa wale aliowaongoza? Ni nini viongozi wetu wa Kanisa wamefanya kutusaidia kuhisi “hamu na wasiwasi wa ustawi wa nafsi [zetu]”? (Yakobo 2:3). Pengine wanafamilia wanaweza kushiriki njia ambazo tunaweza kuwaidhinisha viongozi wetu wa Kanisa. Mnaweza mkafanya mpango wa kufanya kitu fulani kama familia kwa ajili ya viongozi wa Kanisa katika mtaa wenu, kama vile kuandika jumbe za kuwashukuru kwa ajili ya huduma yao au kuwakumbuka wao na familia zao katika maombi yenu.

Yakobo 2:8

Ni jinsi gani neno la Mungu linaponya “nafsi iliyojeruhiwa”?

Yakobo 2:12–21

Mistari hii inafundisha nini kuhusu mtazamo ambao tunapaswa kuwa nao kuhusu mali ya dunia? Tunafanya nini ili kuwasaidia wengine ambao wanahitaji msaada wetu?

Yakobo 3:1–2

Inamaanisha nini kuwa “safi moyoni” na “kumtegemeaMungu kwa mawazo yote”?

Yakobo 4:4–11

Njia moja ya kusaidia familia yako kuelewa maana ya “ kutotingishwa” katika imani yao inaweza kuwa kutafuta mti mkubwa karibu nanyi na kuwauliza wanafamilia watikise mojawapo ya matawi yake. Kisha waruhusu wajaribu kutikisa shina la mti. Kwa nini ni vigumu zaidi kutikisa shina la mti? Tunaweza kujifunza nini kutoka kwenye mafundisho ya Yakobo kuhusu jinsi ya kukuza imani ambayo “haiwezi kutingishwa”?

Picha
mti mkubwa katika bustani

Kama shina la mti, imani yetu katika Kristo yaweza kuwa “isiyoweza kutingishwa.”

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Kibinafsi.

Msikilize Roho. Unapojifunza, kuwa makini na mawazo na hisia zako (ona M&M 8:2–3), hata kama zinaonekana hazihusiani na kile unachosoma. Mawazo hayo yanaweza kuwa ndiyo mambo hasa Mungu anakutaka uyajue na uyafanye.

Picha
Yakobo akiandika kwenye bamba za dhahabu

Nitayatuma Maneno Yao (Mwalimu Yakobo), na Elspeth Caitlin Young

Chapisha