Njoo, Unifuate
Januari 28–Februari 3. Mathayo 3; Marko 1; Luka 3 ‘Itengenezeni Njia ya Bwana’


“Januari 28–Februari 3 Mathayo 3 ; Marko 1; Luka 3: ‘Itengenezeni Njia ya Bwana’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019 (2019)

“Januari 28–Februari 3 Matthew 3 ; Marko1; Luka 3,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019

Picha
Yohana Mbatizaji Anambatiza Yesu

Dirisha-lenye kioo kilichotiwa rangi za kuona katika Hekalu la Illinois, na Tom Holdman

Januari 28–Februari 3

Mathayo 3; Marko 1; Luka 3

“Itengenezeni njia ya Bwana”

Anza kwa kusoma Mathayo 3; Marko 1; na Luka 3. Unapoomba Roho Mtakatifu akuongoze kuelewa sura hizi, Yeye atakupa umaizi ambao ni mahususi kwa ajili yako. Andika misukumo hii, na weka mipango ya kuifanyia kazi.

Andika Misiukumo Yako

Yesu Kristo na injili Yake anaweza kukubadilisha. Luka alidondoa unabii wa kale wa Isaya ambao ulielezea misheni ya Yohana Mbatizaji na matokeo ambayo ujio wa Mwokozi ungeleta “Kila bonde litajazwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyooka, Na palipoparuza patalainishwa” (Luka 3:5; ona pia Isaya 40:4). Huu ni ujumbe kwetu sote, ikijumuisha wale wanaofikiria kuwa hawawezi kubadilika au hawahitaji kubadilika. Kama kitu cha kudumu kama mlima kinaweza kushushwa, basi hakika Bwana anaweza kutusaidia kunyoosha njia zetu zilizopotoka (ona Luka 3:4–5). Tunapokubali mwaliko wa Yohana Mbatizaji wa kutubu na kubadilika, tunaandaa akili na mioyo yetu kumpokea Yesu Kristo ili kwamba nasi pia tuweze “kuona wokovu wa Mungu”(Luka 3:6).

Picha
ikoni ya ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Injili ya Marko

Marko alikuwa nani?

Miongoni mwa waandishi wa Injili, tunajua kidogo tu kuhusu Marko. Tunajua kwamba alikuwa mmisionari mwenza wa Paulo, Petro, na wamisionari wengine kadhaa. Wasomi wengi wa biblia huamini kwamba Petro alimuelekeza Marko kuandika matukio ya maisha ya Mwokozi. Injili ya Marko yawezekana iliandikwa kabla ya hizi zingine tatu.

Ona pia Kamusi ya Biblia, “Marko.”

Mathayo 3:1–12; Marko 1:1–8; Luka 3:2–18

Toba ni badiliko kuu la akili na moyo.

Misheni ya Yohana Mbatizaji ilikuwa ni kuandaa mioyo ya watu ili kumpokea Mwokozi na kuwa zaidi kama Yeye. Alitimizaje hilo? Alitangaza, “Tubuni” (Mathayo 3:2). Alitumia mifano kama vile tunda na ngano kusisitiza umuhimu wa kutubu ili kumpokea Kristo (ona Luka 3:9, 17).

Je, ni mifano gani mingine unayoipata katika maelezo ya huduma ya Yohana Mbatizaji? Fikiria kuiwekea alama katika maandiko yako au kuchora michoro yake katika shajara ya kujifunza. Je, mifano hii inafundisha nini kuhusu injili na umuhimu wa toba?

Toba ya kweli ni “badiliko la akili, mtazamo mpya kuhusu Mungu, kuhusu sisi wenyewe, na kuhusu ulimwengu. … [Humaanisha] badiliko la moyo na mapenzi kwa Mungu” (Kamusi ya Biblia “Toba”). Katika Luka 3:7–14, ni mabadiliko gani Yohana aliwaalika watu kufanya ili kujiandaa kumpokea Kristo? Je, ni kwa jinsi gani ushauri huu unakugusa wewe? Je, ni kwa namna gani wewe unaweza kuonyesha kwamba umetubu kweli? (Ona Luka 3:8.)

Ona pia Tafsiri ya Joseph Smith, Luka 3:4–11 (katika kiambatisho cha Biblia); Kamusi ya Biblia, “Yohana Mbatizaji”; D. Todd Christofferson, “Zawadi Takatifu ya Toba,” Ensign au Liahona, Nov. 2011, 38–41.

Mathayo 3:7; Luka 3:7

Mafarisayo na Masadukayo walikuwa nani?

Mafarisayo walikuwa waumini wa chama cha dini ya Kiyahudi waliojiinua kwa kufuata kikamilifu sheria ya Musa. Walijaribu kudunisha dini kwa kufuata tabia nyingi za kimila. Masadukayo walikuwa Wayahudi matajiri wenye mfanano wa ushawishi wa kidini na kisiasa. Hawakuamini katika injili ya ufufuko. Makundi yote mawili yalikuwa yamepotoka kutoka kwenye nia ya mwanzo wa sheria za Mungu, na wengi wa washiriki wao walikataa kukubali ujumbe wa nabii wa Mungu, Yohana Mbatizaji.

Ona pia Mathayo 23:27; Yohana 1:19–24; Kamusi ya Biblia, “Mafarisayo” na “Masadukayo.”

Mathayo 3:13–17; Marko 1:9–11; Luka 3:15–16, 21–22

Yesu Kristo alibatizwa ili “kutimiza haki yote.”

Wakati wewe ulipobatizwa, ulifuata mfano wa Mwokozi. Linganisha kile unachojifunza kutoka kwenye hadithi hizi za ubatizo wa Mwokozi na kile kilichotokea wakati wa ubatizo wako.

Je, ni nani alimbatiza Yesu, na alikuwa na mamlaka gani?

Je, ni nani alikubatiza wewe, na alikuwa na mamlaka gani?

Je, Yesu Kristo alibatiziwa wapi?

Je, wewe ulibatizwa wapi?

Je, Yesu Kristo alibatizwaje?

Je ,wewe ulibatizwa vipi?

Kwa nini Yesu alibatizwa?

Kwa nini wewe ulibatizwa?

Je, ni kwa jinsi gani Baba wa Mbinguni alionyesha kwamba alipendezwa na Yesu?

Je, ni kwa jinsi gani Baba wa Mbinguni alionyesha kwamba alipendezwa wakati wewe ulipobatizwa? Je, ni kwa jinsi gani Yeye ameonyesha kukubali Kwake tangu wakati huo?

Nefi aliandika baadhi ya mafundisho muhimu kuhusu ubatizo wa Mwokozi. Maneno yake katika 2 Nefi 31 yanakufundisha nini? Fikiria kuweka kumbukumbu ya uzoefu wako wa ubatizo katika shajara yako.

Ona pia Yohana 1:32–33; Mosia 18:8–11; Mafundisho na Maagano 13:1; 20:37, 68–74; “The Baptism of Jesus” (video, LDS.org).

Mathayo 3:16–17; Marko 1:9–11; Luka 3:21–22

Je, Biblia inafundisha kwamba washiriki wa Uungu ni viumbe vitatu tofauti?

Biblia ina ushahidi mwingi kwamba washiriki wa Uungu ni viumbe vitatu tofauti. Kwa mfano, maelezo ya ubatizo wa Mwokozi huunga mkono injili kwamba Mungu Baba, Yesu Kristo, na Roho Mtakatifu ni viumbe watatu tofauti. Mungu Baba aliongea kutoka mbinguni, na Roho Mtakatifu (akiwakilishwa na njiwa) alimshukia Mwokozi Alipokuwa akibatizwa. Haya ni baadhi ya maandiko mengine ambayo hufundisha ukweli sawa na huu: Mwanzo 1:26–27; Mathayo 17:1–5; Yohana 17:20–23; Matendo 7:55–56; and Mafundisho na Maagano 130:22.

Picha
ikoni ya kujifunza kwa familia.

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Kwa Familia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho Mtakatifu anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mapendekezo:

Mathayo 3

Yohana Mbatizaji alikuwa na Ukuhani wa Haruni. Tunaweza kujifunza nini kuhusu Ukuhani wa Haruni tunapojifunza kumhusu yeye? Je, ni kwa jinsi gani mfano wa Yohana unawasaidia wenye Ukuhani wa Haruni kutimiza majukumu yao? (Ona pia M&M 13:1; 20:46–60.)

Mathayo 3:11–17; Marko 1:9–11; Luka 3:21–22

Kuwafundisha wanafamilia kuhusu ubatizo na kipawa cha Roho Mtakatifu, fikiria kuonyesha kitu kichafu na kuwaacha wanafamilia wakioshe kwa maji. Ni kwa jinsi gani tendo hili huwakilisha ubatizo? Kisha waombe wanafamilia kuongea kuhusu baadhi ya sifa za kusafisha za moto. Kwa nini kipawa cha Roho Mtakatifu huelezewa kama “ubatizo wa moto”? Ona Kamusi ya Biblia, “Roho Mtakatifu.”)

Picha
kijana akimbatiza kijana mwenzake.

Tunapobatizwa, dhambi zetu zinaoshwa kabisa.

Mathayo 3:17; Marko 1:11; Luka 3:22

Je, ni wakati gani tumehisi kwamba Mungu amependezwa nasi? Tunaweza kufanya nini kama familia ili kumpendeza Mungu?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi.

Muombe Bwana msaada. Maandiko yalitolewa kwa ufunuo, na ili kuyaelewa vyema tunahitaji ufunuo binafsi. Bwana ameahidi “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa” (Mathayo 7:7).

Picha
Yohana anambatiza Yesu

Yohana Mbatizaji Anambatiza Yesu, na Greg K. Olsen.

Chapisha