Njoo, Unifuate
Februari 11–17. Yohana 2–4: ‘Hamna Budi Kuzaliwa Mara ya Pili’


“February 11–17. Yohana 2–4: ‘Hamna Budi Kuzaliwa Mara ya Pili’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019 (2019)

“February 11–17. Yohana 2–4,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Yesu anazungumza na Nikodemo

Februari 11–17

Yohana 2–4

“Hamna Budi Kuzaliwa Mara ya Pili”

Unaposoma Yohana 2–4, Roho atakufundisha mambo kuhusu uongofu wako mwenyewe. Andika mnong’ono Wake. Unaweza kupata umaizi wa ziada wa kiroho kutoka kwenye mawazo ya kujifunza katika muhtasari huu.

Andika Misukumo Yako

Katika sherehe ya harusi huko Kana, Kristo aligeuza maji kuwa divai—tukio ambalo Yohana aliliita “mwanzo wa ishara” (Yohana 2:11). Hilo ni kweli kwa zaidi ya dhana moja: wakati huo ulikuwa ni muujiza wa kwanza Yesu alioutenda hadharani, unaweza pia kuashiria mwanzo mwingine wa kimiujiza—hatua ya mioyo yetu kugeuzwa tunapokuwa zaidi kama Mwokozi wetu. Muujiza wa maisha yote huanza na uamuzi wa kumfuata Yesu Kristo, kubadilika na kuishi maisha bora kupitia Yeye. Hatimaye badiliko hili linaweza kutimia kabisa kwamba “kuzaliwa mara ya pili” ni mojawapo ya njia bora za kulielezea (Yohana 3:7). Lakini kuzaliwa tena ni mwanzo tu wa njia ya ufuasi. Maneno ya Kristo kwa mwanamke Msamaria kisimani hutukumbusha kwamba kama tukiendelea katika njia hii, mwishowe injili itakuwa “chemchemi ya maji” ndani yetu, “yakibubujikia uzima wa milele” (Yohana 4:14).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Yohana 2:1–11

Nguvu ya Yesu Kristo inaweza kunibadili.

Unaposoma kuhusu Mwokozi kugeuza maji kuwa divai katika Yohana 2:1–11, unapata umaizi gani kuhusu nguvu ya Kristo kukubadili?

Unaweza kupata umaizi wa ziada kwa kukumbuka mitazamo ya watu tofauti waliokuwepo pale, kama vile Mariamu, mitume, na wengine. Ni kwa jinsi gani watu hawa walipiata uzoefu wa muujiza? Unaweza kulinganisha kile unachojifunza kuhusu miujiza katika mistari hii na kile Yesu Kristo alichomfundisha Nikodemo (ona Yohana 3:1–8) na mwanamke kisimani (ona Yohana 4:3–26).

Yohana 3:1–21

Sina budi kuzaliwa mara ya pili ili kuingia ufalme wa Mungu.

Wakati Nikodemo alipomjia Yesu kwa siri, alikuwa mchunguzi mwangalifu. Baadaye, hata hivyo, alimtetea Yesu hadharani (ona Yohana 7:45–52) na aliungana na waaminio katika mazishi ya Mwokozi (ona Yohana 19:38–40). Ni mafundisho gani unapata katika Yohana 3:1–21 ambayo yalimshawishi Nikodemo kumfuata Yesu na kuzaliwa mara ya pili?

Nabii Joseph Smith alifundisha, “Kuzaliwa mara ya pili, huja kwa Roho wa Mungu kupitia ibada” (Teachings of Presidents of the Church: Joseph Smith [2007], 95). Ni wajibu gani ubatizo wako (“kuzaliwa kwa maji” [Yohana 3:5]) na uthibitisho (“kuzaliwa kwa Roho” [Yohana 3:5]) hufanya katika kuzaliwa mara ya pili? Unafanya nini kuendeleza hatua hii ya kubadilika? (Ona Alma 5:11–14.)

Ona pia Mosia 5:7; 27:25–26; “Wokovu,” Mada za Injili, topics.lds.org; David A. Bednar, “Lazima Uzaliwe Upya,” Ensign or Liahona, Mei 2007, 19–22.

Yohana 3:16–17

Baba wa Mbinguni huonyesha upendo wake kwangu kupitia Yesu Kristo.

Mzee Jeffrey R. Holland alifundisha, “ukweli mkuu wa kwanza wa milele yote ni kwamba Mungu hutupenda sisi kwa moyo Wake wote, nguvu, akili, na uwezo” (“Kesho Bwana Atafanya Maajabu kati Yenu,” Ensign au Liahona, Mei 2016, 127). Ni kwa jinsi gani umehisi upendo wa Mungu kupitia zawadi ya Mwana Wake?

Sakramenti hutoa muda wa kufikiria juu ya upendo wa Mungu na zawadi ya Mwana Wake. Nyimbo zipi hukusaidia kuhisi upendo huu? Fikiria kuangalia video ya Mormon Tabernacle Kwaya ikiimba “Nashangazwa” (LDS.org). Unaweza kufanya nini kufanya sakramenti iwe na maana zaidi?

Yohana 4:24

Je, Mungu ni Roho?

Baadhi wanaweza kukanganywa na kauli ya Yesu kwamba Mungu ni Roho. Tafsiri ya Joseph Smith ya mstari huu hutoa ufafanuzi muhimu: “Kwani kwa hao Mungu ameahidi Roho wake” (katika Yohana 4:24, tanbihi a). Ufunuo wa nyakati hizi pia hufundisha kwamba Mungu ana mwili wa nyama na mifupa (ona M&M 130:22–23; ona pia Mwanzo 5:1–3; Waebrania 1:1–3).

Yohana 4:7–26

Yesu Kristo hunipatia maji Yake ya uzima.

Nini Yesu alikuwa akimaanisha alipomwambia mwanamke Msamaria kwamba yeyote anywaye maji anayompa hataona kiu kamwe? Ni kwa jinsi gani injili ni kama maji ya uzima?

Picha
kijito cha maji

Injili ya Kristo ni maji ya uzima ambayo hurutubisha nafsi zetu.

Mojawapo ya ujumbe wa Mwokozi kwa mwanamke Msamaria ilikuwa kwamba jinsi tunavyoabudu ni muhimu zaidi ya wapi tunaabudu (ona Yohana 4:21–24). Je! Unafanya nini ili “kumwabudu Baba katika roho na kweli”? (Yohana 4:23).

Ona pia Mwongozo wa Maandiko, “Abudu”; Dean M. Davies, “Baraka za Kuabudu,” Ensign au Liahona, Nov. 2016, 93–95.

Picha
ikoni ya kujifunza kwa familia

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Kwa Familia na Jioni ya Familia Nyumbani

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mapendekezo:

Yohana 2–4

Familia yako inaposoma sura hizi wiki hii, kuwa makini na jinsi Mwokozi alivyotumia mambo ya kila siku—kuzaliwa, upepo, maji, na chakula—kufundisha kweli za kiroho. Ni kitu gani nyumbani kwako unaweza kutumia kufundisha kweli za kiroho?

Yohana 2:13–17

Unapoepuka mambo yatakayofanya nyumba yako kuwa chafu kimwili na kiroho, inaweza kuwa mahali patakatifu—kama hekalu. Ni nini familia yako inahitaji kuondoa nyumbani ili pawe mahali patakatifu? Utafanya nini ili kuondoa vitu hivyo?

Yohana 3:1–6

Waombe wanafamilia kufikiria muujiza wa ujauzito na kujifungua—hatua ya kuumba kiumbe hai, kinachotembea, chenye akili. Kristo alifundisha kwamba hatuna budi kuzaliwa tena kabla ya kuingia ufalme wa Mungu. Kwa nini kuzaliwa tena ni sitiari ya badiliko linalohitajika kwetu kabla ya kuweza kuingia ufalme wa Mungu? Ni kwa jinsi gani tumepata uzoefu wa hatua ya kuzaliwa tena kiroho?

Yohana 3:16

Waalike wanafamilia kusema tena mstari huu kwa maneno yao wenyewe kama vile walikuwa wanauelezea kwa rafiki. Ni jinsi gani Kristo alitusaidia kuhisi upendo wa Mungu katika maisha yetu?

Yohana 4:5–15

Mwokozi alikuwa anatufundisha nini alipofananisha injili Yake na maji ya uzima? Fikiria kunyanyua glasi ya maji na kuwataka familia yako kuelezea sifa za maji. Kwa nini tunahitaji kunywa maji kila siku? Kwa nini Yesu Kristo alikuwa amefananisha injili Yake na “chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele”? (Yohana 4:14).

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi.

Tafuta ishara. Maandiko daima hutumia vitu, matukio, matendo, au mafundisho kuwakilisha kweli za kiroho. Ishara hizi zinaweza kustawisha uelewa wako wa injili inayofundishwa. Kwa mfano, Mwokozi alifananisha uongofu na kuzaliwa tena.

Picha
Yesu na mwanamke Msamaria kisimani

Maji ya Uzima, na Simon Dewey

Chapisha