Njoo, Unifuate
Juni 17–23. Mathayo 27; Marko 15; Luka 23; Yohana 19: ‘Imekwisha’


“Juni 17–23. Mathayo 27; Marko 15; Luka 23; Yohana 19: ‘Imekwisha’’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2019)

“Juni 17–23. Mathayo 27; Marko 15; Luka 23; Yohana 19,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Kristo mbele ya Pilato

Ecce Homo, na Antonio Ciseri

Juni 17–23.

Mathayo 27; Marko 15; Luka 23; Yohana 19

“Imekwisha”

Mathayo 27; Marko 15; Luka 23; na Yohana 19 inajumuisha maelezo ya saa za mwisho za maisha ya Mwokozi duniani. Tafuta kuhisi upendo Wake kwako unapojifunza kuhusu dhabihu na kifo Chake.

Andika Misukumo Yako

Katika kila neno na tendo, Yesu Kristo alionyesha mfano wa upendo safi—kile Mtume Paulo alichokiita hisani (ona 1 Wakorintho 13). Hakuna muda hili lilikuwa wazi zaidi kuliko wakati wa saa za mwisho za maisha ya Mwokozi duniani. Utulivu wake wa heshima mbele ya mashitaka ya uongo uliashiria kwamba Yeye “hakuona uchungu” (1 Wakorintho 13:5). Utayari Wake kuvumilia mijeledi, mzaha, na kusulubiwa—hali akizuia nguvu Zake kusitisha mateso Yake—ilionyesha kwamba Yeye “alivumilia yote” na “kustahimili yote” (1 Wakorintho 13:4, 7). Huruma Yake kwa mama Yake na rehema Zake kwa watesi Wake—hata katika maumivu Yake yasiyo na kifani—ilionyesha kwamba Yeye “hakutafuta mambo [Yake] mwenyewe” (1 Wakorintho 13:5). Katika nyakati zake za mwisho duniani, Yesu alikuwa akifanya kile alichokifanya katika huduma Yake yote ya duniani—kutufundisha kwa kutuonyesha. Kwa kweli, hisani ni “upendo msafi wa Kristo” (Moroni 7:47).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Mathayo 27; Marko 15; Luka 23; Yohana 19

Utayari wa Yesu Kristo kuteseka unaonyesha upendo Wake kwa Baba na kwetu sisi sote.

Japokuwa Mwokozi alikuwa na nguvu ya kushusha chini “majeshi ya malaika” (Mathayo 26:53), Yeye kwa kujitolea alichagua kuvumilia hukumu zisizo za haki, mzaha wa kikatili, na maumivu ya mwili yasiyofikirika. Je, kwa nini alifanya hivyo? “Kwa sababu ya upendo Wake mkarimu,” Nefi alishuhudia, “na uvumilivu wake kwa watoto wa watu” (1 Nefi 19:9).

Unaweza kuanza kujifunza kwako juu ya saa za mwisho za Mwokozi kwa kusoma 1 Nefi 19:9. Je, ni wapi katika Mathayo 27; Marko 15; Luka 23; na Yohana 19 unapata mifano ya kila jambo ambalo Nefi alisema kuwa Yesu angeteseka?

“[Wana] mhukumu kuwa kitu cha bure”

“[Wana] mpiga mijeledi”

“Wanampiga”

“Wanamtemea mate”

Je, ni vifungu vipi hukusaidia kuhisi “upendo mkarimu” wa Baba wa Mbinguni na Yesu kwako? Je, ni zipi kati ya sifa zilizoonyeshwa na Mwokozi unashawishika kuzikuza zaidi?

Ona pia “Yesu Anahukumiwa mbele ya Pilato” na “Yesu Anapigwa mijeledi na Kusulubiwa” (video, LDS.org).

Mathayo 27:27–49, 54; Marko 15:16–32; Luka 23:11, 35–39; Yohana 19:1–5

Kufanyia mzaha ukweli wa Mungu hakupaswi kudhaifisha imani yangu.

Wakati Yesu alivumilia mzaha katika huduma Yake yote, ilikuwa kali zaidi wakati wa kupigwa Kwake mijeledi na Kusulubiwa. Lakini mzaha huu haungeweza kubadilisha ukweli: Yesu ni Mwana wa Mungu. Unaposoma kuhusu udhalilishaji Yesu aliovumilia, fikiria kuhusu upinzani na mzaha uliopo kwenye Kazi yake leo. Je, ni umaizi gani unapata kuhusu kuvumilia upinzani? Je, ni kitu gani kinakuvutia kuhusu maneno ya akida katika Mathayo 27:54?

Mathayo 27:46; Marko 15:34

Je, Baba wa Mbinguni alimuacha Yesu msalabani?

Mzee Jeffrey R. Holland alitoa umaizi ufuatao: “Ninashuhudia … kwamba Baba mkamilifu haku mwacha Mwanae katika saa ile. … Hata hivyo, ili kwamba ile dhabihu kuu ya Mwanae iweze kuwa kamilifu kama ilivyokuwa ya hiari na ya kipekee, Baba kwa muda mfupi alijiondoa kwa Yesu faraja ya Roho Wake, msaada wa uwepo Wake binafsi. … Ili Upatanisho wa [Mwokozi] uwe usio na mwisho na wa milele, Alitakiwa kujisikia jinsi inavyokuwa kufa sio tu kimwili bali kiroho, kuhisi jinsi inavyokuwa kuondokewa na Roho mtakatifu, akimuacha mtu akihisi mnyonge kabisa, mpweke asiye na tumaini” (“Hakuna Aliyekuwa Pamoja Naye,” Ensign au Liahona, Mei 2009, 87–88).

Luka 23:34

Mwokozi ndiye mfano wetu wa msamaha.

Je, unahisi vipi unaposoma maneno ya Mwokozi katika Luka 23:34? (ona umaizi uliotolewa na Tafsiri ya Joseph Smith katika tanbihi c). Akirejea maneno ya Mwokozi, Rais Henry B. Eyring alifundisha: “Tunapaswa kusamehe na kutoweka kinyongo dhidi ya wale wanaotukwaza. Mwokozi alionyesha mfano kutoka msalabani. … Sisi hatujui mioyo ya wale wanaotukwaza” (“Ili kwamba Tuwe Wamoja,” Ensign, Mei 1998, 68). Je, ni kwa jinsi gani mstari huu hukusaidia ukiwa na tatizo la kumsamehe mtu?

Luka 11:39–43

Je, nini maana ya “paradiso” katika kauli ya Mwokozi kwa yule mwizi?

Katika maandiko, neno paradiso kwa kawaida humaanisha “mahala pa amani na furaha katika ulimwengu wa roho baada ya kifo”—mahala walipoandaliwa wenye haki. Nabii Joseph Smith alifundisha kwamba neno paradiso katika Luka 23:43 “si tafsiri sahihi; Bwana hasa alisema kwamba yule mwizi angekuwa pamoja Naye katika ulimwengu wa roho” (Kweli kwa Imani, 111; ona pia Joseph Smith, Shajara, Juni 11, 1843, josephsmithpapers.org). Katika ulimwengu wa roho, mwizi angesikia injili ikihubiriwa.

Picha
ikoni ya kujifunza kwa familia

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Kwa Familia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko pamoja na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mapendekezo:

Mathayo 27:3–10

Ijapokuwa Yuda alimjua Yesu kibinafsi, ali “mgeuka [Yesu], na alikwazika kwa sababu ya maneno yake” (Tafsiri ya Joseph Smith, Marko 14:31 [katika Marko 14:10, tanbihi a]). Je, ni kitu gani kinaweza kuwafanya watu wanaoonekana kuwa na ushuhuda imara kumgeuka Mwokozi? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kubaki waaminifu kwa Yesu Kristo?

Mathayo 27:11–26; Marko 15:1–15; Luka 23:12–24; Yohana 19:1–16

Je, ni kwa nini Pilato alimtoa Yesu asulubiwe, japokuwa alijua kuwa Yesu hakuwa na hatia? Je, ni mafunzo gani tunayojifunza kutokana na uzoefu wa Pilato kuhusu kusimamia kile tunachojua ni sahihi? Inaweza kusaidia kwa familia yako kuigiza-matukio ambayo huwapa nafasi ya kujaribu kusimamia kile ambacho ni sahihi.

Picha
Kristo akibeba msalaba

“Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka … Golgotha” (Yohana 19:17).

Mathayo 27:46; Luka 23:34, 43, 46; Yohana 19:26–28, 30

Pengine unaweza kutoa kauli moja au zaidi za Mwokozi alizotoa msalabani, zinazopatikana katika mistari hii, kwa kila mwanafamilia na kuwaomba waelezee kile wanachojifunza kuhusu Mwokozi na huduma Yake.

Marko 3:39

Je, ni kwa jinsi gani kusoma kuhusu Kusulubiwa kumeimarisha shuhuda zetu kwamba Yesu ni “Mwana wa Mungu”?

Yohana 19:25–27

Je, tunajifunza nini kutoka katika mistari hii kuhusu jinsi tunavyopaswa kuwapenda na kuwasaidia wanafamilia?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Iga Maisha ya Mwokozi. Inasaidia kujifunza njia ambazo Mwokozi alifundisha—mbinu alizotumia na mambo aliyosema. Lakini nguvu za Mwokozi za kufundisha na kuwainua wengine zilikuja kutokana na … aina ya mtu Aliyekuwa. Kadiri unavyojitahidi kwa bidii kuishi kama Yesu Kristo, ndivyo utakavyoweza zaidi kufundisha kama Yeye” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 13).

Picha
Kristo msalabani

Kristo Msalabani, na Carl Heinrich Bloch

Chapisha