Njoo, Unifuate
Juni 3–9. Yohana 13–17: ‘Kaeni katika Pendo Langu’


“Juni 3–9. Yohana 13–17: ‘Kaeni katika Pendo Langu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2019)

“Juni 3–9. Yohana 13–17,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Chakula cha Mwisho

Kwa Ukumbusho Wangu, na Walter Rane

Juni 3–9.

Yohana 13:-17

“Kaeni katika Pendo Langu”

Unaposoma mafundisho ya Mwokozi katika Yohana 13–17, Roho Mtakatifu atakusaidia kutambua ujumbe ambao ni kwa ajili yako. Andika kumbukumbu ya misukumo unayopokea.

Andika Misukumo Yako

Leo tunaiita “Karamu ya Mwisho,” lakini hatujui kama wanafunzi wa Yesu waligundua kikamilifu, wakati walipokusanyika kwa ajili ya sherehe ya mwaka ya Pasaka, kwamba hiki kingekuwa chakula chao cha mwisho na Bwana wao kabla ya kifo Chake. Yesu, hata hivyo, “alijua kwamba saa yake imefika” (Yohana 13:1). Alikuwa karibu kupitia mateso ya Gethsemane, kusalitiwa na kukataliwa na marafiki Zake wa karibu, na kifo cha maumivu msalabani. Bado pamoja na vitisho vyote hivi mbele Yake, fokasi ya Yesu haikuwa Kwake bali katika kuwatumikia wanafunzi Wake. Yeye kwa unyenyekevu aliosha miguu yao. Aliwafundisha kuhusu upendo. Na aliwahakikishia tena kwamba, kwa namna fulani, Asingewaacha na hawakuhitaji Kumuacha. Wanafunzi wa kipindi kile na cha sasa hupata faraja katika ahadi Zake: “Sitawaacha ninyi yatima” (Yohana 14:18). “Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu” (Yohana 15:10).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Yohana 13–15

Ninaonyesha upendo wangu kwa Yesu Kristo kwa kushika amri Yake ya kupenda.

Yesu alikuwa tayari amefundisha kwamba amri mbili kuu zinahusika na upendo (ona Mathayo 22:34–40). Kwa kuendeleza msisitizo huu, upendo ulikuwa ni dhamira kuu ya maelekezo Yake ya mwisho kwa Mitume Wake. Unaposoma Yohana 13–15, unaweza kuandika au kuwekea alama kila matumizi ya neno upendo.

Unaweza kuona neno amri likirudiwa mara nyingi katika muingiliano na neno upendo katika sura hizi. Je, unaweza kujifunza nini kuhusu uhusiano kati ya upendo na amri kutoka kwenye mafundisho ya Mwokozi? Je, ni maneno gani mengine unayoyaona yamerudiwa mara nyingi pamoja na neno upendo katika sura hizi? Kufuatia kile unachojifunza, fikiria kuandika muhtasari wa mafundisho ya Mwokozi kuhusu upendo.

Ona pia D. Todd Christofferson, “Kaeni katika Pendo Langu,” Ensign au Liahona, Nov. 2016, 48–51.

Yohana 14–16

Roho Mtakatifu hunisaidia kutimiza lengo langu kama mfuasi wa Yesu Kristo.

Yesu Kristo alijua kuwa punde Angewaacha wanafunzi Wake, na Alijua wangehitaji msaada wa kiroho wakati atakapokuwa hayupo. Kwa kuwasaidia kuelewa jinsi gani wangepokea msaada huu, Aliwafundisha kuhusu Roho Mtakatifu. Je, wewe unajifunza nini kuhusu kazi za Roho Mtakatifu kutoka katika maneno ya Mwokozi kwenye mistari ifuatayo?

Je, ni kwa nini wanafunzi walihitaji aina hii ya msaada kutoka kwa Roho Mtakatifu? Je, ni kwa jinsi gani Roho Mtakatifu ametimiza kazi hizi katika maisha yako? Unapoendelea kujifunza Agano Jipya, tafuta njia ambazo kwazo Roho Mtakatifu aliwabariki wanafunzi wa Yesu. Je, ni kwa jinsi gani maisha yako yangekuwa tofauti kama ungemualika Roho Mtakatifu kukushawishi kwa kina zaidi?

Ona pia Mosia 3:19; 5:1–3; 3 Nefi 27:20; Moroni 8:25–26; 10:5; Mafundisho na Maagano 11:12–14; Musa 6:61; “Roho Mtakatifu,” Mada za Injili, topics.lds.org.

Yohana 15:1–8

Ninapokaa ndani ya Kristo, Nitazaa matunda mazuri.

Je, inaweza kumaanisha nini ku “kaa ndani ya [Kristo]”? (Yohana 15:4). Je, ni “tunda” gani huonyesha kwamba umeunganishwa kwenye mzabibu ambao humwakilisha Yesu Kristo?

Yohana 17

Yesu Kristo anaomba kwa ajili ya wanafunzi wake.

Maneno ya Yesu yaliyoandikwa kumbukumbu katika Yohana 17 yanajulikana kama Sala ya Maombezi. Katika sala hii, Yesu aliomba kwa ajili ya Mitume Wake na “wale watakaomuamini [Yeye] kwa sababu ya neno lao” (Yohana 17:20). Hiyo humaanisha Alikuwa akiomba kwa ajili yako. Je, Yesu aliomba nini kutoka kwa Baba Yake kwa niaba yako na waaminio wengine wote?

Sala hii pia hufundisha kweli za ndani, za milele. Je, ni ukweli gani unapata unaposoma?

Yohana 17:11, 21–23

Je, ni kwa jinsi gani Yesu Kristo na Baba wa Mbinguni ni wamoja?

Kwenye sala Yake katika Yohana 17, Yesu alisisitiza umoja Wake na Baba, lakini hii haimaanishi kwamba Yeye na Baba Yake ni mtu mmoja. Wakati Mwokozi alipoomba kwamba wanafunzi Wake wawe na umoja “kama vile”—au katika njia sawa ambayo—Yeye na Baba Yake ni wamoja (Yohana 17:22), Hakuwa akiomba kwamba wanafunzi wawe mtu mmoja. Bali, hamu Yake ilikuwa kwamba wafurahie umoja kama ule Alionao na Baba—umoja mkamilifu wa lengo, moyo, na mawazo.

Picha
Ikoni ya kujifunza kwa familia

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Kwa Familia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mapendekezo:

Yohana 13:1–17

Je, familia yetu inajifunza nini kutoka kwenye mfano wa Mwokozi katika mistari hii? Je, ni kwa njia zipi tunaweza kufuata mfano Wake?

Yohana 13:34–35; 15:9–14

Unapojadili mafundisho ya Mwokozi kuhusu upendo, fikiria pia maneno haya kutoka kwa Rais Thomas S. Monson: “Katika ulimwengu wa leo, hakuna mahali msingi huo wa mwamba wa upendo unahitajika zaidi kuliko nyumbani. Na hakuna mahali ambapo ulimwengu unapaswa kupata mfano bora wa msingi huo kuliko majumbani mwa Watakatifu wa Siku za Mwisho ambao wamefanya upendo kuwa moyo wa maisha ya familia zao. … Upendo ndiyo hasa kiini cha injili, sifa bora zaidi ya nafsi ya mwanadamu” (“Kama Nilivyowapenda Ninyi,” Ensign au Liahona, Feb. 2017, 4–5).

Wanafamilia wako wanaweza kufurahia kuchora picha au kuandika katika karatasi zenye umbo la moyo kitu wanachopenda kuhusu wao kwa wao. Wanaweza kuweka mioyo hii kuzunguka nyumba kama ukumbusho wa kuonyesha upendo kwa kila mmoja.

Yohana 15:1–8

Inaweza kuwa ya kufurahisha kusoma mistari hii nje karibu na mzabibu, mti, au mmea mwingine. Je, ni kwa jinsi gani shughuli hii husaidia wanafamilia wako kuelewa vizuri zaidi mafundisho ya Mwokozi?

Picha
zabibu kwenye mzabibu.

Yesu alifundisha, “Mimi ni mzabibu, ninyi ni matawi” (Yohana 15:5).

Yohana 15:17–27; 16:1–7

Je, ni kwa nini unafikiri Yesu Kristo aliwaonya wanafunzi Wake juu ya mateso? Je, ni kwa jinsi gani wafuasi wa Kristo wanateswa leo? Je, ni kwa jinsi gani ushauri wa Mwokozi katika mistari hii hutusaidia wakati tunapopata mateso?

Yohana 16:33.

Je, ni kwa jinsi gani Kristo ameushinda ulimwengu? Je, ni kwa jinsi gani Upatanisho Wake umetuletea amani na furaha? (ona pia M&M 68:6).

Yohana 17:21–23

Je, ni kwa jinsi gani familia yetu inaweza kuwa na umoja zaidi kama Yesu Kristo na Baba wa Mbinguni walivyo na umoja? Je, ni kwa nini Bwana anataka sisi tuwe na umoja? (ona pia M&M 38:27).

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia rekodi ya kusikiliza. Unapowafundisha familia yako maandiko, fikiria kusikiliza kutoka katika toleo la kusikiliza la maandiko, linalopatikana kwenye LDS.org au Gospel Library app. Kusikiliza kutoka Yohana 13–17 kunaweza kuwa hasa na nguvu kwa sababu sura hizi zina maneno mengi ya Mwokozi.

Picha
Yesu akiosha miguu ya Mitume

Bwana Mtumwa, na Del Parson

Chapisha