Njoo, Unifuate
Agosti 19–25. 1 Wakorintho 1–7: ‘Muwe Katika Nia Moja’


“Agosti 19–25. 1 Wakorintho 1–7: “Muwe Katika Nia Moja’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2019)

Agosti 19–25. 1 Wakorintho 1–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Korintho

Korintho, Kusini mwa Ugiriki, mahali palipo na ofisi na majengo ya baraza, picha na Balage Balogh

Agosti 19–25.

1 Wakorintho 1–7

“Muwe Katika Nia Moja”

Andika misukumo yako unaposoma 1 Wakorintho 1–7. Misukumo hiyo inaweza kujumuisha ushawishi wa kujifunza wazo fulani zaidi, kushiriki na wengine kitu unachojifunza, au kufanya mabadiliko katika maisha yako.

Andika Misukumo Yako

Kipindi cha miezi ambayo Paulo alikaa Korintho, “Wakorintho wengi waliomsikia waliamini, na kubatizwa” (Matendo ya Mitume 18:8). Hivyo ilikuwa ya kuumiza moyo kwa Paulo kusikia, miaka michache tu baadaye, kwamba kulikuwa na “faraka” na “fitina” miongoni mwa Watakatifu wa Korintho na kwamba katika kutokuwepo kwake walianza kusikiliza “hekima ya dunia hii” (1 Wakorintho 1:10–11, 20). Katika kujibu, Paulo aliandika barua ambayo sasa tunaiita 1 Wakorintho. Imejaa mafundisho mazito, na bado wakati huo huo, Paulo alionekana kusikitishwa kwamba Watakatifu hawakuwa tayari kupokea mafundisho yote aliyotaka kuwapa. “Ndugu zangu, mimi, sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni,” aliomboleza, “kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini” (1 Wakorintho 3:1–3). Tunapojiandaa kusoma maneno ya Paulo, itakuwa yenye kusaidia kujitathmini wenyewe utayari wetu kuipokea kweli—ikiwemo utayari wetu kumsikiliza Roho na kuutafuta umoja ndani ya familia zetu, na Watakatifu wenzetu, na Mungu.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

1 Wakorintho 1:10–17; 3:1–11

Waumini wa Kanisa la Kristo wana umoja.

Hatujui maelezo yote kuhusu kutokuwepo kwa umoja kati ya Watakatifu wa Korintho, lakini tunajua kuhusu kutokuwepo kwa umoja katika uhusiano wetu wenyewe. Fikiria kuhusu uhusiano katika maisha yako ambao ungeweza kunufaika kutokana na umoja zaidi; kisha tafuta Paulo alifundisha nini katika 1 Wakorintho 1:10–17; 3:1–11 kuhusu kutokuwepo umoja miongoni mwa Watakatifu wa Korintho. Je, ni utambuzi gani unaweza kupata kuhusu jinsi ya kuendeleza umoja mkubwa zaidi na wengine”

Ona pia Mosia 18:21; 4 Nefi 1:15–17; Mafundisho na Maagano 38:23–27; 105:1–5; “Umoja,” Mada za Injili, topics.lds.org.

1 Wakorintho 1:17–312

Ili kuikamilisha kazi ya Mungu, ninahitaji hekima ya Mungu.

Wakati ni vizuri—na hata tunatiwa moyo—kutafuta hekima popote tunapoweza kuipata (ona 2 Nefi 9:29; M&M 88:118), Paulo alitoa maonyo yenye maneno makali kuhusu hekima ya mwanadamu yenye dosari, ambayo aliiita “hekima ya ulimwengu huu.” Unaposoma 1 Wakorintho 1:17–25, tafakari kirai hiki kinaweza kumaanisha nini. Je, unafikiri Paulo alimaanisha nini kwa “hekima ya Mungu”? Kwa nini tunahitaji hekima ya Mungu ili kukamilisha kazi ya Mungu?

Katika jitihada zako za kutimiza majukumu yako katika kuikamilisha kazi ya Mungu, je, umewahi kupata “hofu, na … kutetemeka kwingi” ambako Paulo alihisi alipokuwa akiwafundisha Watakatifu wa Korintho? (1 Wakorintho 2:3). Je, unapata nini katika mstari 1–5 ambacho hukupa ujasiri? Fikiria jinsi gani unaweza kuonyesha kwamba unaamini “nguvu za Mungu” kuliko “hekima ya mwanadamu.”

ona pia Mafundisho na Maagano 1:17–28.

1 Wakorintho 2:9–16

Ninamhitaji Roho Mtakatifu ili kuelewa mambo ya Mungu.

Kama ungetaka kujifunza zaidi kuhusu kitu kama fundi wa magari au usanifu wa majengo ya zamani, ni kwa jinsi gani ungefanya hilo? Kulingana na 1 Wakorintho 2:9–16, ni kwa jinsi gani kujifunza “mambo ya Mungu” kunatofautiana na kujifunza “mambo ya mwanadamu”? Kwa nini ni lazima tuwe na Roho Mtakatifu ili kuelewa mambo ya Mungu? Baada ya kusoma mistari hii, ni nini unahisi unapaswa kufanya ili kuelewa mambo ya kiroho kikamilifu zaidi? Ni kwa jinsi gani maneno ya Paulo yanaweza kumsaidia mtu anayehangaika na ushuhuda wake?

1 Wakorintho 6:13–20

Mwili wangu ni mtakatifu.

Watu wengi katika Korintho walihisi kwamba uzinzi na uasherati ulikubalika na kwamba miili yao ilikuwa imetengenezwa hasa kwa ajili ya anasa. Kwa maneno mengine, Korintho haikuwa tofauti sana na ulimwengu wa leo. Je, Paulo alifundisha nini katika 1 Wakorintho 6:13–20 ambacho kinaweza kukusaidia kuwaelezea wengine kwa nini unataka kuishi maisha ya usafi kimwili?

Inaweza kuwa pia ya kuvutia kuona jinsi gani Dada Wendy W. Nelson, kama Paulo, aliwatia moyo Watakatifu kuwa wasafi kimwili katika hotuba yake “Mapenzi na Ndoa” (Worldwide Devotional for Young Adults, Jan. 8, 2017, broadcasts.lds.org). Ni kwa jinsi gani kweli kuhusu mapenzi na kujamiana zilizoelezewa na Dada Nelson zinatofautiana na ujumbe wa ulimwengu?

Ona pia Warumi 1:24–27; “Usafi wa kimwili,” Mada za Injili, topics.lds.org.

1 Wakorintho 7:29–33

Je, Paulo alifundisha kwamba ni bora kutokuoa kuliko kuoa?

Mistari kadhaa katika 1 Wakorintho 7 inaonekana kupendekeza kwamba wakati ndoa inakubalika, kubaki bila mwenzi na kujiondoa kabisa kutoka kwenye uhusiano ya kimapenzi ni bora. Hata hivyo, Tafsiri ya Joseph Smith, 1 Wakorintho 7:29–33 (ona kiambatisho cha Biblia) hutusaidia kuelewa kwamba Paulo alikuwa akiwaongelea wale walioitwa kuwa wamisionari, akionelea kwamba walikuwa na uwezo wa kumtumikia Mungu vizuri zaidi kama wangebaki pasipo mwenzi wakati wa misheni zao. Bwana amefundisha kupitia watumishi Wake, akiwemo Paulo, kwamba ndoa ni sehemu ya mpango Wake wa milele na muhimu kwa ajili ya kuinuliwa (ona 1 Wakorintho 11:11; M&M 131:1–4).

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Hapa kuna baadhi ya mapendekezo:

1 Wakorintho 1:10–17; 3:1–11

Familia yako inaposoma mistari hii, waalike kutafuta utambuzi unaoweza kuwasaidia kuwa na umoja zaidi.

1 Wakorintho 3:1–2

Labda mnaweza kusoma mistari hii wakati mkipata asusa ya maziwa na nyama, na mnaweza kulinganisha jinsi watoto wanavyokua kufikia kwenye utu uzima na jinsi tunavyokua kiroho.

1 Wakorintho 3:4–9

Paulo alifananisha jitihada zake za umisionari na kupanda mbegu. Je, kulinganisha kwake hupendekeza nini kuhusu jinsi tunavyopaswa kuikabili dhana ya kuhubiri injili kwa wengine?

1 Wakorintho 6:19–20

Kulinganisha miili yetu na mahekalu, kama Paulo alivyofanya, kunaweza kuwa njia ifaayo kufundisha kuhusu utakatifu wa miili yetu. Pengine unaweza kuonyesha picha za mahekalu, kama vile zile zinazoambatana na muhtasari huu. Kwa nini mahekalu ni matakatifu? Ni kwa jinsi gani miili yetu ni kama mahekalu? Je, tunaweza kufanya nini kuitendea miili yetu kama mahekalu? (Ona “Usafi wa Kimwili,” Kwa Nguvu ya Vijana, 35–37.) Ikiwezekana, nendeni hekaluni pamoja au tembeleeni maeneo ya nje ya hekalu; hii inaweza kuboresha majadiliano yenu kuhusu utakatifu wa hekalu na wa miili yetu.

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Kuwa mvumilivu kwako mwenyewe. Paulo alifundisha kwamba maziwa huja kabla ya nyama wakati tunapojifunza injili (ona 1 Wakorintho 3:1–2). Ukikuta kwamba baadhi ya mafundisho ni magumu kuelewa sasa, kuwa mvumilivu. Amini kwamba majibu yatakuja unapokuwa na imani na kujifunza kwa bidii.

Picha
mahekalu manne

Paulo alifananisha miili yetu na utakatifu wa hekalu. Kwa mzunguko wa kisaa kutoka juu kushoto: Hekalu la Tijuana Mexico, Hekalu la Taipei Taiwan, Hekalu la Tegucigalpa Honduras, Hekalu la Houston Texas.

Chapisha