Njoo, Unifuate
Agosti 19–25. 1 Wakorintho 1–7: ‘Muwe Katika Nia Moja’


“Agosti 19–25, 1 Wakorintho 1–7: ‘Muwe Katika Nia Moja’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2019 (2019)

“Agosti 19–25. 1 Wakorintho 1–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
Korintho

Korintho, Ugiriki Kusini, Jukwaa na Kituo cha Uraia, uchoraji na Balage Balogh

Agosti 19–25

1  Wakorintho 1–7

“Muwe Katika Nia Moja”

Roho Mtakatufu atakusaidia kujua kanuni zipi za injili katika 1 Wakorintho 1–7 zitawasaidia watoto unaowafundisha. Unaposoma sura hizi kwa maombi, andika mawazo na hisia ambazo zinakuja kwako kutoka kwa Roho.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Siku chache kabla, mwalike mtoto mmoja au zaidi kutafuta aya katika 1 Wakorintho 1–7 ambazo wataweza kushiriki pamoja na darasa. Unaweza kuwaalika wazazi wao kusaidia ikibidi.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

1 Wakorintho 2:11–14

Roho Mtakatifu ananifundisha kweli za injili.

Mojawapo ya majukumu ya Roho Mtakatifu ni kutufundisha ukweli. Ni uzoefu gani unaoweza kushiriki pamoja na watoto ili kuwasaidia kuelewa hili?

Shughuli Yamkini

  • Onyesha vitu au picha ambazo zinaonesha njia tunazojifunza kuhusu ulimwengu (kama vile shule, kitabu, au simu ya kiganjani). Tunaweza kujifunza nini tunapotumia vitu hivi? Eleza kwamba katika 1 Wakorintho 2:11 14, Paulo alifundisha kwamba tunaweza kujifunza kuhusu Mungu kupitia Roho wa Mungu pekee, ambaye ni Roho Mtakatifu. Je, tunaweza kufanya nini ili kujifunza “mambo ya Mungu”?

  • Piga makofi unaposema kila silabi katika sentensi “Roho Mtakatifu anatufundisha ukweli.” Waombe watoto kupiga makofi na kurudia kirai hicho. Shiriki na watoto uzoefu wako wakati Roho Mtakatifu alipokusaidia kujua kwamba kitu fulani ni cha kweli.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu Roho Mtakatifu, kama vile “Roho Mtakatifu” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 105 ). Wasaidie watoto kutafuta maneno na virai katika wimbo ambao unafundisha jinsi Roho Mtakatifu husema nasi na kile anachotufundisha sisi.

1 Wakorintho 3:10–11

Yesu Kristo ni msingi wangu.

Watoto wanaweka msingi kwa ajili ya shuhuda zao, na unaweza kuwasaidia kujenga msingi imara juu ya Yesu Kristo.

Shughuli Yamkini

  • Soma 1 Wakorintho 3:11 kwa watoto, na eleza kwamba Yesu Kristo ni msingi wetu. Onyesha watoto picha kadhaa za vitu tunavyoweza kuwa na shuhuda zake, ikijumuisha picha ya Yesu Kristo. Wasaidie kuzipanga picha ili kwamba picha ya Yesu iwe chini, kama msingi, na picha zingine “zinajenga” juu ya ushuhuda Wake.

  • Tengeneza vitendo kwa wimbo “Mtu Mwenye Hekima na Mtu Mpumbavu” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 281, na imba wimbo huo pamoja na watoto. Mpatie kila mtoto jiwe lililoandikwa juu yake “Yesu Kristo ni msingi wangu.” Waache wachukuwe mawe hayo nyumbani ili yawakumbushe kile walichojifunza.

  • Shiriki picha ambazo zinafafanua baadhi ya hadithi unazozipenda kutoka maisha ya Mwokozi, na waombe watoto wakuambie nini kinatokea katika picha. Waache wasimuliane baadhi ya hadithi zao wanazozipenda kuhusu Yesu. Toa ushuhuda wako kwamba Yesu Kristo ni msingi wa imani yako.

1 Wakorintho 6:19

Mwili wangu ni kama hekalu.

Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto kuthamini miili yao kama zawadi kutoka kwa Mungu na kuwa na matamanio makubwa ya kuitunza?

Shughuli Yamkini

  • Onyesha watoto picha za mahekalu (ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia.), na soma maneno haya kutoka 1 Wakorintho 6:19: “Miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu.” Wasaidie watoto kuelewa kwamba Baba wa Mbinguni anatutaka sisi kuitunza miili yetu iwe safi na mitakatifu, kama hekalu.

  • Onyesha picha ya mtoto, na uweke picha kuzunguka picha hiyo ya vitu ambavyo ni vizuri kwa miili yetu na vitu ambavyo ni vibaya. Waalike watoto kuchukuwa zamu kutambua vitu vizuri na kuviondoa vile vibaya.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu miili, kama vile “Kichwa, Mabega, Magoti, na Vidole” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 275), na waulize watoto kwa nini wanashukrani kwa ajili ya miili yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

1 Wakorintho 1:23–25

Mungu ana busara zaidi ya binadamu, na ninaonesha busara ya kweli ninapoamini mafundisho Yake.

Watoto unaowafundisha watapata—kama hawajapata bado—kwamba baadhi ya watu wanafundisha vitu ambavyo kinyume na busara ya Mungu. Kujifunza 1 Wakorintho 1:23–25 kunaweza kuwasaidia watoto kuelewa kwamba Mungu ni mwenye busara kuliko binadamu.

Shughuli Yamkini

  • Someni 1 Wakorintho 1:23–25 pamoja, na wasaidie watoto kutafuta maneno busara na upumbavu. Eleza kwamba watu wengi walifikiri mafundisho ya Paulo yalikuwa ya kijinga, lakini Paulo Alielezea kwamba kuamini injili ya Kristo ni busara ya kweli. Kwa nini ni busara kuamini kile Mungu anachofundisha?

  • Wasaidie watoto waigize jinsi wanavyoweza kuwajibu watu wanaofikiri mafundisho ya Kanisa ni ya “kijinga”—mafundisho kama vile kuamini katika Mwokozi, kutii Neno la Hekima, au kutii sheria ya zaka. Kwa mfano, wanaweza kushuhudia juu ya baraka ambazo zinakuja kutokana na kuishi mafundisho haya.

  • Elezea uzoefu wako ambapo watu wengine walifikiri kwamba imani zako zilikuwa ujinga, au shiriki mfano kutoka kwenye maandiko. Watoto nao wanaweza kushiriki uzoefu unaofanana na huo? Je, ni kwa jinsi gani 1 Wakorintho 1:25 inaweza kutusaidia kubaki waaminifu wakati wengine wanaita imani zetu ujinga?

1 Wakorintho 2:11–14

Roho Mtakatifu ananifundisha ukweli wa injili.

Unawezaje kuwasaidia watoto kutambua kwamba wanamhitaji Roho Mtakatifu ili kuelewa “mambo ya Mungu”?

Shughuli Yamkini

  • Tengeneza orodha ya njia tunazojifunza kuhusu ulimwengu—kwa mfano, vitabu, shule, na mtandao. Kisha someni pamoja 1 Wakorintho 2:11–14. Aya hizi zinafundisha nini kuhusu jinsi tunavyojifunza “mambo ya Mungu”?

  • Waalike watoto kushiriki muda ambao walihisi ushawishi wa Roho Mtakatifu, pia anaitwa “Roho wa Mungu” (1 Wakorintho 2:11–14). Muda kama huu ungeweza kujumuisha na wakati walipokuwa kanisani, wakisali, au kusoma maandiko. Wasaidie kuelewa kwamba Roho Mtakatifu alikuwa anawafundisha ukweli, kama Paulo alivyoeleza.

  • Mwalike kila mtoto kusoma mojawapo ya maandiko haya: 1 Wakorintho 2:11–14; 1 Nefi 10:17; Moroni 10:3–5; na Mafundisho na Maagano 8:2–3. Waombe watoto kushiriki kile walichojifunza kutoka katika mafundisho haya kuhusu jinsi Roho Mtakatifu anavyotufundisha. Watie moyo kuandika marejeo haya pembezoni mwa maandiko yao.

1 Wakorintho 6:19–20

Sina budi kuushughulikia mwili wangu kwa heshima na kuuweka mtakatifu.

Kuelewa kwamba miili yetu ni zawadi kutoka kwa Baba wa Mbinguni itawasaidia watoto kuweka miili yao mitakatifu, hata kama watajaribiwa kufanya vinginevyo.

Shughuli Yamkini

  • Leta zawadi iliyofungwa na picha ya mtoto na hekalu ndani. Waalike watoto wasome 1 Wakoritho 6:19–20 na wabahatishe kilichopo ndani ya zawadi. Waache wafungue zawadi na mjadili ni kwa jinsi gani miili yetu ni kama mahekalu.

  • Zungumza na watoto kuhusu jinsi tutakavyochukulia hekalu. Kama miili yetu ni kama mahekalu, jinsi gani tunapaswa tuichukulie miili yetu? Kuimba au kusoma maneno ya wimbo kuhusu mahekaku, kama vile “The Lord Gave Me a Temple” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 153), kunaweza kusaidia kujibu swali hili. Wakati tumapofanya makosa, ni kwa jinsi gani tunaweza kuyafanya “mahekalu” yetu kuwa safi tena?

  • Someni pamoja sehemu yenye jina “Afya ya Kimwili na Kihisia” katika Kwa Nguvu ya Vijana (2011, 25–27). Waalike watoto kuorodhesha ubaoni ushauri wanaoupata kuhusu jinsi ya kulinda miili yetu.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki pamoja na familia zao wimbo ambao waliuimba katika darasa na kile walichojifunza kutokana na wimbo huo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Shuhudia juu ya Yesu Kristo. Mojawapo ya mambo muhimu unayoweza kufanya kama mwalimu ni kushuhudia juu ya Yesu Kristo. Hii itawasaidia watoto kuimarisha shuhuda zao na kuhisi upendo wa Mwokozi kwa ajili yao.

Chapisha