Agano Jipya 2023
Agosti 21–27. 1 Wakorintho 1–7: “Muunganishwe Pamoja kwa Ukamilifu”


“Agosti 21–27. 1 Wakorintho 1–7: “Muunganishwe Pamoja kwa Ukamilifu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2023)

Agosti 21–27. 1 Wakorintho 1–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
Korintho ya kale

Korintho, Kusini mwa Ugiriki, Kituo cha Baraza na Jiji, mchoro na Balage Balogh Balogh/www.ArchaeologyIllustrated.com

Agosti 21–27

1 Wakorintho 1–7

“Muunganishwe Pamoja kwa Ukamilifu”

Andika misukumo yako unaposoma 1 Wakorintho 1–7. Misukumo hii inaweza kujumuisha ushawishi wa kujifunza zaidi wazo fulani, kushiriki na wengine kitu unachojifunza, au kufanya mabadiliko katika maisha yako.

Andika Misukumo Yako

Kipindi cha miezi ambayo Paulo alikaa Korintho, “Wakorintho wengi waliomsikia waliamini, na kubatizwa” (Matendo 18:8). Hivyo ilikuwa ya kuumiza moyo kwa Paulo kusikia, miaka michache tu baadaye, kwamba kulikuwa na “faraka” na “fitina” miongoni mwa Watakatifu wa Korintho na kwamba katika kutokuwepo kwake walianza kusikiliza “hekima ya ulimwengu huu” (1 Wakorintho 1:10–11,20). Katika kujibu, Paulo aliandika barua ambayo sasa tunaiita 1 Wakorintho. Imejaa mafundisho mazito, na bado wakati huo huo, Paulo alionekana kusikitishwa kwamba Watakatifu hawakuwa tayari kupokea mafundisho yote aliyotaka kuwapa. “Ndugu zangu, mimi, sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni,” aliomboleza, “kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini” (1 Wakorintho 3:1–3). Tunapojiandaa kusoma maneno ya Paulo, itakuwa yenye kusaidia kujitathmini wenyewe utayari wetu kuipokea kweli—ikiwemo utayari wetu kumsikiliza Roho na kuutafuta umoja ndani ya familia zetu, kwa Watakatifu wenzetu, pamoja na Mungu.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

1 Wakorintho 1:10–17; 3:1–11

Waumini wa Kanisa la Kristo wanajitahidi kuwa na umoja.

Hatujui maelezo yote kuhusu kutokuwepo kwa umoja miongoni mwa Watakatifu wa Korintho, lakini tunajua kuhusu kutokuwepo kwa umoja katika uhusiano wetu wenyewe. Fikiria kuhusu uhusiano katika maisha yako ambao ungeweza kunufaika kutokana na umoja zaidi; kisha tafuta kile Paulo alichofundisha katika 1 Wakorintho 1:10–17; 3:1–11 kuhusu kutokuwepo kwa umoja miongoni mwa Watakatifu wa Korintho. Je, ni umaizi gani unaweza kuupata kuhusu jinsi ya kuendeleza umoja mkubwa zaidi kwa wengine?

Ona pia Mosia 18:21; 4 Nefi 1:15–17; Mafundisho na Maagano 38:23–27; 105:1–5; Mada za Injili “Umoja,” topics.ChurchofJesusChrist.org.

1 Wakorintho 1:17–31;2

Ili kuitimiza kazi ya Mungu, ninahitaji hekima ya Mungu.

Wakati ni vizuri—na hata tunatiwa moyo—kutafuta hekima popote tunapoweza kuipata (ona 2 Nefi 9:29; Mafundisho na Maagano 88:118), Paulo alitoa maonyo yenye maneno makali kuhusu hekima ya mwanadamu yenye dosari, ambayo aliiita “hekima ya ulimwengu huu.” Unaposoma 1 Wakorintho 1:17–25, tafakari kirai hiki kinaweza kumaanisha nini. Je, unafikiri Paulo alimaanisha nini kwa “hekima ya Mungu”? Kwa nini tunahitaji hekima ya Mungu ili kutimiza kazi ya Mungu?

Katika jitihada zako za kutimiza majukumu yako katika kuitimiza kazi ya Mungu, je, umewahi kupata “hofu, na … kutetemeka kwingi” ambako Paulo alihisi alipokuwa akiwafundisha Watakatifu wa Korintho? (1 Wakorintho 2:3). Je, unapata nini katika 1 Wakorintho 2:1–5 ambacho hukupa wewe ujasiri? Fikiria jinsi gani unaweza kuonyesha kwamba unaamini “nguvu za Mungu” kuliko “hekima ya mwanadamu.”

Ona pia Mafundisho na Maagano 1:17–28.

1 Wakorintho 2:9–16

Ninamhitaji Roho Mtakatifu ili kuelewa mambo ya Mungu.

Kama ungetaka kujifunza zaidi kuhusu kitu kama ufundi wa magari au usanifu wa majengo ya zamani, ni kwa jinsi gani ungefanya hilo? Kulingana na 1 Wakorintho 2:9–16, ni kwa jinsi gani kujifunza “mambo ya Mungu” kunatofautiana na kujifunza “mambo ya mwanadamu”? Kwa nini ni lazima tuwe na Roho Mtakatifu ili kuelewa mambo ya Mungu? Baada ya kusoma mistari hii, ni nini unahisi unapaswa kufanya ili kuelewa mambo ya kiroho kikamilifu zaidi? Ni kwa jinsi gani maneno ya Paulo yanaweza kumsaidia mtu anayehangaika na ushuhuda wake?

1 Wakorintho 6:13–20

Mwili wangu ni mtakatifu.

Watu wengi katika Korintho walihisi kwamba uzinzi na uasherati ulikubalika na kwamba miili yao ilikuwa imetengenezwa hasa kwa ajili ya anasa. Kwa maneno mengine, Korintho haikuwa tofauti sana na ulimwengu wa leo. Je, Paulo alifundisha nini katika 1 Wakorintho 6:13–20 ambacho kinaweza kukusaidia kuwaelezea wengine kwa nini unataka kuishi maisha ya usafi kimwili?

Kama Paulo, Dada Wendy W. Nelson aliwahimiza Watakatifu kuwa wasafi kimwili, ona ujumbe wake “Upendo na Ndoa” (worldwide devotional for young adults, Jan. 8, 2017, broadcasts.ChurchofJesusChrist.org). Kulingana na Dada Nelson, ni baraka gani huja kutokana na kuishi viwango vya Bwana kuhusu upendo na mahusiano ya kimapenzi?

1 Wakorintho 7:29–33

Je, Paulo alifundisha kwamba ni bora kutokuoa kuliko kuoa?

Mistari kadhaa katika 1 Wakorintho 7 inaonekana kupendekeza kwamba wakati ndoa inakubalika, kubaki bila mwenzi na kujiondoa kabisa kutoka kwenye uhusiano wa kimapenzi ni bora. Hata hivyo, Tafsiri ya Joseph Smith, 1 Wakorintho 7:29–33 (katika kiambatisho cha Biblia) hutusaidia kuelewa kwamba Paulo alikuwa akiwaongelea wale walioitwa kuwa wamisionari, akionelea kwamba walikuwa na uwezo wa kumtumikia Mungu vizuri zaidi kama wangekuwa waseja wakati wa misheni zao. Bwana amefundisha kupitia watumishi Wake, akiwemo Paulo, kwamba ndoa ni sehemu ya mpango Wake wa milele na muhimu kwa ajili ya kuinuliwa (ona 1 Wakorintho 11:11; Mafundisho na Maagano 131:1–4).

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

1 Wakorintho 1:10–17; 3:1–11.Familia yako inaposoma mistari hii, waalike kutafuta umaizi unaoweza kuwasaidia kuwa na umoja zaidi.

1 Wakorintho 3:1–2.Labda mngeweza kusoma mistari hii wakati mkinywa maziwa na kula nyama. Unaweza kulinganisha jinsi watoto wanavyokua kufikia kwenye utu uzima na jinsi tunavyokua kiroho.

1 Wakorintho 3:4–9.Paulo alifananisha jitihada zake za umisionari na kupanda mbegu. Je, kufananisha kwake kunatufundisha nini kuhusu kushiriki injili?

1 Wakorintho 6:19–20.Kulinganisha miili yetu na mahekalu, kama Paulo alivyofanya, kunaweza kuwa njia ifaayo kufundisha kuhusu utakatifu wa miili yetu. Pengine unaweza kuonyesha picha za mahekalu, kama vile zile zinazoambatana na muhtasari huu. Kwa nini mahekalu ni matakatifu? Ni kwa jinsi gani miili yetu ni kama mahekalu? Je, tunaweza kufanya nini kuitendea miili yetu kama mahekalu? (Ona pia toleo maalumu la Agosti 2020 la Liahona kuhusu ujinsia.)

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “The Lord Gave Me a Temple,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 153.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Kuwa mvumilivu kwako mwenyewe. Paulo alifundisha kwamba maziwa huja kabla ya nyama wakati tunapojifunza injili (ona 1 Wakorintho 3:1–2). Ukikuta kwamba baadhi ya mafundisho ni magumu kuelewa sasa, kuwa mvumilivu. Amini kwamba majibu yatakuja unapokuwa na imani na kujifunza kwa bidii.

Picha
mahekalu manne

Paulo alifananisha miili yetu na utakatifu wa hekalu. Kwa mzunguko wa saa kutoka juu kushoto: Hekalu la Tijuana Mexico, Hekalu la Taipei Taiwan, Hekalu la Tegucigalpa Honduras, Hekalu la Houston Texas.

Chapisha