Agano Jipya 2023
Agosti 21–27. 1 Wakorintho 1–7: “Muunganishwe Pamoja kwa Ukamilifu”


“Agosti 21–27, 1 Wakorintho 1–7: ‘Muunganishwe Pamoja kwa Ukamilifu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2023 (2022)

“Agosti 21–27. 1 Wakorintho 1–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2023

Picha
Korintho ya kale

Korintho, Ugiriki ya Kusini, Baraza na Kitovu cha Jiji, mchoro na Balage Balogh/www.ArchaeologyIllustrated.com

Agosti 21–27

1 Wakorintho 1–7

“Muunganishwe Pamoja kwa Ukamilifu”

Roho Mtakatufu atakusaidia kujua kanuni zipi za injili katika 1 Wakorintho 1–7 zitawasaidia watoto unaowafundisha. Unaposoma sura hizi kwa maombi, andika mawazo na hisia ambazo zinakuja kwako kutoka kwa Roho.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waulize watoto kama walishiriki na familia zao kitu walichojifunza katika darasa la msingi wiki iliyopita. (Unaweza kuhitaji kwa kifupi kurejea somo la wiki iliyopita.) Kama ni hivyo, walishiriki nini?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

1 Wakorintho 2:11–14

Roho Mtakatifu ananifundisha kweli za injili.

Mojawapo ya majukumu ya Roho Mtakatifu ni kutufundisha ukweli. Ni uzoefu gani unaoweza kushiriki pamoja na watoto ili kuwasaidia kuelewa hili?

Shughuli Yamkini

  • Onyesha vitu au picha ambazo zinaonesha njia tunazojifunza kuhusu ulimwengu (kama vile shule, kitabu au simujanja). Tunaweza kujifunza nini tunapotumia vitu hivi? Eleza kwamba katika 1 Wakorintho 2:11, 14, Paulo alifundisha kwamba tunaweza kujifunza kuhusu Mungu kupitia Roho wa Mungu pekee, ambaye ni Roho Mtakatifu. Je, tunaweza kufanya nini ili kujifunza “mambo ya Mungu”?

  • Piga makofi unaposema kila silabi katika sentensi “Roho Mtakatifu anatufundisha ukweli.” Waombe watoto kupiga makofi na kurudia kirai hicho. Shiriki na watoto uzoefu wako wakati Roho Mtakatifu alipokusaidia kujua kwamba kitu fulani ni cha kweli.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu Roho Mtakatifu, kama vile “Holy Ghost” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 105). Wasaidie watoto kutafuta maneno na virai katika wimbo ambavyo vinafundisha jinsi Roho Mtakatifu husema nasi na kile anachotufundisha sisi.

1 Wakorintho 3:10–11

Yesu Kristo ni msingi wangu.

Watoto wanaweka msingi kwa ajili ya shuhuda zao, na unaweza kuwasaidia kujenga msingi imara juu ya Yesu Kristo.

Shughuli Yamkini

  • Wasomee watoto, 1 Wakorintho 3:11 na uelezee kwamba Yesu Kristo ni msingi wetu. Onyesha watoto picha kadhaa za vitu tunavyoweza kuwa na shuhuda zake, ikijumuisha picha ya Yesu Kristo. Wasaidie kuzipanga picha ili kwamba picha ya Yesu iwe chini, kama msingi, na picha zingine “zinajenga” juu ya ushuhuda Wake.

  • Buni vitendo kwa ajili ya wimbo “The Wise Man and the Foolish Man” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 281), na uimbe wimbo huo pamoja na watoto. Mpatie kila mtoto jiwe lililoandikwa juu yake “Yesu Kristo ni msingi wangu.” Waache waende na mawe hayo nyumbani ili yawakumbushe kile walichojifunza.

  • Shiriki picha ambazo zinafafanua baadhi ya hadithi unazozipenda kutoka maisha ya Mwokozi, na waombe watoto wakuambie nini kinatokea katika picha. Waache wasimuliane baadhi ya hadithi zao wanazozipenda kuhusu Yesu. Toa ushuhuda wako kwamba Yesu Kristo ni msingi wa imani yako.

1 Wakorintho 6:19

Mwili wangu ni kama hekalu.

Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto kuthamini miili yao kama zawadi kutoka kwa Mungu na kuwa na matamanio makubwa ya kuitunza?

Shughuli Yamkini

  • Onyesha watoto picha za mahekalu (ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia), na soma maneno haya kutoka 1 Wakorintho 6:19: “Miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu.” Wasaidie watoto kuelewa kwamba Baba wa Mbinguni anatutaka sisi kuitunza miili yetu iwe safi na mitakatifu, kama hekalu.

  • Onyesha picha ya mtoto, na uweke picha kuzunguka picha hiyo za vitu ambavyo ni vizuri kwa miili yetu na vitu ambavyo ni vibaya. Waalike watoto kuchukua zamu kutambua vitu vizuri na kuviondoa vile vibaya.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu miili, kama vile “Head, Shoulders, Knees, and Toes” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 275), na waulize watoto kwa nini wanashukuru kwa ajili ya miili yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

1 Wakorintho 1:23–25

Kuwa mwenye busara inamaanisha kutumaini katika hekima ya Mungu.

Watoto unaowafundisha watapata—kama hawajapata bado—kwamba baadhi ya watu wanafundisha vitu ambavyo ni kinyume na hekima ya Mungu. Kujifunza 1 Wakorintho 1:23–25 kunaweza kuwasaidia watoto kuelewa kwamba tunaweza kutumainia hekima ya Mungu kwa sababu ni kuu kuliko yetu.

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto wasome 1 Wakoritho 1: 23–25 na watafute maneno haya hekima na upumbavu. Eleza kwamba watu wengi walifikiri mafundisho ya Paulo yalikuwa ni upumbavu, lakini Paulo alielezea kwamba kuamini injili ya Kristo ni hekima ya kweli. Kwa nini ni busara kuamini kile Mungu anachofundisha?

  • Wasaidie watoto waigize jinsi wanavyoweza kuwajibu watu wanaofikiri mafundisho ya Kanisa ni ya “upumbavu”—mafundisho kama vile kuamini katika Mwokozi, kutii Neno la Hekima, au kutii sheria ya zaka. Kwa mfano, wanaweza kushuhudia juu ya baraka ambazo zinakuja kutokana na kuishi mafundisho haya.

  • Shiriki uzoefu wako ambapo watu wengine walifikiri kwamba imani zako zilikuwa upumbavu, au shiriki mfano kutoka kwenye maandiko. Waache watoto washiriki uzoefu sawa na huo. Je, ni kwa jinsi gani 1 Wakorintho 1:25 inaweza kutusaidia kubaki waaminifu wakati wengine wanaiita imani zetu upumbavu?

1 Wakorintho 2:11–14

Roho Mtakatifu ananifundisha kweli za injili.

Unawezaje kuwasaidia watoto kutambua kwamba wanamhitaji Roho Mtakatifu ili kuelewa “mambo ya Mungu”?

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto kutengeneza orodha ya njia tunazojifunza kuhusu ulimwengu—kwa mfano, vitabu, shule, na mtandao. Kisha someni pamoja 1 Wakorintho 2:11–14. Mistari inafundisha nini kuhusu jinsi tunavyojifunza “mambo ya Mungu”?

  • Simulia kuhusu wakati ambapo ulijifunza kitu kupitia Roho wa Mungu. Wasaidie watoto kutambua nyakati ambazo wamemhisi Roho. Ni “mambo gani ya Mungu” (1 Wakorintho 2:11) ambayo Roho ametusaidia kuyaelewa?

  • Mwalike kila mtoto kusoma mojawapo ya maandiko haya: 1 Wakorintho 2:11–14; 1 Nefi 10:17; Moroni 10:3–5; na Mafundisho na Maagano 8:2–3. Waombe watoto kushiriki kile walichojifunza kutoka katika maandiko haya kuhusu jinsi Roho Mtakatifu anavyotufundisha sisi. Kwa nini tunashukuru kwa ajili ya kipawa cha Roho Mtakatifu?

1 Wakorintho 6:19–20

Sina budi kuutendea mwili wangu kwa heshima na kuuweka mtakatifu.

Kuelewa kwamba miili yetu ni zawadi kutoka kwa Baba wa Mbinguni kutawasaidia watoto kuweka miili yao kuwa mitakatifu, hata kama watajaribiwa kufanya vinginevyo.

Shughuli Yamkini

  • Leta chombo chenye picha ya mtoto na hekalu ndani yake. Waalike watoto wasome 1 Wakoritho 6:19–20 na wabashiri kilichopo ndani ya chombo. Waache wakifungue na mjadili ni kwa jinsi gani miili yetu ni kama mahekalu.

  • Zungumza na watoto kuhusu jinsi tunavyopaswa kulitendea hekalu. Kama miili yetu ni kama mahekalu, ni kwa jinsi gani tunapaswa kuitendea miili yetu? Kuimba au kusoma maneno ya wimbo kuhusu mahekaku, kama vile “The Lord Gave Me a Temple” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,153), kunaweza kusaidia kujibu swali hili. Tunapofanya makosa, tunawezaje kuyafanya “mahekalu” yetu kuwa safi tena?

  • (Someni kwa pamoja “Afya ya Mwili na Akili” (katika Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana (kijitabu, 2022], 22–29.) Waalike watoto kuorodhesha ubaoni ushauri wanaoupata kuhusu jinsi ya kulinda miili yetu.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki pamoja na familia zao wimbo ambao waliuimba katika darasa na kile walichojifunza kutokana na wimbo huo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Shuhudia juu ya Yesu Kristo. Mojawapo ya mambo muhimu unayoweza kufanya kama mwalimu ni kushuhudia juu ya Yesu Kristo. Hii itawasaidia watoto kuimarisha shuhuda zao na kuhisi upendo wa Mwokozi kwa ajili yao.

Chapisha