Agano Jipya 2023
Oktoba 9–15. Wafilipi; Wakolosai: “Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu”


“Oktoba 9–15. Wafilipi; Wakolosai: ‘Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Oktoba 9–15. Wafilipi; Wakolosai,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
Paulo akitoa imla ya barua akiwa gerezani

Oktoba 9–15

Wafilipi; Wakolosai

“Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu”

Ni lini ilikuwa mara ya mwisho wewe kusoma misukumo ya kiroho uliyoandika wakati wa kujifunza kwako Agano Jipya? Inaweza kusaidia kupitia tena ushawishi ambao umekuwa ukiupata.

Andika Misukumo Yako

Paulo aliandika nyaraka zake kwa Wafilipi na Wakolosai wakati akiwa mfungwa katika Rumi. Lakini barua hizi hazina toni unayoweza kutegemea kutoka kwa mtu aliye gerezani. Paulo alizungumza zaidi kuhusu furaha, kushangilia, na kutoa shukrani kuliko alivyofanya kuhusu mateso na majaribu: “Kristo anahubiriwa,” alisema, “na kwa hiyo nafurahi, naam, nami nitafurahi” (Wafilipi 1:18). Na “nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho, nikifurahi na kuuona … uthabiti wa imani yenu katika Kristo” (Wakolosai 2:5). Kwa hakika, “amani ya Mungu” ambayo Paulo aliipata katika hali zake ngumu “hupita akili zote” (Wafilipi 4:7), lakini ilikuwa hata hivyo ni uhalisia. Katika majaribu yetu wenyewe, tunaweza kujisikia wenye amani sawa na hii na “kufurahi katika Bwana siku zote” (Wafilipi 4:4). Tunaweza, kama Paulo alivyofanya, kutegemea kikamilifu kwa Yesu Kristo, “ambaye katika yeye tuna ukombozi” (Wakolosai 1:14). Tunaweza kusema, kama Paulo alivyosema “Nayaweza mambo yote katika Kristo anitiaye nguvu” (Wafilipi 4:13; ona pia Wakolosai 1:11).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Wafilipi 2:5–11; Wakolosai 1:12–23

Imani yangu imejengwa juu ya Yesu Kristo.

Rais Russell M. Nelson alisema kwamba yeye alipofokasi kujifunza kwake maandiko juu ya mistari kuhusu Yesu Kristo, imekuwa na matokeo mazuri kwake kwamba alihisi kuwa ni kama “mtu tofauti!” (“Kuvuta Nguvu ya Yesu Kristo kwenye Maisha Yetu,” Liahona, Mei 2017, 39). Fikiria kufuata mfano wake unaposoma Wafilipi na Wakolosai (ona hasa Wafilipi 2:5–11; Wakolosai 1:12–23). Unajifunza nini kuhusu Mwokozi? Ni kwa jinsi gani kweli hizi zinakusaidia kuwa “mwanamume au mwamamke tofauti?

Wafilipi 2:12–13

Je “tunautimiza wokovu [wetu] wenyewe”?

Watu wengine hutumia kirai “utimizeni wokovu wenu wenyewe” (Wafilipi 2:12) kuunga mkono wazo kwamba tunaokolewa tu kwa juhudi zetu wenyewe. Wengine hutumia fundisho la Paulo ”mnaokolewa kwa neema kwa njia ya imani” (Waefeso 2:8)—wakidai kwamba hakuna matendo yanayohitajika ili kupata wokovu. Hata hivyo, maandiko, ikijumuisha maandishi ya Paulo, kwa uwazi yanafundisha umuhimu wa vyote viwili neema ya Yesu Kristo na juhudi binafsi ili kupokea wokovu. Na hata katika juhudi zetu za kutimiza wokovu wetu wenyewe, “ni Mungu atendaye kazi ndani yenu” (Wafilipi 2:13; ona pia Wafilipi 1:6; 2 Nefi 25:23; Kamusi ya Biblia, “Neema”).

Wafilipi 3:4–14

Injili ya Yesu Kristo inastahili kila dhabihu.

Paulo aliacha vingi wakati alipoongoka kwenye injili ya Yesu Kristo, ikiwemo nafasi mashuhuri aliyokuwa nayo katika jumuiya ya Wayahudi kama Mfarisayo. Katika Wafilipi 3:4–14, tafuta Paulo alipata nini kwa sababu alikuwa radhi kujitoa dhabihu kwa ajili ya injili. Je, ni kwa jinsi gani yeye alihisi kuhusu dhabihu yake?

Kisha fikiria ufuasi wako wewe mwenyewe. Je, wewe umetoa dhabihu gani kwa ajili ya injili ya Yesu Kristo? Je, wewe umepokea nini? Je, kuna dhabihu yoyote ya ziada unayohisi unahitajika kufanya ili kuwa mfuasi wa Mwokozi aliyejitoa kikamilifu?

Ona pia 3 Nefi 9:19–20; Mafundisho na Maagano 58:2–5; Taylor G. Codoy, “Siku Moja Zaidi,” Liahona, Nov. 2018, 34–36.

Wafilipi 4:1–13

Ninaweza kupata furaha kwa Kristo, bila kujali hali yangu.

Maisha ya Paulo ni kielelezo halisi cha ukweli ulioelezewa na Rais Russell M. Nelson: “Wakati fokasi ya maisha yetu inapokuwa katika … Yesu Kristo na injili Yake, tunaweza kujihisi wenye furaha bila kujali nini kinatokea—au hakitokei—katika maisha yetu. Furaha huja kutoka Kwake, na kwa sababu Yake” (“Furaha na Kuendelea Kusalia Kiroho,” Liahona, Nov. 2016, 82).

Unaposoma Wafilipi—hususani sura ya 4—tafuta kauli zinazoweza kukusaidia kupata furaha katika hali yoyote ya maisha yako. Je, ni lini umepata “amani ya Mungu” wakati wa changamoto? (mstari wa 7). Je, ni lini umepata nguvu “kupitia Kristo” ya kufanya mambo magumu? (imstari wa 13). Kwa nini unafikiri ni muhimu “kuwa mwenye kuridhika” katika hali zote? (mstari wa 11). Je, ni kwa jinsi gani kufanyia mazoezi sifa katika mstari wa 8 hukusaidia kupata furaha katika hali zako?

Ona Alma 33:23; Dieter F. Uchtdorf, “Shukuru katika Hali Zo Zote,” Liahona, Mei 2014, 70–77.

Wakolosai 3:1–17

Wafuasi wa Yesu Kristo hufanywa “upya” pale wanapoishi injili Yake.

Je, ni kwa jinsi gani unaweza kujua kwamba injili ya Yesu Kristo inakusaidia kuwa “mtu mpya”? Njia mojawapo ya kutafakari hili ni kutafiti Wakolosai 3:1–17 na kutengeneza orodha ya mitazamo, sifa, na matendo ya “mtu wa zamani” na orodha nyingine ya mitazamo, sifa, na matendo ya “mtu mpya.”

Andika mawazo yako kuhusu jinsi Mwokozi anavyokubadilisha, ili kwamba uweze kuyarejelea baadaye na kutafakari jinsi gani unavyoendelea.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Wafilipi.Familia yako inaweza kugundua maneno furaha au shangilia yakirudiwa mara kwa mara katika Wafilipi. Kila mara mnapokutana na moja ya maneno haya, mnaweza kusimama na kujadili Paulo alifundisha nini kuhusu jinsi ya kuwa na furaha.

Wafilipi 2:14–16.Ni kwa jinsi gani tunaweza “kuangaza kama nuru katika ulimwengu”?

Wafilipi 4:8.Pengine familia yako inaweza kuonyesha mambo ya “kutafakari” ambayo yanaendana na maelezo katika mstari huu (ona pia Makala ya Imani 1:13). Ni kwa jinsi gani familia yako itabarikiwa kwa kufuata ushauri wa Paulo?

Wakolosai 1:23; 2:7.Pengine familia yako inaweza kusoma mistari hii wakiwa wamekaa kuzunguka mti au wakiwa wanaangalia picha ya mti (kama ile ambayo inaambatana na muhtasari huu). Inamaanisha nini “kujengwa” na “kuwa na shina” katika Kristo? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kusaidiana sisi kwa sisi kuimarisha mashina yetu ya kiroho?

Wakolosai 2:2–3.Familia yako ingeweza kufurahia kujaza “sanduku la hazina” kwa vitu ambavyo vinawakilisha “utajiri” na “hazina za hekima na maarifa” unayopata katika injili.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa “Rejoice, the Lord Is King!,” Nyimbo za Kanisa, na. 66.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Ishi ushuhuda wako. “Unafundisha kile wewe ulicho,” Mzee Neal A. Maxwell alifundisha. “Sifa zako zitakumbukwa zaidi … kuliko kweli fulani katika somo fulani” (katika Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,13).

Picha
mti wenye mizizi mingi

Paulo alifundisha kwamba imani yetu inapaswa “kuwa yenye shina” katika Yesu Kristo (Wakolosai 2:7).

Chapisha