Agano Jipya 2023
Oktoba 16–22. 1 na 2 Wathesalonike: “Kuyatengeneza Mapungufu ya Imani Yenu”


“Oktoba 16–22. 1 na 2 Wathesalonike: ‘Kuyatengeneza Mapungufu ya Imani Yenu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Oktoba 16–22. 1 na 2 Wathesalonike,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
akina dada wamisionari wakizungumza na mvulana

Oktoba 16–22

1 na 2 Wathesalonike

“Kuyatengeneza Mapungufu ya Imani Yenu”

Kama hatuandiki misukumo tunayopokea kutoka kwa Roho tunaweza kuisahau. Je, Roho anakushawishi kuandika nini unaposoma 1na 2 Wathesalonike?

Andika Misukumo Yako

Katika Thesalonike, Paulo na Sila walishitakiwa kwa “kuupindua ulimwengu” (Matendo ya Mitume 17:6). Mahubiri yao yaliwakasirisha viongozi fulani miongoni mwa Wayahudi, na viongozi hawa walichochea watu kufanya ghasia (ona Matendo ya Mitume 17:1–10). Matokeo yake, Paulo na Sila walishauriwa kuondoka Thesalonike. Paulo alihofia kuhusu waongofu wapya wa Thesalonike na mateso waliyokuwa wakipata, lakini hakuweza kurudi kuwatembelea tena. “Nilipokuwa siwezi kuvumilia tena,” aliandika, “Nalituma mtu ili kujua imani yenu.” Katika kujibu, Timotheo msaidizi wa Paulo, aliyekuwa akitumikia katika Thesalonike, “alituletea habari njema za imani yenu na upendo wenu” (1 Wathesalonike 3:5–6). Hata hivyo, Watakatifu wa Thesalonike walijulikana kama vielelezo “kwa watu wote waaminio” (1 Wathesalonike 1:7), na habari kuhusu imani yao ilisambaa katika miji ya mbali. Fikiria shangwe na faraja ya Paulo kusikia kwamba kazi yake miongoni mwao “haikuwa bure” (1 Wathesalonike 2:1). Lakini Paulo alijua kwamba uaminifu katika kipindi cha nyuma hautoshi kuendelea kuishi katika siku za baadaye, na alikuwa na hofu juu ya ushawishi wa walimu wa uongo miongoni mwa Watakatifu (ona 2 Wathesalonike 2:2–3). Ujumbe wake kwao, na kwetu, ni kuendelea “kuyatengeneza mapungufu ya imani [yetu]” na “kuzidi sana” katika upendo (ona 1 Wathesalonike 3:10; 4:10).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

1 Wathesalonike 1–2

Wafuasi wa Kristo huwahudumia wengine kwa dhati na kwa upendo.

Katika 1 Wathesalonike, maneno ya Paulo hufunua vyote kujali na shangwe ya mtu ambaye amejitoa mwenyewe kikamilifu kuwatumikia watoto wa Mungu. Hasa katika sura mbili za mwanzo za 1 Wathesalonike, utakuta maneno na virai ambavyo huelezea sifa na matendo yanayomwelezea Bwana. Kwa mfano, unajifunza nini kutoka katika 1 Wathesalonike 1:5–8; 2:1–13 kuhusu kumtumikia Bwana?

Fikiria kuhusu fursa zako mwenyewe za kumtumikia Mungu na watoto Wake. Ni kipi unachopata katika sura hizi ambacho kinakutia msukumo kuboresha huduma yako? Fikiria kujiuliza mwenyewe maswali kulingana na kile unachokipata, kama vile “Je, Mimi ni mfano juu ya mambo ninayoyajua?” (ona 1 Wathesalonike 1:7).

1 Wathesalonike 3:7–13; 4:1–12

“Awaongezee na kuwazidisha katika upendo.”

Paulo alifurahia uaminifu wa Watakatifu wa Thesalonike (ona 1 Wathesalonike 3:7–9). Lakini pia aliwataka wao “wapate kuzidi sana” katika uaminifu huo (1 Wathesalonike 4:1). Unaposoma 1 Wathesalonike 3:7–13; 4:1–12, tafakari njia unazoweza “kuzidi sana” kiroho (1 Wathesalonike 4:10). Kwa mfano, tazama vile Paulo alivyotumia maneno kama “utakatifu” na “utakaso.” Je, unajifunza nini kutoka kwenye maandishi ya Paulo kuhusu maana ya maneno haya? Je, ni kwa jinsi gani Mwokozi anaweza kukusaidia kuwa mtakatifu zaidi na kutakaswa zaidi?

Ona pia Mwongozo wa Maandiko, “Takatifu,” “Utakaso,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org.

1 Wathesalonike 4:16–18; 5:1–10; 2 Wathesalonike 1:4–10

Kama mimi ni mwaminifu na mwangalifu, nitakuwa nimejiandaa kwa ajili ya Ujio wa Pili wa Mwokozi.

Katika 1 Wathesalonike 5:1–10, Paulo alitumia sitiari kadhaa kufundisha kuhusu wakati Yesu atakaporudi duniani. Unapojifunza sitiari hizi, fikiria kuandika misukumo inayokujia kuhusu Ujio wa Pili wa Yesu Kristo:

  • “Mwivi ajavyo usiku”:

  • “Utungu umjiavyo mwenye mimba”:

  • Sitiari zingine unazopata:

Ni kweli zipi za ziada unajifunza kutoka katika 1 Wathesalonike 4:16–18; 5:1–10; 2 Wathesalonike 1:4–10? Wewe unashawishika kufanya nini ili kujihadhari na kujiandaa kwa ajili ya ujio wa Mwokozi?

Ona pia D. Todd Christofferson, “Kujiandaa kwa ajili ya Kurudi kwa Bwana,” Liahona, Mei 2019, 81–84.

2 Wathesalonike 2

Ukengeufu, au kuanguka kutoka kwenye ukweli, kulitabiriwa kuutangulia Ujio wa Pili.

Katikati ya ongezeko la mateso, Watakatifu wa Thesalonike wengi waliamini Ujio wa Pili wa Mwokozi lazima ulikaribia. Lakini Paulo alijua kwamba kabla ya Yesu kurudi duniani kungekuwepo na ukengeufu—uasi au “kuanguka” kutoka kwenye ukweli (ona 2 Wathesalonike 2:1–4). Unaweza kupanua uelewa wako juu ya Ukengeufu Mkuu—na uelewa wako wa Urejesho—kwa kutafakari baadhi ya yafuatayo:

  • Maandiko yaliyotabiri Ukengeufu: Isaya 24:5; Amosi 8:11–12; Mathayo 24:4–14; 2 Timotheo 4:3–4

  • Maandiko yanayoonyesha ukengeufu ulikuwa tayari umeanza katika wakati wa Paulo: Matendo ya Mitume 20:28–30; Wagalatia 1:6–7; 1 Timotheo 1:5–7

  • Uchunguzi kuhusu Ukengeufu Mkuu uliofanywa na waleta mabadiliko wa Kikristo:

    Martin Luther: “Sikutafuta kingine zaidi ya kuleta mabadiliko kwa Kanisa katika kuendana na Maandiko Matakatifu. … Kwa urahisi ninasema kwamba Ukristo umetoweka kati ya wale ambao walipaswa kuutunza” (katika E. G. Schweibert, Luther and His Times: The Reformation from a New Perspective [1950],590).

    Roger Williams: “Ukengeufu … mpaka sasa umeharibu kila kitu kwamba hakuwezi kuwepo na kupona kutokana na huo ukengeufu mpaka Kristo atume mitume wapya kupanda upya makanisa” (katika Philip Schaff, The Creeds of Christendom [1877],851).

Ona pia 2 Nefi 28; Mada za Injili, “Ukengeufu,” topics.ChurchofJesusChrist.org.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

1 Wathesalonike 3:9–13.Je, ni nini kinachokupendeza kuhusu hisia alizokuwa nazo Paulo kwa rafiki zake? Ni kwa jinsi gani tunaweza “kuongezeka na kuzidi sana katika upendo, sisi kwa sisi”? (mstari wa 12).

1 Wathesalonike 4:13–18.Ni virai gani katika mistari hii vinavyoelezea kuhusu ufufuko vinakupa wewe faraja?

1 Wathesalonike 5:14–25.Unapopitia tena ushauri wa Paulo katika 1 Wathesalonike 5:14–25, mwalike kila mwanafamilia atafute kirai ambacho familia inaweza kufokasi juu yake. Tafuta njia za ubunifu za kutundika virai hivi nyumbani kama ukumbusho. Kwa mfano, kila mmoja angeweza kutafuta au kuchora picha ambazo zinaelezea au kuimarisha kirai ambacho yeye amechagua.

2 Wathesalonike 3:13.Je, tumewahi kuhisi “kukata tamaa katika kutenda mema”—kuzidiwa, pengine, na mahitaji ya ufuasi? Je, ni kitu gani hutusaidia tunapohisi hivyo? (Ona Wagalatia 6:9; Mafundisho na Maagano 64:33.) Ni kwa jinsi gani tunaweza kusaidiana wakati hili linapotokea?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “I’m Trying to Be like Jesus,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 78–79

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tafuta ufunuo kila siku. “Ufunuo mara nyingi huja ‘mstari juu ya mstari’ (2 Nefi 28:30), wala sio wote kwa wakati mmoja. … Usifikirie [kujifunza injili] kama shughuli ambayo unaitengea muda bali kama vile tu shughuli ambayo unaifanya kila wakati” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,12).

Picha
Yesu akiwa mawinguni

Kristo Aliyefufuka, na Robert T. Barrett

Chapisha