Agano Jipya 2023
Oktoba 9–15. Wafilipi; Wakolosai: “Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu”


“Oktoba 9-15. Wafilipi; Wakolosai: ‘Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2023 (2022)

“Oktoba 9–15. Wafilipi; Wakolosai,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2023

Picha
Paulo akitoa imla ya barua akiwa gerezani

Oktoba 9–15

Wafilipi; Wakolosai

“Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu”

Soma Wafilipi and Wakolosai, huku ukifikiria kuhusu watoto unaowafundisha. Tafuta mwongozo wa kiungu kuhusu jinsi ya kuwafundisha kanuni zilizo katika nyaraka hizi.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waulize watoto walifanya nini wiki hii iliyopita ili kufanyia kazi kitu walichojifunza katika darasa la wiki iliyopita. Kwa mfano, walifanya nini ili kumfikia mtu aliyehitaji rafiki?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Wafilipi 1:3–4; Wakolosai 1:3, 9

Viongozi wa Kanisa wananipenda na wanasali kwa ajili yangu.

Paulo mara kwa mara alianza nyaraka zake kwa kuonyesha upendo kwa waumini wa Kanisa na kuwaambia kwamba alisali kwa ajili yao. Fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia watoto kuelewa kwamba viongozi wao wa Kanisa wanawapenda.

Shughuli Yamkini

  • Soma Wafilipi 1:3–4 na Wakolosai 1:3, 9 kwa sauti, na waombe watoto kukunja mikono yao na kuinamisha vichwa vyao kila wakati wanaposikia maneno sali, kusali, na sala. Eleza kwamba Mtume Paulo alisali kwa ajili ya waumini wa Kanisa, kama vile viongozi wetu wa Kanisa wanavyosali kwa ajili yetu leo.

  • Onyesha picha ya Yesu Kristo, na usome baadhi ya mstari ya andiko ambayo inaelezea Yeye akisali kwa ajili ya mtu fulani (kwa mfano, Luka 22:32; 3 Nefi 19:21, 23). Yesu aliomba nini wakati alipoomba kwa ajili ya wengine?

  • Wasaidie watoto kutaja majina ya baadhi ya viongozi wao wa Kanisa, kama vile rais wa Msingi, askofu, na Rais wa Kanisa. Eleza kwamba viongozi hawa wanamwomba Baba wa Mbinguni kuwabariki watoto na kuwasaidia kuishi kwa haki. Fikiria kuwaeleza watoto kile unachosema wakati unaposali kwa ajili yao.

Wafilipi 4:4, 8

Ninaweza kushangilia katika Bwana.

Paulo aliwatia moyo Watakatifu kushangilia—hata kama walikabiliwa na majaribu magumu na Paulo mwenyewe alikuwa gerezani. Utawasaidia vipi watoto waone kwamba kumfuata Yesu Kristo kunaleta shangwe?

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto wasikilize neno lililorudiwa wakati unaposoma Wafilipi 4:4. Waombe watoto wakuoneshe kile ambacho wanafanya wanaposhangilia. Waambie watoto kwa nini wewe “unashangilia katika Bwana”—kwa nini unajisikia mwenye furaha kwa sababu ya Yesu Kristo. Acha watoto washiriki jinsi wanavyojisikia kuhusu Yesu Kristo.

  • Onyesha vitu au picha ambayo inawakilisha vitu ambavyo vinakusaidia wewe “kushangilia katika Bwana” (Wafilipi 4:4), kama vile uumbaji Wake, hekalu, Ufufuko Wake, au familia. Waache watoto wachukue zamu kuchagua picha au kitu, na kisha waelezee kwa nini kinakufanya uwe na furaha. Waalike kuelezea vitu ambavyo vinawasaidia wao kufurahia katika Bwana.

  • Someni Wafilipi 4:8 pamoja, na wasaidie watoto kufikiria juu ya vitu ambavyo vinaendana na maelezo katika mstari huu (ona pia Makala ya Imani 1:13). Waalike watoto kuchora picha za vitu hivi.

Wakolosai 1:23; 2:6–7

Imani yangu inapaswa “kukita mizizi” katika Yesu Kristo.

Kama watoto wanajenga maisha yao na imani yao juu ya Mwokozi, watakuwa na uwezo wa kustahimili dhoruba za maisha.

Shughuli Yamkini

  • Onyesha picha ya mti kutoka muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia wakati unaposoma virai muhimu kutoka Wakolosai 1:23; 2:6–7 (au onyesha video ya “Spiritual Whirlwinds” katika ChurchofJesusChrist.org). Je, nini kingetokea kwa mti huu kama dhoruba ingekuja na mti haukuwa na mizizi imara? Waache watoto wasimame na wajifanye kuwa mti ambao una mizizi dhaifu katika dhoruba na kisha mti wenye mizizi imara. Shuhudia kwamba imani katika Mwokozi inaweza kutusaidia kuwa kama mti wenye mizizi imara? Ndipo tunapoweza kustahmili “dhoruba” za kiroho, kama majaribu na nyakati ngumu.

  • Mualike mtoto kuchora mti ubaoni. Waombe watoto kutaja baadhi ya vitu wanavyoweza kufanya ili kuwa na “mizizi iliyojikita” katika Yesu Kristo. Kila wakati mtoto anapotaja kitu fulani, mwalike yeye aje kuongeza mzizi kwenye mchoro.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Wafilipi 4:4–13

Kama nina imani katika Yesu Kristo, ninaweza kuwa na furaha hata katika nyakati ngumu.

Paulo aliteseka na majaribu mengi, lakini alikuwa na furaha kwa sababu alikuwa na imani katika Yesu Kristo.

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto wafikirie kwamba wako gerezani, kama vile Mtume Paulo alivyokuwa wakati alipoandika Waraka kwa Wafilipi. Soma Wafilipi 4:4–13 pamoja na watoto na waombe watafute maneno yafuatayo “shangilia,” “amani,” na “kuridhika.” Je, ni kwa nini Paulo aliweza kufurahi na kujisikia amani hata akiwa gerezani? Kisha wasaidie watoto kutafuta maneno “Bwana,” “Mungu,” na “Kristo” katika mistari hii. Wasaidie kuelewa kwamba imani ya Paulo katika Yesu Kristo ilifanya iwezekane kwake yeye kufurahi.

  • Waalike watoto wakusaidie kukamilisha sentensi kama zifuatavyo: “ninaweza kuwa katika giza na bado nikaona vitu kama nina . Ninaweza kuwa nje siku ya joto kali na bado nikajisikia nimepoa kama nina Ninaweza kuwa na nyakati ngumu na bado nikapata shangwe kama nina . Ni nini Wafilipi 4:4–13 inapendekeza tunaweza kufanya ili tupate shangwe? Waalike watoto kushiriki baadhi ya nyimbo za dini au maandiko kuhusu Yesu ambayo yanaweza kuwasaidia kusikia shangwe wakati wa nyakati ngumu.

Wafilipi 4:8

Ninaweza “kufikiria juu ya” mambo ambayo ni ya ukweli, uaminifu, na safi.

Watoto mara kwa mara wanawekwa mbele ya mambo yaliyo maovu na machafu. Unaweza kuwasaidia kutafuta mambo yenye kutia moyo na yaliyo mema.

Shughuli Yamkini

  • Mwombe mtoto mmoja asome Wafilipi 4:8 kwa sauti wakati wengine wanatafuta maneno katika Makala ya Imani 1:13 ambayo ni sawa au yanafanana. Mwalike mtu mmoja kuandika maneno haya ubaoni. Waulize watoto maneno haya yana maana gani, na wasaidie wayafafanue kama inavyohitajika. Je, ni kwa nini tunapaswa “kutafakari juu ya” mambo haya? Tunawezaje sisi “kuyatafuta” hayo?

  • Waombe watoto kutaja vitu ambavyo vinaweza kuwa sawa na maelezo katika Wafilipi 4:8. Waalike kuweka orodha wiki hii ya kitu cho chote waonacho kinachofanana na maelezo haya. Wahimize kuleta orodha zao kwenye Msingi wiki ijayo na kuelezea kile walichopata.

Wakolosai 1:23; 2:6–7

Imani yangu inapaswa “kukita mizizi” katika Yesu Kristo.

Shetani anajaribu kudhoofisha imani yetu kupitia majaribu na mafundisho ya uongo. Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuimarisha imani yao katika Mwokozi ili kwamba “wasiondoshwe mbali na tumaini la injili hii”? (Wakolosai 1:23).

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kuchora picha ambazo zinawakilisha ukweli wanaoupata katika Wakolosai 1:23; 2:6–7. Waache washiriki picha zao pamoja na darasa na kueleza ukweli unaowakilishwa na picha zao.

  • Onyesha video ”Spiritual Whirlwinds.” Je, baadhi ya majaribu na mafundisho ya uongo ulimwenguni leo ambayo huweza kudhoofisha imani yetu ni yapi? Watie moyo watoto kuandika kitu kimoja wanachoweza kufanya ili kuimarisha imani yao ili kwamba “wakite mizizi” (Wakolosai 2:7) katika Yesu Kristo. Waombe waweke kadi hiyo mahali ambapo wataiona kila siku.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki pamoja na familia zao kile walichojifunza kuhusu Yesu Kristo. Wangeweza kutumia ukurasa wa shughuli ya wiki hii au maandiko waliyosoma darasani leo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Watoto ni wadadisi na wanajifunza kupitia matukio mapya na tofauti. Tumia shughuli zinazowasaidia watoto kusogea sogea, kutumia milango yao yote ya fahamu, kuchunguza, na kujaribu vitu vipya. Mapendekezo katika “Kukidhi Mahitaji ya Watoto Wadogo” mwanzoni mwa nyenzo hii yanaweza kusaidia. (Ona pia Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.)

Chapisha