Agano Jipya 2023
Septemba 25–Oktoba 1. Wagalatia: “Tembea katika Roho”


“Septemba 25–Oktoba 1. Wagalatia: ‘Tembea katika Roho’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2023 (2022)

“Septemba 25–Oktoba 1. Wagalatia,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2023

Picha
Kristo anamtokea Paulo gerezani

Mwokozi mfufuka alimtembelea Paulo gerezani (ona Matendo ya Mitume 23:11). Yesu Kristo anaweza kutuweka huru kutokana na “nira ya utumwa” (Wagalatia 5:1).

Septemba 25–Oktoba 1

Wagalatia

“Tembea katika Roho”

Unaposoma Wagalatia, je, ni misukumo gani unayokuwa nayo kuhusu kile watoto katika darasa lako wanahitaji kujifunza?

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wape watoto dakika chache kuchora kitu fulani walichojifunza kutoka kwenye majadiliano ya hivi karibuni ya injili nyumbani au kanisani. Acha watoto washiriki kile kila mchoro unawakilisha.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Wagalatia 5:22–23

Roho Mtakatifu hunisaidia kuhisi upendo, furaha, na amani.

Watoto wadogo wanaweza kutambua matunda ya Roho. Hii itawaandaa wao kutafuta ushawishi wa Roho Mtakatifu katika maisha yao yote.

Shughuli Yamkini

  • Tundika au onyesha picha kadhaa za aina ya matunda, na waalike watoto kuelezea jinsi kila tunda linaonja. Eleza kwamba kama vile matunda yalivyo na ladha tofauti, sisi tunaweza kumhisi Roho Mtakatifu katika njia tofauti, kama vile upendo na amani. Eleza baadhi ya njia ambazo wewe umewahi kumhisi Roho Mtakatifu katika maisha yako, na acha watoto nao washiriki jinsi Roho Mtakatifu anavyohisika kwao.

Picha
matufaha katika mti

Watoto wa umri wote wanaweza kupata uzoefu wa “tunda la Roho.”

  • Soma Wagalatia 5:22–23 pamoja na watoto, na fafanua maneno ambayo yawezekana hawajayajui. Mwalike kila mtoto kuchagua tunda la Roho lililotajwa katika mistari hii na kusimulia kuhusu muda alipopata uzoefu wa tunda hilo. Waalike watoto kuchora picha za kawaida za uzoefu wao.

Wagalatia 6:2

Yesu Kristo ananitaka niwasaidie wale wenye shida.

Maelekezo katika Wagalatia 6:2 yanafanana na mafundisho ya Alma katika Mosia 18:8 kwa watu waliokuwa karibu kubatizwa. Chukua nafasi hii kuwasaidia watoto kujiandaa kwa ajili ya maagano ya ubatizo.

Shughuli Yamkini

  • Onyesha picha ya mtoto akibatizwa (kama vile Kitabu cha Sanaa za Injili, na.104). Waulize watoto kile mtoto anafanya. Eleza kwamba tunapobatizwa, tunafanya maagano, au ahadi. Soma Wagalatia 6:2 au Mosia 18:8 kuwasaidia watoto kujifunza mojawapo ya vitu tulivyoahidi kufanya: kubebeana mizigo. Waalike watoto kuchora picha za njia wanazoweza kuwasaidia wengine wanaobeba mizigo.

  • Wasomee watoto kirai hiki kutoka Wagalatia 6:2: “Mchukuliane mizigo.” Ili kuelezea hii inamaanisha nini, mpe mmojawapo wa watoto kitu fulani kizito akibebe. Kisha omba mtu ajitolee kumsaidia mtoto kubeba mzigo huo. Eleza kwa watoto kwamba vitu vingi vinaweza kuwa kama mzigo, kama kuwa mgonjwa au kuhuzunika au kuwa mpweke. Tufanye nini kumsaidia mtu mwenye aina hii ya mzigo?

Wagalatia 6:7–9

Matendo yetu, yote mazuri na mabaya, yana matokeo yake.

Kwa kufundisha hilo tunavuna kile tulichopanda, kama ilivyoelezewa katika Wagalatia 6:7–9, unaweza kuwafundisha watoto kufikiria juu ya matokeo ya matendo yao.

Shughuli Yamkini

  • Onyesha mbegu na mboga. Wasomee watoto Wagalatia 6:7–9. Waalike watoto wajifanye wanapanda mbegu wanaposikia neno panda. Waombe wajifanye wanachuma mboga kutoka kwenye mmea wanaposikia neno vuna.

  • Waonyeshe watoto aina kadhaa za mboga, na wasaidie kupata mbegu katika kila moja. Weka mbegu katika chombo, na waache watoto wachukue zamu kuchagua moja na kusimulia ni mboga gani itaota kama wanaipanda. Wasaidie waone kwamba kama mbegu tunazopanda zinaamua mboga tunayopata, maamuzi tunayofanya yanaamua matokeo na baraka hatimaye tunazopata.

  • Fanya mstari sakafuni kwa utepe. Weka sura yenye furaha na sura ya huzuni mkabala na miisho ya mstari. Mwalike mtoto kusimama katikati ya mstari, na awasaidie watoto wengine wafikirie chaguzi ambazo zitaelekeza kwenye furaha au huzuni. Kwa kila uchaguzi, muombe mtoto aliyepo katikati apige hatua kuelekea upande wa furaha au upande wa huzuni. Rudia shughuli hii mara kadhaa, na waache watoto wengine wachukue zamu kusimama juu ya utepe.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Wagalatia 3:26–28

Kubatizwa hutufanya sisi kuwa “wamoja katika Kristo.”

Paulo aliwafundisha Watakatifu wa Galatia kwamba walipobatizwa wangekuwa “wamoja katika Kristo Yesu.” Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto kujitahidi kujenga umoja unaoelezewa katika Wagalatia 3:26–28?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kusoma Wagalatia 3:26–28 ukiwa na swali akilini: Ni nini kinatokea ninapobatizwa? Unaweza kuhitaji kuzingatia juu ya virai kama “kumvaa Kristo” au “mmoja katika Kristo.” Yawezekana virai vinamaanisha nini? Ni kwa jinsi gani “kumvaa Kristo” ni sawa sawa na kujichukulia jina Lake juu yetu wenyewe (ona Mafundisho na Maagano 20:75–79). Tunaweza kufanya nini ili kuwaonyesha wengine kwamba tumejichukulia jina Lake juu yetu wenyewe?

  • Someni pamoja Wagalatia 3:28, na zitambueni baadhi ya njia watu waliojitambulisha wenyewe wakati walipokuwa wakibatizwa katika siku za Paulo. Wasaidie watoto kutaja baadhi ya njia wanazojitambulisha wenyewe leo. Je, Paulo anajaribu kutufundisha nini kuhusu jinsi tunavyopaswa kuchukuliana wakati tunapobatizwa?

Wagalatia 5:16, 22–23

Kama “nikienenda kwa Roho” nitapokea “tunda la Roho.”

Wakati tunapobatizwa na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, tunaweza kupokea tunda la Roho zaidi katika maisha yetu. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto kutambua tunda hili katika maisha yao?

Shughuli Yamkini

  • Mpe kila mtoto kipande cha karatasi (unaweza kukata karatasi katika maumbo ya tunda), na waombe watoto kutafuta “tunda la Roho” lililoorodheshwa katika Wagalatia 5:22–23. Waalike kuandika mojawapo ya hayo matunda upande mmoja wa karatasi yao na neno ambalo lina maana ya kinyume chake upande mwingine. (Wasaidie kuelewa maneno ambayo hawana uzoefu nayo.) Waalike washiriki matunda yao na darasa. Tunaweza kufanya nini ili Roho Mtakatifu daima awe pamoja nasi?

  • Waalike watoto wasome kuhusu tunda la Roho katika Wagalatia 5:22–23 na andika kuhusu au chora picha ya wakati walihisi mojawapo ya matunda hayo. Waombe wasimulie hadithi zao au picha na mtu mwingine katika darasa. Je, ni kwa nini tunda ni njia nzuri ya kutusaidia kuelewa jinsi Roho anavyotushawishi?

Wagalatia 6:7–9

Matendo yetu, yote mazuri na mabaya, yana matokeo yake.

Wasaidie watoto kuelewa kwamba matokeo ya tabia zetu wakati mwingine yanakuja mara moja na wakati mwingine yanaweza kuja “katika kipindi kijacho” (mstari wa 9).

Shughuli Yamkini

  • Someni pamoja Wagalatia 6:7–9. Toa orodha ya vitendo (au mbegu za “kupanda” na matokeo (au tunda “tunalovuna”). Waombe watoto kulinganisha matendo na matokeo yake.

  • Waalike watoto kuorodhesha baadhi ya baraka wanazotegemea kuzipokea kutoka kwa Baba wa Mbinguni. Wasaidie kufikiri juu ya “mbegu” ambazo lazima wapande ili “wavune” baraka hizi.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wasaidie watoto kuangalia njia ambazo ukweli waliojifunza leo unavyoweza kutumika katika maisha yao ya kila siku. Kwa mfano, ungeweza kuwaalika kutazamia matokeo mazuri, au “tunda,” ambalo huja kwa sababu ya uamuzi mzuri waliofanya.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Rekebisha shughuli kulingana na umri wa watoto unaowafundisha. Wape watoto fursa za kushiriki, lakini kumbuka kwamba uwezo wao wa kufanya hivyo utatofautiana kulingana na umri na kupevuka kwao. Watoto wadogo wanaweza kuhitaji mwongozo zaidi na maelekezo. Kadiri wanavyopevuka, watoto wanaweza kuchangia zaidi na kuwa bora katika kushiriki mawazo yao. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.)

Chapisha