Agano Jipya 2023
Oktoba 2–8. Waefeso: “Kwa Kusudi la Kuwakamilisha Watakatifu”


“Oktoba 2–8. Waefeso: ‘Kwa Kusudi la Kuwakamilisha Watakatifu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2023 (2022)

“Oktoba 2–8. Waefeso,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2023

Picha
familia ikitazama picha

Oktoba 2–8

Waefeso

“Kwa Kusudi la Kuwakamilisha Watakatifu”

Unapojifunza Waraka kwa Waefeso, fikiria kuhusu ni kanuni gani ungeweza kusisitiza ili kuwabariki watoto unaowafundisha. Andika mawazo yo yote ambayo yanakuja akilini wakati unaposoma.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto kusimama kwenye mstari. Ukianzia mbele ya mstari, mpe kila mtoto nafasi ya kushiriki kitu ambacho yeye amejifunza hivi karibuni kuhusu injili wakati wa kujifunza maandiko kifamilia, katika Msingi, au mahali pengine po pote.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Waefeso 2:19

Waumini wa Kanisa wanapaswa kuwa marafiki na “wenyeji.”

Je, watoto katika darasa lako wapo zaidi kama “wageni” au “wenyeji” kwa kila mmoja na pamoja na waumini wengine wa kata? Wasaidie kuelewa kwamba ingawa tuna tofauti, Mwokozi anatusaidia kuwa wamoja na kupendana.

Shughuli Yamkini

  • Weka picha ya Mwokozi katikati ya darasa. Waalike watoto kusimama sehemu tofauti za chumba kuwakilisha “wageni” au “wageni kutoka nje ya nchi.” Wasaidie kuelewa kwamba maneno haya yanamaanisha watu tusiowajua. Unaposoma Waefeso 2:19, waalike kwenda mbele kuelekea picha ya Kristo mpaka watakaposimama wakiwa wamekaribiana. Waambie kwamba tunapokuja karibu zaidi kwa Mwokozi, tunaweza kuja kuunganika na wengine kama “wananchi wenzetu,” au marafiki.

  • Tafuta picha za watoto kutoka sehemu tofauti za ulimwengu na zifiche kuzunguka chumba. Weka picha ya Mwokozi mbele ya chumba. Alika darasa lako kuwa katika jozi kama wamisionari na wafanye zamu kutafuta picha ya “mgeni” na kuiweka karibu na picha ya Mwokozi. Wasaidie kuelewa kwamba watu wanapobatizwa, wanakuwa sehemu ya familia yetu ya Kanisa, au “watu wa nyumbani mwake Mungu.” Je, tunawezaje kumsaidia mtu aliye mgeni ajisikie anakaribishwa?

Waefeso 6:1–3

Baba wa Mbinguni ananitaka niwatii wazazi wangu.

Unaposoma Waefeso 6:1–3, fikiria njia unazoweza kuwasaidia watoto kuelewa kwa nini ni muhimu kuwatii wazazi wao.

Shughuli Yamkini

  • Soma Waefeso 6:1 kwa darasa, au msaidie mmojawapo wa watoto kuisoma. Wasaidie kufikiria nyakati ambapo waliwatii wazazi wao. Waombe waelezee jinsi walivyobarikiwa kwa kutii na jinsi walivyojisikia wakati walipotii. Kwa nini ni muhimu kuwatii wazazi wetu?

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu utii, kama vile “Quickly I’ll Obey” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 197). Waache watoto wapeane zamu kutaja kitu ambacho wazazi wamewaomba wafanye, na waalike kuigiza kukifanya kitu hicho.

  • Onesha picha ya Yesu Kristo akiwa anabatizwa (ona Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 35), na ashiriki jinsi Mwokozi alivyomtii Baba wa Mbinguni kwa kubatizwa (ona 2Nefi 31:6–7). Elezea matukio ambayo wewe ulitii wazazi wako na ukabarikiwa. Kwa nini Baba wa Mbinguni anatutaka sisi tuwatii wazazi wetu?

Waefeso 6:10–18

Silaha za Mungu zinaweza kunilinda dhidi ya uovu.

Je, utawasaidiaje watoto kuelewa kwamba kufanya mambo ya haki ni kama kuvaa silaha?

Shughuli Yamkini

  • Onyesha picha ya mtu aliyevaa silaha za kivita, kama vile yule aliye katika ukurasa wa shughuli ya wiki hii au muhtasari wa wiki hii katika Njoo Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia. Unapofanyia muhtasari Waefeso 6:10–18, waonyeshe watoto jinsi vipande tofauti vya silaha za vita vinavyolinda sehemu tofauti za mwili. (Ona “Silaha Zote za Mungu,” Rafiki, Juni 2016, 24–25)

  • Lete vitu kadha darasani ambavyo vingeweza kuwakilisha vipande vya silaha vilivyotajwa katika Waefeso 6:14–17 (kwa mfano, kofia au aproni), au tengeneza vipande vya kawaida vya silaha za kivita kutokana na karatasi. Acha watoto wachukue zamu kuvaa “silaha za vita.” Wasaidie kuelewa jinsi tunavyovaa silaha za Mungu (kwa mfano, kwa kujifunza maandiko, kuhudumia wengine, kusali, kutii, na kadhalika). Ni kwa jinsi gani kufanya mambo haya kunatulinda sisi dhidi ya uovu?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Waefeso 2:13–19

Sisi ni “wenyeji” wa nyumbani mwake Mungu.

Watoto wanaimarishwa wanapokuwa na marafiki wazuri katika injili. Unawezaje kuwasaidia kujenga urafiki mzuri zaidi kati yao?

Picha
Shughuli ya Msingi

Sisi ni “wenyeji” pamoja na Watakatifu wa Mungu.

Shughuli Yamkini

  • Someni Waefeso 2:19 pamoja, na mjadiliane inamaanisha nini kuwa mgeni au mgeni kutoka nje ya inchi. Elezea tukio ambalo wewe ulijiona kama mgeni au mgeni kutoka nje ya nchi na mtu fulani akakusaidia kujisikia umekaribishwa na kukubalika. Waalike watoto kushiriki uzoefu kama huo. Tunaweza kufanya nini ili tuwe “wenyeji” badala ya kuwa wageni? Je, kuna watoto katika darasa lako wasiohudhuria kila mara, labda kwa sababu wanajiona kama wageni? Wasaidie watoto kuja na mpango wa kuwasaidia hao waumini kujisikia wamekaribishwa na wanapendwa.

  • Ili kuwasaidia watoto kuimarisha uhusiano na kila mmoja, andika maswali machache ubaoni ambayo yatawafanya mara moja washiriki kitu fulani kuhusu wao wenyewe, kama vile Lini uliweza kuona sala ikijibiwa? au Ni kitu gani upendacho kukifanya na familia yako? Wagawe watoto katika jozi, na waalike kuulizana maswali haya. Tulijifunza nini kuhusu kila mmoja wetu?

Waefeso 6:1–3

Baba wa Mbinguni ananitaka niwatii na kuwaheshimu wazazi wangu.

Fikiria kuhusu njia unazoweza kuwasaidia watoto kuelewa kwa nini ni muhimu kuwatii wazazi wao.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wasome Waefeso 6:1–3 binafsi na kutambua virai ambavyo vinawagusa. Waalike kushiriki virai hivi na kwa nini wanahisi virai hivi ni muhimu.

  • Waalike watoto kutafuta na kuzungumza kuhusu mifano ya watu katika maandiko ambao waliwatii na kuwaheshimu wazazi wao, kama vile Mwokozi (ona Luka 2:42–52), Ruthu (ona Ruthu 1), au Nefi (ona 1 Nefi 3:1–8). Kwa nini ni muhimu kuwatii na kuwaheshimu wazazi wetu?

  • Mpe kila mtoto kipande cha karatasi chenye neno heshimu juu yake. Jadili neno hilo lina maana gani. Waalike watoto kuandika au kuchora kwenye karatasi zao kitu wanachoweza kufanya ili kuonyesha kwamba wanawaheshimu wazazi wao.

Waefeso 6:10–18

Silaha ya Mungu inaweza kunilinda dhidi ya uovu.

Unaposoma Waefeso 6:10–18, fikiria baadhi ya hatari za kiroho ambazo watoto wanakabiliana nazo na jinsi unavyoweza kusaidia kuwaimarisha watoto dhidi ya hatari hizo.

Shughuli Yamkini

  • Wakati mtoto mmoja anaposoma Waefeso 6:10–18, muombe mtoto mwingine kuorodhesha au kuchora ubaoni vipande vya silaha vilivyotajwa. Kwa nini silaha ni muhimu katika mapambano? Tunawezaje kuvaa silaha za kiroho kila siku?

  • Mpangie kila mtoto achore na kuweka alama kipande cha silaha kilichoelezewa katika Waefeso 6:14–17. Je, ni kwa jinsi gani vipande hivi vya silaha vitatulinda dhidi ya uovu? Bwana anawaahidi nini hao wanaovaa silaha za Mungu? (ona Waefeso 6:13). Inamaanisha nini “kustahimili katika siku ya uovu”?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kumtafuta mtu mmoja wiki hii ambaye yawezekana anajisikia kuwa yu mgeni. Wape changamoto ya kufanya kitu fulani ili kumfikia mtu huyo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie watoto wadogo wajifunze kutoka kwenye maandiko. Watoto wadogo wanaweza kujifunza kutoka kwenye maandiko, lakini wanahitaji kufokasi katika mstari mmoja au hata kirai kimoja tu muhimu. Unaweza kuwaalika watoto kusimama wakati wanaposikia neno maalumu au kirai. (Ona kufundisha katika Nji ya Mwokozi25–26.)

Chapisha