Agano Jipya 2023
Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako


“Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
mama na mtoto wakijifunza maandiko

Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako

Kujifunza maandiko kama familia kila mara ni njia yenye nguvu zaidi ya kuisaidia familia yako kuona ushawishi wa Roho Matakatifu na kujifunza injili. Ni kiasi gani na kwa muda gani mnasoma kama familia siyo muhimu kama vile kuwa endelevu katika jitihada zenu. Unapofanya kujifunza kwako maandiko kuwa sehemu muhimu ya maisha ya familia yako, utawasaidia wanafamilia wako kuja karibu na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo na kujenga shuhuda zao juu ya msingi wa neno la Mungu. Fikiria kushauriana pamoja kuhusu maswali yafuatayo:

  • Je, ni kwa jinsi gani wanafamilia yako wanaweza kuhimizana kujifunza maandiko kama watu binafsi?

  • Je, wanafamilia yako wanaweza kufanya nini ili kuhimizana kushiriki kile wanachojifunza?

  • Je, ni kwa jinsi gani unaweza kusisitiza kanuni unazojifunza katika Agano Jipya kwenye nyakati za kila siku za kufundisha?

Kumbuka kwamba nyumbani ni mahali bora pa kujifunza injili. Unaweza kujifunza na kufundisha injili nyumbani katika njia ambazo haziwezekani katika darasa la Kanisani. Kuwa mbunifu unapofikiria njia za kuisaidia familia yako kujifunza kutoka kwenye maandiko. Fikiria baadhi ya mawazo yafuatayo ili kuboresha kujifunza maandiko kwa familia yako.

Picha
familia na viongozi wa Kanisa wakiimba pamoja nyumbani

Tumia Muziki

Imbeni nyimbo zinazoimarisha kanuni zinazofundishwa katika maandiko. Wimbo uliopendekezwa au wimbo wa watoto umeorodheshwa katika kila muhtasari wa wiki. Unaweza kuwauliza wanafamilia maswali kuhusu maneno au virai katika mashairi ya nyimbo. Kwa kuongezea kwenye kuimba, familia yako inaweza kutenda vitendo vinavyoendana na nyimbo au kusikiliza nyimbo zikiimbwa taratibu wakati wakifanya shughuli zingine. Kwa mawazo zaidi, ona “Kujumuisha Muziki Mtakatifu katika Kujifunza kwako Injili” katika nyenzo hii.

Shiriki Maandiko Yenye Maana Zaidi

Wape wanafamilia muda wa kuelezea vifungu vya maandiko ambavyo wameona vina maana zaidi wakati wa kujifunza kwao binafsi.

Tumia Maneno Yako Mwenyewe

Waalike wanafamilia kufanya muhtasari kwa maneno yao wenyewe kile wanachojifunza kutoka kwenye maandiko mnayojifunza.

Yafanyie kazi Maandiko katika Maisha Yako

Baada ya kusoma kifungu cha maandiko, waalike wanafamilia kuelezea jinsi kifungu hicho kinavyohusiana na maisha yao.

Uliza Swali

Waalike wanafamilia kuuliza swali la injili, na kisha kutumia muda kutafuta mistari inayoweza kusaidia kujibu swali hilo.

Onyesha picha

Chagua mstari unaouona una maana, na ubandike mahali ambapo wanafamilia watauona mara kwa mara. Waalike wanafamilia wengine kufanya zamu ya kuchagua andiko la kubandika.

Picha
mama ma watoto wakijifunza maandiko

Tengeneza Orodha ya Maandiko

Kama familia, chagueni mistari kadhaa ambayo mngependa kujadili wiki inayofuata.

Kariri Maandiko

Chagua kifungu cha maandiko ambacho kina maana kwa familia yako, na waalike wanafamilia kukikariri kwa kukirudia kila siku au kucheza mchezo wa kukariri.

Shiriki Masomo ya Vitendo

Tafuta vitu ambavyo vinahusiana na kanuni za injili katika mistari ambayo mnasoma kama familia. Waalike wanafamilia kuongelea jinsi gani kila kitu kinavyohusiana na mafundisho katika maandiko.

Chagua Mada

Waruhusu wanafamilia wafanye zamu za kuchagua mada ambayo familia itajifunza pamoja. Tumia Mwongozo wa Mada, Kamusi ya Biblia, au Mwongozo wa Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org) ili kutafuta vifungu vya maandiko kuhusu mada hiyo.

Chora picha

Someni mistari michache kama familia, na kisha toa muda kwa wanafamilia kuchora kitu kinachohusiana na kile mnachokisoma. Tumieni muda kujadili mchoro wa kila mmoja.

Igiza Hadithi

Baada ya kusoma hadithi, waalike wanafamilia kuiigiza. Baadaye, zungumzieni kuhusu jinsi hadithi hiyo inavyohusiana na mambo mnayopitia kama watu binafsi na kama familia.

Rais Russell M. Nelson alisema: “Ninakuahidi ya kwamba utakapofanya bidii kupanga upya nyumba yako ili iwe kituo cha kujifunza injili, baada ya muda siku zako za Sabato hakika zitakuwa za kupendeza sana. Watoto.wako watafurahia kujifunza na kuishi mafundisho ya Mwokozi, na ushawishi wa adui katika maisha yako na katika nyumba yako utapungua. Mabadiliko katika familia yako yatakuwa ya kuvutia na endelevu” (“Kuwa Mtakatifu wa Siku za Mwisho wa Mfano,” Liahona, Nov. 2018, 113).

Chapisha