Agano la Kale 2022
Mei 30–Juni 5. Waamuzi 2–4; 6–8; 13–16: “Bwana Akawainulia Mwokozi”


“Mei 30–Juni 5. Waamuzi 2–4; 6–8; 13–16: ‘Bwana Akawainulia Mwokozi,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Mei 30–Juni 5. Waamuzi 2–4; 6–8; 13–16,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Debora akiwa na majeshi

Kielelezo cha Debora akiongoza majeshi ya Israeli, © Lifeway Collection/licensed from goodsalt.com

Mei 30–Juni 5.

Waamuzi 2–4; 6–8; 13–16

“Bwana Akawainulia Mwokozi”

Maandiko yanashuhudia juu ya Yesu Kristo. Tafakari jinsi hadithi ulizozisoma katika Waamuzi zinavyokusaidia kuwa karibu na Yeye.

Andika Misukumo Yako

Wote tunajua ni jinsi gani ilivyo kutenda kosa, kujisikia vibaya kuhusu hilo, na kisha kutubu na kuamua kubadilisha njia zetu. Ila katika namna fulani tunasahau maamuzi yetu ya awali, na, tunapokabiliana na majaribu, tunaweza kujikuta tunafanya makosa tena. Mfumo huu mbaya ni sawa kabisa na uzoefu wa Waisraeli unaoelezewa katika kitabu cha Waamuzi. Wakishawishiwa na imani na matendo ya kuabudu ya Wakanaani—ambao walipaswa kuwafurusha kutoka kwenye nchi—Waisraeli walivunja maagano yao na Bwana na kugeukia mbali kutoka kwenye kumwabudu Yeye. Matokeo yake, walipoteza ulinzi Wake na kuanguka utumwani. Na bado kila mara jambo hili lilipotokea, Bwana aliwapa nafasi ya kutubu na kuwainulia mwokozi, kiongozi wa kijeshi aliyeitwa “mwamuzi.” Si waamuzi wote katika kitabu cha Waamuzi walikuwa waadilifu, ila baadhi yao walikuwa na imani kuu katika kuwakomboa wana wa Israeli na kuwarejesha katika uhusiano wa agano lao na Bwana. Hadithi hizi zinatukumbusha kwamba pasipo kujali chochote kilichotupeleka mbali kutoka kwa Yesu Kristo, Yeye ni Mkombozi wa Israeli na daima yupo tayari kutukomboa sisi na kutukaribisha tena Kwake.

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Waamuzi, ona “kitabu cha Waamuzi” katika kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Waamuzi 2:1–19; 4:1–16

Bwana ananipatia ukombozi ninapokosea.

Kitabu cha Waamuzi kinaweza kutumika kama onyo kwetu: hata bada ya uzoefu wa nguvu za Bwana katika maisha yetu, mara nyingi inawezekana kuanguka. Kitabu kinaweza pia kutoa hamasa kwa wale ambao huanguka, kwani Bwana anatoa njia ya kurudi. Mfano, unaposoma Waamuzi 2:1–19, angalia matendo yaliyowaongoza Waisraeli mbali kutoka kwa Bwana na jinsi gani Bwana alivyowakomboa. Ni nini mistari hii inakufundisha kuhusu Bwana? Unaweza kufanya nini ili uendelee kubaki mwaminifu zaidi Kwake?

Utakuta mpangilio wa uasi, huzuni, na ukombozi vimejirudia kote katika kitabu cha Waamuzi (ona hasa sura ya 3, 4, 6, na 13). Unasoma kitabu cha Waamuzi, tafakari kile waamuzi walichokifanya kuwakomboa Waisraeli na jinsi gani Mwokozi hukusadia pale unapohitaji ukombozi.

Mfano mmoja stahiki wa mtu aliyesaidia kuikomboa Israeli ni Debora. Soma kumhusu yeye katika Waamuzi 4:1–16, na angalia ushawishi aliokuwa nao juu ya watu waliomzunguka. Ni maneno yapi au matendo yapi ya Debora yanakuonyesha wewe kuwa alikuwa na imani katika Bwana? Unahisi Debora alimaanisha nini kwa swali lake katika mstari wa 14: “Je! Bwana hakutoka atangulie mbele yako?”

Ona pia Alma 7:13; Mafundisho na Maagano 84:87–88.

Waamuzi 2:13

Nani walikuwa Baali na Ashtarothi?

Baali alikuwa mungu wa dhoruba wa Wakanaani, na Ashtarothi alikuwa mungu wa kike wa rutuba wa Wakanaani. Kuabudu miungu hawa wawili inaonyesha ni jinsi gani rutuba ya ardhi na ya watu ni muhimu kwa Wakanaani. Jinsi watu walivyowaabudu hawa na miungu wengine wa uongo—ikijumuisha, nyakati nyingine, uovu wa uzinzi na sadaka za watoto—yalikuwa ni machukizo mbele za Bwana.

Waamuzi 6–8

Bwana anaweza kutenda miujiza nikiamini katika njia zake.

Ili kupokea miujiza ya Bwana katika maisha yetu, tunapaswa kuamini katika njia Zake, hata kama njia zake zinaonekana si za kawaida. Hadithi ya Gideoni, ipatikanayo katika Waamuzi 6–8, ni mfano mzuri wa hili. Ni kwa namna gani Bwana alitenda miujiza isiyotarajiwa wakati jeshi la Gideoni lilipowashinda Wamidiani? Je, unahisi Bwana anajaribu kukufundisha nini? Ni kwa jinsi gani umeona Bwana akifanya kazi Yake katika njia ionekanayo isiyo ya kawaida?

Ona Russell M. Nelson, “Kwa Mungu Hakuna Lisilowezekana,” Ensign, Mei 1988, 33–35.

Waamuzi 13–16

Nguvu hutokana na uaminifu kwa maagano yangu na Mungu.

Samsoni alipoteza vyote nguvu za kimwili na nguvu za kiroho kwa sababu alivunja maagano yake na Mungu, ikijumuisha yale ambayo yalihusika hususani kwa Wanazareti (kwa taarifa kuhusu Wanazareti, ona Hesabu 6:1–6; Waamuzi 13:7). Unaposoma hadithi ya Samsoni katika Waamuzi 13–16, tafakari kila agano ulilofanya. Ni kwa kiasi gani umebarikiwa kuwa na nguvu kwa sababu umeshika maagano hayo? Unajifunza nini kutoka katika hadithi ya Samsoni kinachokutia moyo kubaki mkweli kwenye maagano yako na Mungu?

Picha
Samsoni akisukuma nguzo

Samsoni Anaangusha Nguzo, na James Tissot pamoja na wengine

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Waamuzi 2:10.Baada ya Yoshua kufariki, kizazi kilichofuata cha Waisraeli “hawakumjua Bwana.” Ongea na familia yako kuhusu namna gani wanamjua Bwana na “kazi ambazo yeye [amefanya]” kwa ajili yao. Utahakikishaje kuwa maarifa haya yatahifadhiwa kwa ajili ya vizazi vijavyo?

Waamuzi 3:7–10.Mistari hii inafupisha mpangilio unaotokea mara nyingi katika kitabu chote cha Waamuzi. Wanafamilia yako wanaposoma mistari hii, wanaweza kugundua kile Waisraeli walichofanya kuasi kutoka kwa Bwana na kile Bwana alichofanya kuwakomboa. Ni kitu gani kinaweza kutuongoza kumsahau Bwana? Ni kwa jinsi gani Yeye anaweza kutukomboa? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwa na imani thabiti katika Yeye?

Waamuzi 6:13–16, 25–30.Gideoni alionyesha ujasiri mkubwa katika kumtii Bwana, ingawa matendo yake hayakuwa maarufu. Ni nini ambacho Bwana ametuomba tutende ambacho wengine wanaweza wasikubaliane nacho? Ni kwa namna gani maneno ya Bwana kwa Gideoni katika mstari wa 13–16 yanatuhamasisha kufanya jambo jema?

Waamuzi 7.Je, unaweza kutumia kuigiza au shughuli nyingine ya kiubunifu kusaidia familia yako kujifunza kutokana na uzoefu wa jeshi la Gideoni lililoelezewa katika sura hii? Ni kwa jinsi gani maneno ya Bwana katika sura hii (ona, kwa mfano,, mstari wa 2 na 15) yanatumika katika maisha yetu?

Waamuzi 13:5.Maagano ya Samsoni na Bwana yalimpa nguvu, kama ambavyo maagano yetu yanavyotupatia nguvu. Familia yako inaweza kufurahia kufanya baadhi ya mazoezi ya mwili na kujadili namna gani mazoezi hayo yanaweza kutusaidia kuwa na nguvu. Tunaweza kufanya nini ili kutusaidia kuwa wenye nguvu kiroho? Kwa ajili ya baadhi ya mawazo, wanafamilia wangeweza kusoma Mosia 18:8–10; Mafundisho na Maagano 20:77, 79. Ni kwa jinsi gani kushika maagano yetu kunatupa nguvu za kiroho?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Redeemer of Israeli,” Nyimbo za Kanisa, na. 6.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Fanyia kazi kile unachojifunza. Unaposoma, jiulize namna gani unaweza kutumia kile unachojifunza, na kuweka sharti kukifanya. Mruhusu Roho akuongoze. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 35.)

Picha
Gideoni na jeshi

Jeshi la Gideoni, na Daniel A. Lewis

Chapisha