Agano la Kale 2022
Mei 23–29. Yoshua 1–8; 23–24: “Iweni Hodari na Moyo wa Ushujaa”


“Mei 23–29. Yoshua 1–8; 23–24: ‘Iweni Hodari na Moyo wa Ushujaa,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Mei 23–29. Yoshua 1–8; 23–24,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Musa akimsimika Yoshua

Kielelezo cha Musa akimsimika Yoshua, na Darrell Thomas

Mei 23–29

Yoshua 1–8; 23–24

“Iweni Hodari na Moyo wa Ushujaa”

Unaposoma kitabu cha Yoshua, tafakari vitu ulivyosoma kuhusu Waisraeli vinavyoweza kuongeza imani yako katika Yesu Kristo.

Andika Misukumo Yako

Ilikuwa imechukua vizazi vingi, lakini ahadi ya Bwana ilikuwa karibu kutimizwa: wana wa Israeli walikuwa kwenye ukingo wa kurithi nchi ya ahadi. Ila katika njia yao ulisimama Mto Yordani, kuta za Yeriko, na waovu lakini watu wenye nguvu waliomkataa Bwana (ona 1 Nefi 17:35). Juu ya hayo, kiongozi wao mpendwa Musa alikuwa ameondoka. Hali ingewafanya baadhi ya Waisraeli kujihisi dhaifu na waoga, ila Bwana alisema, “Iweni hodari na moyo wa ushujaa.” Kwa nini walipaswa kujisikia namna hii? Sio kwa sababu ya nguvu zao wenyewe—au hata za Musa au Yoshua—ila kwa sababu “Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako” (Yoshua 1:9). Tunapokuwa na mito yetu ya kuvuka na kuta za kubomoa, vitu vya kushangaza vinaweza kutokea katika maisha yetu, kwa sababu ni “Bwana [ambaye] atatenda mambo ya ajabu kati [yetu]” (Yoshua 3:5).

Kwa ajili ya muhtasari wa kitabu cha Yoshua, ona “kitabu cha Yoshua” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
Learn More image
Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Yoshua 1:1–9

Mungu atakuwa pamoja nami ikiwa nitakuwa mwaminifu Kwake.

Fikiria jinsi ambavyo ilikuwa kwa Yoshua kuitwa kuwa mbadala wa Musa. Angalia kile Bwana alichosema katika Yoshua 1:1–9 ili kumpa moyo. Fikiria changamoto ngumu unazokabiliana nazo; ni nini katika mistari hii kinakupa moyo?

Inaweza kuwa ya kufurahisha kuona kwamba jina Yoshua (Yehoshua au Yeshua kwa Kiebrania) linamaanisha “Yehova anaokoa.” Na jina Yesu linatoka katika neno Yeshua. Kwa hiyo kadri unavyosoma kuhusu Yoshua, zingatia namna gani misheni yake ya kuwaongoza wana wa Israeli katika nchi ya ahadi inakukumbusha kuhusu misheni ya Mwokozi.

Ona pia Ann M. Dibb, “Kuwa mwenye Moyo Mkuu,” Liahona, Mei 2010, 114–16.

Yoshua 2

Vyote imani na matendo ni muhimu kwa wokovu.

Wakristo wa kale walimwona Rahabu kama mfano wa nguvu ya vyote viwili imani na matendo (ona Waebrania 11:31; Yakobo 2:25). Unaposoma Yoshua 2, fikiria wajibu wa imani ya Rahabu na matendo katika kujiokoa mwenyewe, familia yake, na wapelelezi wa Waisraeli. Hili linakufundisha nini wewe kuhusu namna gani imani yako katika Kristo na matendo yako vinaweza kukushawishi wewe na wengine?

Unaweza kuwa na hamu ya kujua kwamba Rahabu alikuwa ni mhenga wa wote Mfalme Daudi na Yesu Kristo (ona Mathayo 1:5). Ni somo lipi tunaweza kujifunza kutoka katika hili?

Picha
Rahabu

Rahabu dirishani kwake. Kusubiri Ahadi, na Elspeth Young.

Yoshua 3–4

Ninaweza kupata uzoefu wa “maajabu” ya Mungu ikiwa nina imani katika Yesu Kristo.

Bwana anatamani kwamba “watu wote wa duniani wapate kujua mkono wa Bwana, ya kuwa ni mkono wenye uweza” (Yoshua 4:24). Unaposoma Yoshua 3–4, tafakari jinsi unavyojua mkono wa Bwana ni wenye uweza. Ni kwa namna gani Bwana ametenda “maajabu” maishani mwako ? (Yoshua 3:5). Unawezaje kupata uzoefu—au kutambua—maajabu hayo mara kwa mara? (kwa mfano, ona Yoshua 3:17).

Kwa nini unafikiri Waisraeli walihitaji kujitakasa wenyewe kabla ya kuvuka Mto Yordani? Ni umuhimu gani unaupata katika ukweli kwamba mto uligawanyika tu baada ya “nyayo za makuhani … kutiwa katika maji ya ukingoni”? (Yoshua 3:13, 15).

Kwa matukio mengine ya muhimu yaliyotokea katika Mto Yordani, ona 2 Wafalme 2:6–15; 5:1–14; na Marko 1:9–11. Unapotafakari maandiko haya, ni muunganiko gani unauona kati ya matukio haya?

Ona pia Gérald Caussé, “Je, Bado ni Nzuri Sana Kwako?Liahona, Mei 2015, 98–100; “Exercise Faith in Christ” (video), ChurchofJesusChrist.org.

Yoshua 6–8

Utiifu huleta nguvu za Mungu katika maisha yangu.

Sura hizi zinahusika na vita juu ya nchi ya Yeriko na Ai. Unapozisoma, fikiria jinsi unavyopambana na majaribu katika maisha yako mwenyewe (kwa mfano, ona Yoshua 7:10–13). Unajifunza nini kuhusu jinsi Mungu anavyoweza kukusaidia na nini unachoweza kufanya kufikia nguvu Zake? Kwa mfano, ni nini kinakuvutia kuhusu maelekezo ya Bwana kwa ajili ya kuichukua Yeriko? (ona Yoshua 6:1–5). Labda maelezo katika Yoshua 7 yatakushawishi wewe kuamua ikiwa “kuna kitu kilichowekwa wakfu” katika maisha yako unachohitaji kuondoa (Yoshua 7:13).

Yoshua 23–24

“Ambatana na Bwana Mungu wako.”

Baada ya kuigawanya nchi ya ahadi kati ya kabila kumi na mbili za Israeli (ona Yoshua 13–21), Yoshua aliwapa mafundisho yake ya mwisho. Unaposoma mafundisho haya katika Yoshua 23–24, unaweza kuweka orodha ya maonyo, ushauri, na baraka zilizoahidiwa ulizoziona. Kwa kuzingatia kila kitu ambacho Waisraeli walikuwa wamepitia, kwa nini unafikiri Yoshua aliamua kuwaambia mambo haya wakati wa siku za mwisho za uhai wake? Unapata nini ambacho kinakutia msukumo “kuambatana na Bwana”? (Yoshua 23:8).

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Yoshua 1:8.Mstari huu unapendekeza nini kuhusu jinsi tunavyoweza kufanyia kazi kujifunza kwetu binafsi maandiko na kama familia? Ni kwa jinsi gani maandiko “yamefanikisha njia zetu” na “kutusitawisha sana”?

Yoshua 4:3, 6–9.Baada ya kusoma kile ambacho Bwana aliwataka Waisraeli kufanya kwa mawe kutoka Mto Yordani, familia yako ingeweza kuzungumza kuhusu mambo makubwa ambayo Bwana amewafanyia. Baadae ungeweza kutoa jiwe kwa kila mwanafamilia na kuwaalika kuchora au kuandika jambo lolote ambalo Bwana amewafanyia.

Yoshua 6:2–5.Familia yako inaweza kuwa na burudani wakiigiza maelekezo Bwana aliyowapa Waisraeli ili kuishinda Yeriko. Ni nini Bwana anaweza kututaka sisi kujifunza kutokana na hadithi hii?

Yoshua 24:15.Baada ya kusoma mstari huu, wanafamilia wanaweza kushiriki uzoefu ambapo walichagua kumtumikia Bwana ingawa ilikuwa vigumu. Kwa nini ni muhimu kufanya uchaguzi wa kumtumikia Yeye “siku hii” badala ya kusubiri kuamua mpaka hali itakapojitokeza? Tunawezaje kuwaunga mkono wanafamilia wa “nyumba” yetu pale tunapojitahidi “kumtumikia Bwana”?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Choose the Right,” Nyimbo za Kanisa, na. 239.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Toa ushuhuda wako kila mara. Ushuhuda wako wa dhati wa ukweli unaweza kuathiri kwa nguvu familia yako. Hauhitaji kuwa wa kushawishi au mrefu. Ushuhuda unakuwa na nguvu zaidi unapokuwa wa moja kwa moja na wa kutoka moyoni. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 11.)

Picha
Kuta za Yeriko zikianguka

Bwana alisababisha kuta za Yeriko kuanguka. © Providence Collection/licensed from goodsalt.com

Chapisha