Agano la Kale 2022
Septemba 5–11. Isaya 1–12; “Mungu Ni Wokovu Wangu”


“Septemba 5–11. Isaya 1–12: ‘Mungu Ni Wokovu Wangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Septemba 5–11. Isaya 1–12,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Famila: 2022

Picha
nabii wa kale anaandika

Nabii Isaya Atabiri Kuzaliwa kwa Kristo, na Harry Anderson

Septemba 5–11

Isaya 1–12

“Mungu Ni Wokovu Wangu”

Tafuta mwongozo wa kiroho unapojifunza. Maneno ya Isaya yanaeleweka vizuri wakati “tunapojawa na roho wa unabii,” kama alivyofundisha Nefi (2 Nefi 25:4).

Andika Misukumo Yako

Hata ikiwa hii ni mara yako ya kwanza kusoma kitabu cha Isaya, unaweza kupata vifungu ambavyo vinaonekana kuwa vya kawaida. Hiyo ni kwa sababu, kati ya manabii wote wa Agano la Kale, Isaya ndiye anayenukuliwa mara nyingi katika vitabu vingine vya maandiko, pamoja na Mwokozi mwenyewe. Maneno ya Isaya pia huonekana mara nyingi katika nyimbo na muziki mwingine mtakatifu. Kwa nini Isaya amenukuliwa mara nyingi?

Hakika sehemu ya sababu ni kwamba Isaya alikuwa na kipawa cha kuelezea neno la Mungu kwa lugha ya wazi, ya kukumbukwa. Lakini ni zaidi ya hilo. Isaya amewatia moyo manabii kwa vizazi kwa sababu kweli alizofundisha zilivuka kizazi chake mwenyewe—Waisraeli walioishi kati ya 740 na 701 KK. Jukumu lake lilikuwa kufungua macho yetu kwa kazi kubwa ya Mungu ya ukombozi, ambayo ni kubwa zaidi kuliko taifa moja au wakati mmoja. Kutoka kwa Isaya, Nefi alijifunza kwamba yeye na watu wake, ingawa walitengwa na Israeli ingine, bado walikuwa sehemu ya watu wa agano la Mungu. Katika Isaya, waandishi wa Agano Jipya walipata unabii juu ya Masiya ambao ulikuwa ukitimizwa mbele ya macho yao. Na katika Isaya, Joseph Smith alipata msukumo kwa kazi ya siku za mwisho ya kukusanya Israeli na kujenga Sayuni. Unaposoma Isaya, utapata nini?

Kwa mengi kuhusu Isaya na maandiko yake, ona “Isaya” katika Kamusi ya Biblia. Kwa taarifa kuhusu muda ambao Isaya aliishi, ona 2 Wafalme 15–20 na 2 Mambo ya Nyakati 26–32.

Picha
Learn More image
Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Isaya 1–12

Ninawezaje kuelewa vyema mafundisho ya Isaya?

Akizungumzia maandishi ya Isaya, Mwokozi alisema, “Mpekue hivi vitu kwa bidii; kwani maneno ya Isaya ni makuu” (ona 3 Nefi 23:1–3). Walakini kwa wengi, Isaya inaweza kuwa vigumu kuielewa. Hivi ni baadhi ya vidokezo vya kukusaidia kupata maana zaidi katika maneno ya Isaya:

  • Tafakari ishara na sitiari aliyotumia Isaya. Kwa mfano, tafakari kile unachofikiria Isaya alitaka kuwasiliana wakati aliandika juu ya shamba la mizabibu (ona Isaya 5:1–7), maji ya Shilohi (ona Isaya 8:5–10), bendera (ona Isaya 5:26), na bendera (ona Isaya 11:10, 12).

  • Kwa kila sura unayosoma, jiulize mwenyewe, “Ninajifunza nini kuhusu Yesu Kristo?” (ona 1 Nefi 19:23).

  • Tafuta mada ambazo zinaonekana kufaa kwa siku zetu, kama vile maisha na huduma ya Yesu Kristo, kutawanyika na kukusanyika kwa Israeli, siku za mwisho, na Milenia. Unaweza pia kuweka orodha ya marejeo kutoka kwa Isaya ambayo yanafundisha juu ya mada hizi.

  • Tumia visaidizi vya kujifunza vinapopatikana, kama vile kamusi, tanbihi ya Biblia, vichwa vya sura, na Mwongozo wa Maandiko.

Ona pia 2 Nefi 25:1–8.

Isaya 1; 3;5

“Acheni kutenda mabaya.”

Isaya aliendelea kuuonya Ufalme wa Yuda juu ya hali yao ya kiroho. Baada ya kusoma Isaya 1, 3, na 5, unawezaje kuelezea hali ya kiroho ya watu? Je! Ni maonyo gani unayoyapata ambayo unahisi yanafaa kwa siku zetu?

Mbali na maonyo, unaweza pia kuandika jumbe za matumaini kwa Israeli yenye dhambi (ona, kwa mfano, Isaya 1:16–20, 25–27; 3:10). Je, unajifunza nini kumhusu Bwana kutoka kwenye jumbe hizi?

Isaya 2; 4; 11–12

Mungu atatenda kazi kubwa katika siku za mwisho.

Maandiko mengi ya Isaya ni unabii ambao una maana maalum kwa ajili ya siku zetu. Ni yapi kati ya maelezo ya Isaya ya siku za mwisho katika sura ya 2; 4; 11–12 yanakutia moyo haswa? (Mafundisho na Maagano 113:1–6 hutoa ufahamu wa kusaidia kuhusu Isaya 11.) Unajifunza nini kuhusu kukusanyika kwa Israeli na ukombozi wa Sayuni? Je, unahisi kutiwa msukumo kufanya nini baada ya kusoma sura hizi?

Ona pia Isaya 5:26; 10:20.

Isaya 6

Manabii wanaitwa na Mungu.

Katika sura ya 6, Isaya alisimulia wito wake wa kuwa nabii. Unaposoma sura hii, ni nini kinachokuvutia juu ya kile ambacho Isaya alipitia? Ni kwa jinsi gani sura hii inashawishi jinsi unayofikiria juu ya Bwana, manabii Wake, na kazi ambayo wameitwa kuifanya?

Picha
mwanamke amemshika mtoto

“ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume” (Isaya 9:6).

Isaya 7–9

Isaya alitoa unabii juu ya Kristo.

Mwanzoni mwa huduma ya Isaya, Ufalme wa Israeli (pia huitwa Efraimu) uliunda muungano na Shamui ili kujilinda dhidi ya Ashuru. Israeli na Shamu zilitaka kumlazimisha Ahazi, mfalme wa Yuda, ajiunge na muungano wao. Lakini Isaya alitabiri kwamba muungano huo utashindwa na akamshauri Ahazi amtegemee Bwana (ona Isaya 7–9, hususani Isaya 7:7–9; 8:12–13).

Kama vile Isaya alivyomshauri Ahazi, alitoa unabii kadhaa maarufu, kama vile ule unaopatikana katika Isaya 7:14; 8:13–14; 9:2, 6–7. Ingawa haijulikani kabisa unabii huu ulimaanisha nini wakati wa Ahazi, ni wazi unatumika kwa Yesu Kristo (ona pia Mathayo 1:21–23; 4:16; 21:44; Luka 1:31–33). Unajifunza nini kumhusu Mwokozi kutoka kwenye mistari hii?

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Isaya 1:16–18.Ili kuwasaidia wana familia kuelewa mistari hii, ungeweza kusoma sehemu ya “Baadhi Yetu Tunahisi Kamwe Hatuwezi Kuwa Vazuri vya Kutosha” kutoka kwenye ujumbe wa Dada Sharon Eubank “Kristo: Ni Nuru Iangazayo Gizani” (Ensign au Liahona, Mei 2019,75). Au unaweza kuonyesha jinsi madoa yanavyoweza kuondolewa kwenye mavazi. Ni jinsi gani ujumbe wa Bwana katika mistari hii ni tofauti na kile anachotaka Shetani tuamini?

Isaya 2:1–5.Wanafamilia wangeweza kuchukua mojawapo ya mistari hii na kuchora kile inachoeleza. Je! Hekalu linatufundisha nini juu ya njia za Bwana? Je, tunabarikiwa vipi “tunapotembea katika nuru ya Bwana”? (Isaya 2:5).

Isaya 4:5–6.Je! Bwana anatuahidi nini katika mistari hii? Je, ahadi hizi zinaweza kumaanisha nini? Ni jinsi gani Yeye anazitimiza? (Ona pia Kutoka 13:21–22.)

Isaya 7:14; 9:1–7.Kutumia michoro au picha kutoka kwenye majarida ya Kanisa, unaweza kutengeneza bango kuonyesha baadhi ya mambo tunayojifunza kuhusu Yesu Kristo kutoka kwenye mistari hii.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “High on the Mountain Top,” Nyimbo za Kanisa, na. 5

Kuboresha Kujifunza Kibinafsi.

Muombe Bwana msaada. Ili kuelewa maandiko, tunahitaji ufunuo binafsi. Bwana ameahidi “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa” (Mathayo 7:7).

Picha
Hekalu la Idaho Falls Idaho katika dhoruba

Isaya alifundisha kwamba tabanakulo lingekuwa “mahali pa kukimbilia” na “pa kujificha wakati wa tufani na mvua” (Isaya 4:6).Hekalu la Idaho Falls Idaho

Chapisha