Agano la Kale 2022
Septemba 19–25. Isaya 40-49; “Watulizeni Mioyo, Watu Wangu”


“Septemba 19–25. Isaya 40–49; ‘Watulizeni Mioyo, Watu Wangu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Septemba 19–25. Isaya 40–49,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Famila: 2022

Picha
Yesu akimponya kipofu

Akimponya Kipofu, na Carl Heinrich Bloch

Septemba 19–25

Isaya 40–49

“Watulizeni Mioyo, Watu Wangu”

Isaya mara nyingi alitumia lugha ya mifano. Zingatia mawazo na hisia ambazo ishara hizi huleta akilini na moyoni mwako. Hii inaweza kukusaidia wewe zaidi kuelewa kile alichofundisha.

Andika Misukumo Yako

“Watulizeni” ni neno la kwanza la Isaya sura ya 40. Inaashiria mwanzo wa sauti tofauti, mkazo tofauti katika ujumbe wa nabii. Ambapo maandishi ya mwanzo ya Isaya yalionya Israeli na Yuda juu ya uharibifu na utekaji ambao utakuja kwa sababu ya dhambi zao, unabii huu wa baadaye ulikusudia kuwafariji Wayahudi zaidi ya miaka 150 baadaye—baada ya Yerusalemu kuharibiwa, hekalu lilinajisiwa, na watu walichukuliwa mateka na Babeli. Lakini unabii huu unafika hata mbali zaidi katika siku za usoni kuliko kwa Waisraeli walioshindwa, waliovunjika moyo. Wanazungumza nasi, ambao wakati mwingine pia huhisi kushindwa, kuvunjika moyo, na hata kupotea.

Ujumbe wa Isaya kwao na kwetu ni rahisi “Msiogope” (Isaya 43:1). Vyote havijapotea. Bwana hajakusahau, na Yeye ana nguvu juu ya hali ambazo zinaonekana kuwa nje ya udhibiti wako. Je! Bwana sio “aliyeziumba mbingu, na … aliyeitandaza nchi na … yeye awapaye pumzi watu walio juu yake”? (Isaya 42:5). Je! Yeye hana nguvu zaidi kuliko Babeli, kuliko dhambi, kuliko chochote kinachokushikilia mateka? “Unirudie,” Yeye anasihi, “maana nimekukomboa.” (Isaya 44:22). Anaweza kuponya, kurejesha, kutia nguvu, kusamehe, na kufariji—chochote kinachohitajika kwako, kwa upande wako, ili kukombolewa.

Kujifunza jinsi Nefi na Yakobo walivyofanana Isaya 48–49 kwa watu wao, ona 1 Nefi 22 na 2 Nefi 6.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Isaya 40–49

Yesu Kristo anaweza kunifariji na kunipa tumaini.

Lazima ilikatisha tamaa, na hata ikawaumiza, kwa Waisraeli kujikuta wenyewe mateka huko Babeli. Wengi wanaweza kujiuliza ikiwa walikuwa wamepoteza milele nafasi yao kama watu wateule wa agano la Mungu. Unaposoma Isaya 40–49, tafuta vifungu ambavyo vingeweza kutoa faraja na tumaini. Kwa kila kifungu unachopata, tafakari na uandike kile Bwana anaweza kuwa anasema kwako katika mistari hii. Hapa kuna mistari michache ambayo unaweza kuanza nayo.

Unawezaje kushiriki jumbe hizi na mtu ambaye anahitaji kutiwa moyo au matumaini? (ona Isaya 40:1–2).

Ona pia Jeffrey R. Holland, “Mwangaza Kamili wa Tumaini,” Ensign au Liahona, Mei 2020, 81-84.

Picha
mto kwenye msitu

Kwa kumtii Bwana, tunaweza kuwa na “amani … kama mto” (Isaya 48:18).

Isaya 40:3–8, 15–23; 42:15–16; 47:7–11

Nguvu za Mungu ni kubwa kuliko za ulimwengu.

Isaya aliwakumbusha watu wake mara kwa mara juu ya nguvu isiyo na kifani ya Mungu, hata ikilinganishwa na nguvu dhalimu ya kidunia iliyowazunguka. Tafuta ujumbe huu unaposoma Isaya 40:3–8, 15–23; 42:15–16; na 47:7–11 (kumbuka kwamba sura ya 47 imeelekezwa kwa mtekaji nyara wa Israeli, Babeli). Je, vifungu hivi vinakufundisha nini kuhusu mambo ya kidunia? Vinakufundisha nini kuhusu Mungu? Tafakari kwa nini ujumbe huu unaweza kuwa muhimu kwa Wayahudi walioko utumwani. Kwa nini una thamani kwako?

Ona pia “Abide with Me!Nyimbo za Kanisa, na. 166.

Isaya 41:8–13; 42:1–7; 43:9–12; 44:21–28; 45:1–4; 48:10; 49:1–9

“Wewe ni mtumishi wangu;”

Kote katika Isaya 40–49 Bwana anazungumza juu ya “mtumishi” Wake na “mashahidi” Wake. Katika baadhi ya vifungu maneno haya yanaonekana kumrejea Yesu Kristo (ona Isaya 42:1–7), vingine vinataja nyumba ya Israeli (ona Isaya 46:4), na vingine vinamtaja Mfalme Koreshi, ambaye aliruhusu Wayahudi kurudi kwenda Yerusalemu na kujenga upya hekalu (ona 44:26–45:4.). Katika kila kisa, hata hivyo, unaweza pia kufikiria jinsi vifungu vinavyotumika kwako kama mtumishi na shahidi wa Bwana. Kwa mfano, tafakari maswali kama haya:

Isaya 41:8–13; 42:6; 44:21. Je! Bwana amekuita ufanye nini? Fikiria miito rasmi ya Kanisa pamoja na majukumu mengine ya agano ya kumtumikia. Je, Yeye anakusaidiaje na “kukushika mkono [wako] (Isaya 42:6) ukiwa unahudumu? Je! “Amekuumbaje” wewe kuwa mtumishi wake? (ona pia Isaya 48:10).

Isaya 43:9–12. Ni namna gani wewe umekuwa shahidi wa Yesu Kristo? Ni uzoefu upi katika maisha yako umekuonyesha kuwa Yeye ni Mwokozi?

Isaya 49:1–9. Ni jumbe zipi unazipata katika mistari hii ambazo zinaweza kusaidia wakati juhudi zako na huduma zinaonekana kuwa “si kitu, na ni bure”? (mstari wa 4).

Ona pia Mosia 18:9; Henry B. Eyring, “Mtoto na Mfuasi,” Ensign au Liahona, Mei 2003, 29-32.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Isaya 40:3–4.Kuchunguza nini inaweza kumaanisha “kuandaa… njia ya Bwana,” familia yako inaweza kunyoosha kitu kilichopotoka, kusafisha sakafu chafu, au kufanya njia wazi kwenye ardhi ya miamba. Pia ungeweza kuonyesha picha za Yohana Mbatizaji na Joseph Smith (ona Kitabu cha Sanaa cha Injili, na. 35,87). Je, waliandaaje njia kwa ajili ya ujio wa Bwana? (ona Luka 3:2–18; Mafundisho na Maagano 135:3). Je, tunaandaaje njia kwa ajili Yake? (kwa mfano, ona Mafundisho na Maagano 33:10.).

Isaya 40:28; 43:14–15; 44:6.Ni majina gani au vyeo vya Yesu Kristo tunavyovipata katika mistari hii? Kila jina linatufundisha nini kumhusu Yeye?

Isaya 41:10; 43:2–5; 46:4.Mistari hii inapatikana katika wimbo “How Firm a Foundation” (Nyimbo za Dini, na 85). Familia yako inaweza kufurahia kuimba wimbo pamoja na kupata virai ndani yake ambavyo ni sawa na virai katika mistari hii. Ni nini virai hivi vinatufundisha kumhusu Yesu Kristo?

Isaya 44:3–4; 45:8.Baada ya kusoma mistari hii, familia yako inaweza kumwagilia mmea unapozungumza juu ya baraka ambazo Bwana amemwaga juu yao. Ni nini kinachotokea kwa mmea wakati unamwagiliwa maji? Bwana anatarajia nini kutoka kwetu Anapotubariki?

Isaya 48:17–18.Fikiria kuonyesha picha au video za mito na mawimbi ya bahari. Amani inaweza kuwa kama mto vipi? Je! wema unawezaje kuwa kama mawimbi?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “How Firm a Foundation,” Nyimbo za Kanisa, na. 85.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Fafanua maneno. Jaribu kutafuta ufafanuzi wa maneno katika maandiko ambayo huyaelewi—na hata maneno unayofikiria unayaelewa. Wakati mwingine ufafanuzi unaweza kukusaidia kusoma mstari kwa njia tofauti na kupata umaizi mpya wa kiroho.

Picha
Yesu pamoja na msichana na mwanamume.

“Bwana amewafariji watu wake, Naye atawahurumia watu wake walioteswa” (Isaya 49:13).Marhamu ya Giliadi na Anne Adele Henrie

Chapisha