Agano la Kale 2022
Agosti 29–Septemba 4. Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12 “Kumcha Bwana Ni Mwanzo wa Hekima”


“Agosti 29–Septemba 4. Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12; ‘Kumcha Mungu Ni Mwanzo wa Hekima,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Agosti 29–Septemba 4. Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
mwanaume akisoma maandiko

Agosti 29–Septemba 4

Mithali 1–4; 15–16; 22; 31; Mhubiri 1–3; 11–12

“Kimcha Mungu Ni Mwanzo wa Hekima”

Fikiria jinsi kusoma kwako Mithali na Mhubiri kunaweza kukusaidia “tega sikio lako kusikia hekima, ukauelekeza moyo wako upate kufahamu” (Mithali 2:2).

Andika Misukumo Yako

Katika sura ya kwanza ya kitabu cha Mithali, tunapata maneno haya: “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako,” (Mithali 1:8). Mithali inaweza kuonekana kama mkusanyiko wa maneno ya busara kutoka kwa mzazi mwenye upendo, ambaye ujumbe wake mkuu ni kwamba baraka za amani na mafanikio huja kwa wale wanaotafuta hekima—haswa aina ya hekima ambayo Mungu hutoa. Lakini Mithali inafuatwa na kitabu cha Mhubiri, ambacho kinaonekana kusema, “Sio rahisi hivyo.” Mhubiri aliyenukuliwa katika Mhubiri aliona kwamba “Akatia moyo [wake] ili kuijua hekima” lakini bado alipata “kujilisha upepo” na “wingi wa huzuni” (Mhubiri 1:17–18). Kwa njia tofauti, kitabu kinauliza, “Je! Kunaweza kuwa na maana halisi katika ulimwengu ambao kila kitu kinaonekana kuwa bure, cha muda mfupi, na hakina uhakika?”

Na bado, wakati vitabu viwili vinaangalia maisha kwa mitazamo tofauti, vinafundisha ukweli sawa. Mhubiri anatangaza: “Jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu” (Mhubiri 12:13). Hi ni kanuni ile ile inayopatikana katika Mithali: “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote. … Usiwe mwenye hekima machoni pako; Mche Bwana” (Mithali 3:5,7). Haijalishi maisha yana nini, hata wakati inaonekana kuwa ya kutatanisha na ya kubahatisha, ni bora kila wakati kumtumaini Bwana Yesu Kristo.

Kwa ajili ya muhtasari wa vitabu hivi, ona “Mithali, kitabu cha” na “Mhubiri” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Mithali 1–4; 15–16

“Tega sikio lako kusikia hekima.”

Kitabu cha Mithali kimejaa ufahamu juu ya hekima. Fikiria kuweka alama neno “hekima” na maneno yanayohusiana, kama “maarifa” na “ufahamu,” kama unavyoyapata katika sura ya 1–4 na 15–16. Ni kwa jinsi gani sura hizi zinaathiri jinsi unavyofikiri kuhusu hekima? Kutokana na unachokitafuta, ni kwa vipi utaielezea hekima ambayo “Bwana anatoa”? (Mithali 2:6). Fikiria jinsi unavyotafuta msaada wa Bwana wa kuwa mwenye “hekima moyoni” (Mithali 16:21). Ni baraka zipi huja kutokana na hekima ya Mungu?

Ona pia Mithali 8–9; Mathayo 7:24–27; 25:1–13.

Mithali 1:7; 2:5; 16:6; 31:30; Mhubiri 12:13

“Kumcha Bwana” ni nini?

Mzee David A Bednar anaelezea: “Tofauti na woga wa kilimwengu ambao husababisha hofu na dukuduku, kucha kiungu ni chanzo cha amani, uhakika, na matumaini. … Inajumuisha hisia ya ndani ya unyenyekevu, heshima na kumcha Bwana Yesu Kristo; utii kwa amri Zake; na kutarajia Hukumu ya Mwisho na haki mikononi Mwake. … Uchaji wa kiungu ni kumpenda na kumtuamini Yeye” (“Kwa hiyo Wakaondoa Hofu Yao; Liahona, Mei 2015, 48–49).

Ona pia Mithali 8:13.

Mithali 4

“Ulisawazishe pito la mguu wako.”

Mithali 4 inaelezea hekima na haki kama “njia” au “mapito” (ona pia Mithali 3:5–6). Unaposoma sura hii, unaweza kupata vifungu ambavyo vinakusaidia kutafakari “pito la miguu yako” (mstari wa 26) na jinsi hatua zako zinavyokusogeza karibu na Bwana. Kwa mfano, nini mstari wa 11–12 and 18–19 inakufundisha kuhusu baraka za kufuata njia sahihi? Je mstari wa 26 na 27 ina maana gani kwako?

Ona pia 2 Nefi 31:18–21.

Mithali 15:1–2, 4, 18,28; 16:24–32

“Jawabu la upole hugeuza hasira”

Baadhi ya mithali katika sura za 15 na16 zinaweza kukuhimiza kuboresha jinsi unayowasiliana na wengine, haswa wapendwa. Kwa mfano, fikiria juu ya nyakati maalum ambapo ungeweza kutumia “jibu la upole” badala ya “maneno yaumizayo” (Mithali 15:1). Ni kwa jinsi gani ushauri katika Mithali 16:24–32 unakusaidia kufikiri kuhusu maneno unayotumia?

Fikiria ufahamu huu kutoka kwa Mzee W. Craig Zwick: “Jibu la ‘upole’ ni jibu lenye busara—maneno yenye nidhamu kutoka kwa moyo mnyenyekevu. Haimaanishi kamwe hatuzungumzi moja kwa moja au kwamba tunalegeza ukweli wa mafundisho. Maneno ambayo yanaweza kuwa thabiti katika habari yanaweza kuwa ya upole moyoni” (“Unafikiria Nini?Liahona, Mei 2014,42).

Picha
mwanamke akimlisha ndege wa bahari

Nani Anaweza Kumpata Mwanamke Mwema?II, na Louise Parker

Mithali 31:10–31.

“Mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.”

Mithali 31:10–31 inaelezea “mwanamke mwema,” au mwanamke mwenye nguvu kubwa ya kiroho, uwezo, na ushawishi. Unaweza kujaribu kufupisha kwa maneno yako mwenyewe nini kila moja ya aya hizi zinasema juu yake. Je! Ni tabia gani zingine ambazo unaweza kuiga?

Mhubiri 1–3;12

Maisha ya Duniani ni ya muda.

Kwa nini ni muhimu kwako kukumbuka kwamba mengi katika ulimwengu huu, kama vile Mhubiri 1–2 inasisitiza, ni “ubatili” (au ni ya muda na mara nyingi siyo muhimu)? Unagundua nini katika sura ya 12 ambayo huupatia uzima thamani ya milele?

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Mithali.Familia yako inaweza kufurahia kuunda “kitabu chenu cha Mithali”—mkusanyiko wa ushauri wa busara kutoka kwenye maandiko na manabii wa siku za mwisho.

Mithali 1:7; 2:5; 16:6; Mhubiri 12:13–14.Ili kuwasaidia wanafamilia kuelewa Mithali 1:7; 2:5; 16:6; Mhubiri 12:13, inaweza kusaidia kubadilisha neno hofu na neno kama unyenyekevu, upendo, au utiifu (ona pia Waebrania 12:28). Ni kwa jinsi gani hii inaathiri jinsi tunavyofikiria kuhusu mistari hii? Ni kwa jinsi gani tunaonyesha kwamba tunamcha Bwana?

Mithali 3:5–7.Ili kuwasaidia wanafamilia kuona nini mistari hii inafundisha, unaweza kuwaomba waegemee kwenye kitu kilicho imara na thabiti, kama ukuta. Kisha wangeweza kujaribu kuegemea kitu ambacho sio kigumu, kama ufagio. Kwa nini hatupaswi “kutegemea ufahamu wetu”? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuonyesha kwamba tunamwamini Yesu Kristo kwa mioyo yetu yote?

Mithali 15:1–2,18; 16:24,32.Ni kwa jinsi gani maneno yetu yanaathiri roho katika nyumba yetu? Labda wanafamilia wangeweza kujizoeza kutoa “jibu la upole” kwa “maneno yaumizayo” na kujaribu kutumia kile wanachojifunza katika mawasiliano ya wao kwa wao. Wimbo kama “Kindness Begins with Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto,145) unaweza kusaidia kuimarisha kanuni hii.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Where Love Is,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 138–39.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Maneno ya maandiko yanawahusu wote. Vifungu vingine vya maandiko hutaja wanaume tu au wanawake tu (kama vile Mithali 3:13; 31:10). Katika hali nyingi, hata hivyo, kanuni katika vifungu hivi zinatumika kwa kila mtu.

Picha
Yesu akiwaongoza kondoo wawili msituni

“Katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako” (Mithali 3:6). Ananiongoza, na Yongsung Kim, havenlight.com

Chapisha