Agano la Kale 2022
Desemba 12–18. Malaki : “Nimewapenda Ninyi, Asema Bwana”


“Desemba 12–18. Malaki: Nimewapenda Ninyi, Asema Bwana,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Desemba 12–18. Malaki,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Sanamu ya Christus

Desemba 12–18

Malaki

“Nimewapenda Ninyi, Asema Bwana”

Jina Malaki linamaanisha “mjumbe wangu” (Kamusi ya Biblia, “Malaki”). Unapojifunza ujumbe wa Malaki kwa Israeli, unapata ujumbe gani kwa maisha yako? Maneno ya Malaki yanahusiana vipi na siku zetu?

Andika Misukumo Yako

“Nimewapenda ninyi,” Bwana aliwaambia watu Wake kupitia nabii Malaki. Lakini Waisraeli, ambao walikuwa wameteseka kwa vizazi vingi vya mateso na utumwa, walimuuliza Bwana, “Umetupenda kwa njia gani?” (Malaki 1:2). Baada ya yote Israeli ilipitia, huenda wakajiuliza ikiwa historia ya Israeli ya kale kweli ni hadithi ya upendo wa Mungu kwa watu wake wa agano.

Unapotafakari juu ya kile ulichosoma katika Agano la Kale mwaka huu, unapata ushahidi gani juu ya upendo wa Mungu? Ni rahisi kuona mifano mingi ya udhaifu wa kibinadamu na uasi. Walakini katika yote hayo, Mungu hakuacha kamwe kuwafikia kwa upendo. Wakati wana wa Yakobo walipomtendea vibaya ndugu yao Yusufu, Bwana bado aliandaa njia ya kuwaokoa na njaa (ona Mwanzo 45:4–6). Wakati Israeli walilalamika jangwani, Mungu aliwalisha mana (ona Kutoka 16:1–4). Hata Israeli walipomwacha Yeye, na kugeukia miungu ingine, na kutawanyika, Mungu hakuwaacha kabisa lakini aliwaahidi kwamba ikiwa watatubu, atawakusanya na kuwakomboa “kwa rehema nyingi” (ona Isaya 54:7).

Iliyotazamwa kwa njia hii, Agano la Kale ni hadithi yasubira ya Mungu, upendo wa kudumu. Na hadithi hii inaendelea leo. “Jua la Haki [litatokea] na uponyaji katika mabawa yake,” Malaki alitoa unabii (Malaki 4:2). Yesu Kristo alikuja, akileta uponyaji wa mwili na kiroho kwa wote wanaomjia Yeye. Yeye ndiye dhibitisho kuu ya upendo wa Mungu kwa Israeli ya kale na kwetu sisi sote.

Kwa habari zaidi kuhusu kitabu cha Malaki, angalia, (ona “Malaki” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Malaki 1–4.

“Nirudieni nami nitawarudia.”

Katika siku za Malaki, Waisraeli walikuwa tayari wamejenga upya hekalu huko Yerusalemu, lakini kama watu bado walihitaji kujenga tena uhusiano wao na Bwana. Unapojifunza Malaki, tafuta maswali ambayo Bwana aliwauliza Waisraeli au ambayo walimwuliza Yeye. Fikiria kujiuliza maswali kama hayo (mifano kadhaa imependekezwa hapa chini) kukusaidia kutathmini uhusiano wako na Bwana na kujisogeza kwake.

  • Je, nimehisi vipi upendo wa Bwana kwangu? (ona Malaki 1:2).

  • Je! Matoleo yangu kwa Bwana humheshimu Yeye kweli? (ona Malaki 1:6–11).

  • Ni kwa njia zipi ninahitaji “kurudi” kwa Bwana? (Ona Malaki 3:7).

  • Je! Ninamwibia Mungu kwa njia yoyote? (ona Malaki 3:8–11).

  • Je! Mtazamo wangu wakati wa shida unadhihirisha hisia zangu kwa Bwana? (ona Malaki 3:13–15; ona pia 2:17).

Ona pia D. Todd Christofferson “Kadiri ya Wengi Niwapendao, Ninawakemea na Kuwarudi,” Liahona, Mei 2011, 97–100.

Malaki 1:6–14.

Bwana anahitaji “sadaka safi.”

Maneno ya Bwana katika Malaki 1 yanaonyesha kwamba makuhani wa Israeli walikuwa wakitoa wanyama wenye kilema na wagonjwa kama dhabihu hekaluni, ambayo Bwana alikuwa amewakataza (ona Mambo ya Walawi 22:17–25). Je! Dhabihu hizi zinapendekeza nini juu ya hisia za makuhani kwa Bwana? (ona Malaki 1:13). Kwa nini Bwana anatutaka tumpe matoleo yetu bora? Fikiria juu ya dhabihu ambazo Bwana amekuomba kutoa. Je, unaweza kufanya nini ili kumpa Yeye “matoleo bora”? (Malaki 1:11; ona pia 3:3).

Ona pia Moroni 7:5–14.

Malaki 3–4.

Unabii wa Malaki unatimizwa katika siku za mwisho.

Wakati Mwokozi alipotembelea mabara ya Amerika, alinukuu Malaki 3–4 kwa Wanefi (ona 3 Nefi 24–25). Mnamo 1823, malaika Moroni alishiriki sehemu za sura hizo hizi na Joseph Smith (ona Joseph Smith—Historia 1:36–39; ona pia Mafundisho na Maagano 2). Kwa nini unafikiri maneno ya Malaki yanarudiwa mara nyingi katika maandiko? (Ona pia Mafundisho na Maagano 27:9; 110:13–16; 128:17–18). Kwa maoni yako, ni jumbe gani kutoka Malaki 3–4 yanaonekana muhimu sana kwa siku zetu?

Wakati Moroni aliponukuu Malaki 4:5–6 kwa Joseph Smith, alifanya hivyo “kwa tofauti kidogo na jinsi inavyosoma” katika Biblia (Joseph Smith—Historia 1:36). Tofauti ya Moroni inaongeza nini kwa uelewa wetu wa unabii huu? Ili kujifunza zaidi juu ya kuja kwa Eliya na jinsi unabii huu unavyotimizwa leo (ona Mafundisho na Maagano 110:13 na Mzee David A. Bednar, “Mioyo ya Watoto Itageuka” (Liahona, Nov. 2011, 24–27). Kwa nini una shukrani kwamba Eliya amekuja?

Picha
Eliya akiwatokea Joseph Smith na Oliver Cowdery katika Hekalu la Kirtland

Mchoro wa Eliya akiwatokea Joseph Smith na Oliver Cowdery katika Hekalu la Kirtland, na Robert T. Barrett

Malaki 3:8–12.

Kulipa zaka kunafungua madirisha ya mbinguni.

Unaposoma Malaki 3:8–12, fikiria kuhusu uzoefu wako mwenyewe wa kulipa zaka. Kirai “madirisha ya mbinguni yatafunguliwa” (mstari wa 10) kinamaanisha nini kwako?

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Malaki 1:2.Ni kwa jinsi gani familia yako ingejibu swali linalopatikana katika Malaki 1:2—”[Bwana] ametupendaje? Ni baadhi ya ushahidi gani mwingine wa upendo wa Bwana kwetu?

Malaki 3:8–12.Unaposoma Malaki 3:8–12, waalike wana familia kushiriki mawazo yao au mawazo kuhusu zaka. Ni baraka gani za kimwili na kiroho ulizoziona kwa kulipa zaka? (ona David A. Bednar, “Madirisha ya Mbinguni,” Liahona, Nov. 2013, 17–20 ). Wanafamilia wanaweza kufurahia kuchora picha kuwakilisha baraka hizi na kuzitundika hizi picha dirishani.

Malaki 3:13–18.Inamaanisha nini kwetu kuwa wa Bwana na kuwa mmoja wa “vito” Vyake?

Malaki 4:5–6.Baada ya kusoma aya hizi, familia yako inaweza kutambua majibu ya maswali yafuatayo kuhusu unabii wa Malaki: Nani? Nini? Lini? Wapi? Kwa nini? (ona pia Mafundisho na Maagano 2).

Ni kwa jinsi gani tunageuza mioyo yetu kwa baba zetu? Je, ni kwa jinsi gani tunabarikiwa tunapofanya hivyo? Unaweza kutafakari maswali haya wakati unatazama video “The Promised Blessings of Family History” (ChurchofJesusChrist.org). Tunaweza kufanya nini kama familia ili kupata baraka hizi?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Family History—I Am Doing It,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto,94.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Uliza Maswali Unapojifunza. Unapojifunza maandiko, maswali yanaweza kuja akilini mwako. Tafakari maswali haya na tafuta majibu.

Picha
mwanamke akipunga kitambaa cheupe na mababu wengi nyuma yake

Hosanna ya Mourning, na Rose Datoc Dall. Mwanamke anayeitwa Mourning anasimama katika ulimwengu wa roho, akiwa amezungukwa na mababu zake. Anasherehekea ukombozi wake kutoka kwa utumwa wa kiroho.

Chapisha