Agano la Kale 2022
Desemba 5–11. Hagai; Zekaria 1–3; 7–14; “Utakatifu kwa Bwana”


“Desemba 5–11. Hagai; Zekaria 1–3; 7–14; “Utakatifu kwa Bwana,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022 (2021)

“Desemba 5–11. Hagai; Zakaria 1–3; 7–14,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2022

Picha
Hekalu la Laie Hawaii

Hekalu la Laie Hawaii

Desemba 5–11

Hagai; Zekaria 1–3; 7–14

“Utukufu kwa Bwana”

Kusoma maandiko kunaalika ufunuo. Kuwa wazi kwa jumbe ambazo Roho Mtakatifu hufunua kwako unaposoma Hagai na Zekaria.

Andika Misukumo Yako

Baada ya utumwa wa miongo kadhaa, kundi la Waisraeli, labda wakiwemo manabii Hagai na Zekaria, waliruhusiwa kurudi Yerusalemu. Wengine katika kundi hili walikumbuka jinsi Yerusalemu ilivyokuwa kabla ya kuharibiwa. Fikiria hisia zao wakati walipoona kifusi ambacho hapo awali kilikuwa nyumba zao, mahali pao pa ibada, na hekalu lao. Kwa wale ambao walishangaa kama hekalu lingefanana tena na “nyumba ya Bwana katika utukufu wake wa kwanza” (Hagai 2:3), nabii Hagai alisema maneno ya Bwana ya kutia moyo: “Kuweni hodari, enyi watu wote wa nchi, asema Bwana. na fanya kazi: kwa maana mimi niko pamoja nawe, … usiogope.” “Nitaijaza nyumba hii na utukufu, … na mahali hapa nitatoa amani.” (Hagai 2:4–5, 7,9.)

Lakini haikuwa tu hekalu takatifu ambalo lilihitaji kujengwa upya. Kwa njia nyingi, watu wa Mungu walikuwa magofu kiroho. Na kujenga watu watakatifu huchukua zaidi ya kukata mawe na kuyapanga ili kujenga ukuta wa hekalu. Leo, mahekalu yana maandishi “Utakatifu kwa Bwana,” na maneno hayo hayatumiki kwa jengo tu bali kwa njia ya maisha. Kuchora maneno haya juu ya “juga za farasi” na “kila chombo huko Yerusalemu” (Zekaria 14:20–21) ni muhimu tu ikiwa pia imeandikwa kwenye kila moyo. Utakatifu wa kweli unahitaji kwamba maneno na sheria za Bwana “zishike” (Zekaria 1:6) katika sisi, ikiruhusu nguvu Yake ibadilishe asili zetu ili tuwe watakatifu kama Yeye (ona Mambo ya Walawi 19:2).

Kwa ajili ya muhtasari wa vitabu vya Hagai na Zakaria, ona “Hagai” na “Zakaria” katika Kamusi ya Biblia.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Hagai1; 2:1–9

“Fikiria njia zako.”

Kulikuwa na mambo mengi muhimu ya kufanya ili kujenga upya Yerusalemu. Lakini baada ya takribani miaka 15 kupita tangu kurudi kwa Waisraeli, Bwana hakufurahishwa kwamba ujenzi wa hekalu haukupewa kipaumbele cha juu (ona Hagai 1:2–5; ona pia Ezra 2:24). Unaposoma Hagai 1; 2:1–9, fikiria maswali kama haya: Waisraeli walipata matokeo gani kwa sababu walikuwa hawajamaliza hekalu? Ni baraka gani Bwana aliwaahidi ikiwa watamaliza ujenzi wa nyumba Yake? Unaweza kuchukua fursa hii “kuzingatia njia zako”—kufikiria juu ya vipaumbele vyako na jinsi unavyoweza kuvioanisha na vya Bwana.

Ona pia Mafundisho na Maagano 95; Terence M. Vinson, “Wafuasi wa Kweli wa Mwokozi,” Ensign au Liahona, Nov. 2019, 9–11.

Sefania 1–3; 7–8;14

Bwana anaweza kunifanya kuwa mtakatifu.

Dada Carol F. McConkie alifundisha: “Utakatifu ni kufanya uchaguzi ambao utamfanya Roho Mtakatifu kuwa kiongozi wetu. Utakatifu unaweka kando mielekeo yetu ya asili na kuwa ‘mtakatifu kupitia upatanisho wa Kristo Bwana’ [Mosia 3:19]. … Matumaini yetu ya utakatifu yamejikita katika Kristo, kwa rehema Zake na neema Yake” (“Uzuri wa Utukufu,” Ensign au Liahona, Mei 2017, 9–10). Weka mafundisho haya akilini unaposoma maneno ya Bwana, yaliyotolewa kupitia nabii Zekaria, yakihimiza Israeli kuwa takatifu zaidi: Zakaria 1:1–6; 3:1–7; 7:8–10; 8:16–17. Kumbuka vitu ambavyo Bwana aliiomba Israeli ifanye ili aweze kuwafanya kuwa watakatifu. Je, anakusaidiaje kuwa mtakatifu zaidi?

Zekaria 2:10–11; 8:1–8; 14:9–11, 20–21 inaelezea jinsi maisha yatakavyokuwa katika siku zijazo wakati sisi sote tutakaa na Bwana katika hali ya utakatifu. Je! Maelezo haya yanaweza kumaanisha nini kwa wale waliokuwa wakijenga upya Yerusalemu katika wakati wa Zekaria? Yana maana gani kwako?

Picha
Kuingia kwa shangwe kwa Yesu katika Yerusalemu

“Tazama, Mfalme wako anakuja kwako; yeye ni mwenye haki, na ana wokovu; mnyenyekevu, na amepanda punda” (Zekaria 9:9). Kuingia kwa Shangwe, na Harry Anderson

Zekaria 9:9–11; 11:12–13; 12:10; 13:6–7; 14:1–9

Yesu Kristo ndiye Masiya aliyeahidiwa.

Machapisho kadhaa ya Zekaria yanaelekeza kwa huduma ya kidunia ya Yesu Kristo na pia Ujio wa Pili Wake. Linganisha unabii ufuatao kutoka kwa Zekaria na vifungu vinavyohusiana kutoka kwenye vitabu vingine vya maandiko:

Ulijifunza nini juu ya Mwokozi wakati unasoma vifungu hivi? Kwa nini ni muhimu kwako kujua kuhusu vifungu hivi?

Ona pia Mwongozo wa Maandiko, “Masiya,” (scriptures.ChurchofJesusChrist.org).

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Hagai 1:2–7.Mistari hii inaweza kuiongoza familia yako “kuzingatia njia zako.” Labda wanafamilia wangeigiza virai katika mstari wa 6. Je! Mstari huu unafundisha nini juu ya kuthamini vitu vya ulimwengu kuliko vitu vya Mungu? Mnaweza kushauriana pamoja juu ya vipaumbele vya familia yako. Kuimba wimbo kama “I’m Trying to Be Like Jesus” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 78–79) inaweza kusaidia familia yako kutathmini kile mnachofanya vizuri na maeneo ambayo mnaweza kuboresha.

Hagai 2:1–9.Ili kutambulisha mistari hii, unaweza kushiriki hadithi ya Hekalu la Provo City Center, ambalo lilijengwa upya kutoka kwa tabanakulo linalopendwa ambalo lilikuwa limeteketea (ona video “Provo City Center Temple Completed,” ChurchofJesusChrist.org). Wakati familia yako inasoma Hagai 2:1–9, unaweza kuuliza wanafamilia kufikiria juu ya kitu maishani mwetu ambacho kinaweza kuwa kama kazi ya kujenga tena hekalu ambalo lilikuwa limeharibiwa. Je! Bwana hutujengaje baada ya msiba au shida?

Zekaria 3:1–7.Unaposoma mistari hii, unaweza kuonyesha familia yako nguo chafu. Je! Yoshua angejisikiaje aliposimama mbele ya malaika amevaa nguo chafu? Ni kwa jinsi gani dhambi ni kama nguo chafu? Je! Zekaria 3:1–7 inatufundisha nini kuhusu msamaha? Mnaweza basi kusafisha nguo pamoja na kuzungumza juu ya nguvu ya utakaso ya Upatanisho wa Mwokozi.

Zekaria 8:1–8.Ni nini kinatuvutia kuhusu maono ya Zekaria kuhusu siku zijazo za Yerusalemu? Je! Tunapata nini hapo ambacho tungependa kukiona katika jamii yetu? Ni kwa jinsi gani tunaweza kumwalika Mwokozi “akae katikati [yetu]”? (ona Gary E. Stevenson, “Nyumba Takatifu, Mahekalu Takatifu,” Ensign au Liahona, Mei 2009, 101–3).

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “I’m Trying to Be like Jesus,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 78–79

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Chukua fursa za kujitathmini. Unapojifunza maandiko, mara nyingi utahamasika kutafakari kujitolea kwako kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Tenda kulingana na misukumo unayoipata.

Picha
Ratiba ya nyakati inayoonyesha jinsi Provo Tabernacle huko Provo, Utah, USA, lilivyoharibiwa na moto na kujengwa upya kama Hekalu la Provo City Center

Chapisha