Njoo, Unifuate
Machi 2–8. 2 Nefi 31–33: “Hii ndiyo Njia”


“Machi 2–8. 2 Nefi 31–33: ‘Hii ndiyo Njia,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Machi 2–8. 2 Nefi 31–33,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2020

Picha
Yesu akiwafundisha wafuasi Wake

Kristo Akiwafundisha Wafuasi Wake, na Justin Kunz

Machi 2–8

2 Nefi 31–33

“Hii ndiyo njia;

Anza maandalizi yako kwa kusoma 2 Nefi 31–33. Tafuta mwongozo wa Roho kuhusu nini cha kuwafundisha watoto. Muhtasari huu unaweza kukupatia baadhi ya mawazo.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kwa sababu Nefi alifundisha kuhusu ubatizo wa Kristo, waombe watoto kushiriki jambo walilojifunza kuhusu ubatizo. Wanaweza pia kushiriki mawazo na hisia kuhusu ubatizo wao wenyewe au ubatizo wa rafiki zao au wanafamilia.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

2 Nefi 31

Yesu Kristo alinifundisha jinsi ya kurudi kwa Baba wa Mbinguni.

Nefi alifundisha kwamba kufuata mfano na mafundisho ya Mwokozi ni njia pekee ya “kuokolewa katika ufalme wa Mungu” (2 Nefi 31:21).

Shughuli za Yakini

  • Onyesha picha kwenye muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapofanya ufupisho wa tukio la ubatizo wa Yesu (ona 2 Nefi 31:4–13). Elezea kwamba ubatizo ni hatua moja kwenye njia ya kurudi kuishi na Baba wa Mbinguni. Mwalike mtu ambaye amebatizwa karibuni kuwaambia watoto jinsi anavyohisi kuhusu ubatizo.

  • Elezea kwamba Yesu Kristo alitufundisha sisi kile tunachohitaji kufanya ili kurudi kwake baada ya kufa. Chora njia ubaoni, na weka picha ya Kristo mwisho wa njia. Wape watoto picha ambazo huwakilisha vipengele vya injili ya Kristo (imani katika Kristo, toba, ubatizo, kipawa cha Roho Mtakatifu, na kuvumilia hadi mwisho). Wasaidie kuweka picha hizo kwenye njia.

  • Wasaidie watoto kujifunza makala ya imani ya nne. Imbeni kwa pamoja wimbo kuhusu moja ya kanuni ya kwanza ya injili, kama vile “Faith,” “When I Am Baptized,” au “Choose the Right Way” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 96–97, 103, 160–61).

2 Nefi 32:3.

Ninaweza kusherehekea maneno ya Kristo.

Ni kwa jinsi gani uzoefu wako kwenye “[ku]sherehekea maneno ya Kristo” (2 Nefi 32:3) unawasaidia watoto kuelewa kifungu hiki cha maneno?

Shughuli za Yakini

  • Waombe watoto kutaja baadhi ya vyakula wanavyovipenda sana, na waalike kuigiza jinsi wanavyoweza kuvisherehekea. Soma 2 Nefi 32:3, na waombe watoto wasikilize kile Nefi alisema tunapaswa kukisherehekea. Je, inamaanisha nini kusherehekea maandiko? Elezea kwamba maandiko ni sehemu moja ambapo tunaweza kupata maneno ya Kristo.

  • Andika maneno Mungu na Bwana ubaoni. Waalike watoto kufungua ukurasa wa andiko na kutafuta maneno haya. Wape msaada kama itahitajika. Shuhudia kwamba tunaposoma maandiko, tunaweza kujifunza kuhusu Mungu.

2 Nefi 32:8–9

Baba wa Mbinguni ananitaka kusali kila wakati.

Mistari hii inaweza kuwapa msukumo watoto kufanya sala kuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku.

Shughuli za Yakini

  • Waulize watoto ni wakati gani wanasali. Je, wanasali asubuhi? Usiku? Kabla ya chakula? Wasaidie watoto kufikiria matendo ya kuonyesha wakati gani tunaweza kusali, kama vile tunapoamka, tunapokwenda kulala, na kula—au wakati mwingine wowote. Wasomee mstari wa kwanza au miwili kutoka 2 Nefi 32:9, na sisitiza kifungu cha maneno “sali kila wakati.”

  • Waulize watoto jinsi gani wanasali. Ni nini wanafanya kwa vichwa vyao, mikono, na kadhalika?? Ni mambo gani wanasema? Waombe kufikiria kwamba wewe hujui jinsi ya kusali, na acha wakufundishe. Je, ni kwa nini Baba wa Mbinguni anataka tusali?

Picha
msichana mdogo akisali

Tunaweza kuzungumza na Mungu kupitia sala.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

2 Nefi 31

Yesu Kristo alinifundisha jinsi ya kurudi kwa Baba wa Mbinguni.

Tunaweza kurudi kwa Mungu baada ya maisha haya kwa kufuata injili Yesu Kristo aliyofundisha: imani katika Kristo, toba, ubatizo, kipawa cha Roho Mtakatifu, na kuvumilia hadi mwisho.

Shughuli za Yakini

  • Onyesha picha kwenye muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia, na waombe watoto kushiriki kile wanachojua kuhusu ubatizo wa Yesu (ona Mathayo 3:13–17). Weka maneno yafuatayo katika mpangilio usio mzuri ubaoni: Yesu alimshuhudia Baba kwamba atakuwa mwaminifu Kwake. Waalike watoto kusoma 2 Nefi 31:7 kama darasa na weka maneno katika mpangilio mzuri.

  • Waulize watoto kile ambacho wangeweza kumwambia mtu anayejiandaa kubatizwa, na wasaidie kuweka pamoja ushauri wao kwenye kadi ndogo wanazoweza kumpa mtu. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuendelea kufuata mfano wa Yesu baada ya kubatizwa?

  • Elezea kwamba injili ya Kristo inajumuisha mambo Yesu Kristo aliyofundisha ambayo tunapaswa kufanya ili kurudi kwa Baba wa Mbinguni. Andika kwenye vipande tofauti vya karatasi imani katika Kristo, toba, ubatizo, kipawa cha Roho Mtakatifu, na kuvumilia hadi mwisho, na vitawanye ndani ya chumba. Wasomee watoto 2 Nefi 31:11–19, na waalike watoto kufanya zamu kuruka kutoka karatasi moja hadi nyingine pale wanaposikia kanuni hizi zikitajwa. Wasaidie kufikiria uzoefu walioupata kwa kila kanuni.

2 Nefi 32:3–5

Ninaweza kusherehekea maneno ya Kristo.

Kwa nini watoto wanahitaji kuelewa umuhimu wa kusherehekea maneno ya Kristo?

Shughuli za Yakini

  • Waombe watoto wafikirie sherehe. Ni vyakula gani wangetaka kwenye sherehe? Ni nini wangekula kwanza? Kisha waalike kufikiria nini kusherehekea maandiko kunaweza kumaanisha pale unaposoma 2 Nefi 32:3. Ni kwa nini Nefi alitumia neno sherehe kutufundisha jinsi gani tunapaswa kusoma neno la Mungu? Ni kwa nini hakusema tu soma? Je, inamaanisha nini kusherehekea maandiko? Shiriki na watoto baraka ulizopokea pale uliposherehekea maandiko.

  • Kamilisha ukurasa wa shughuli pamoja na watoto, na waalike kuweka lengo kufanya angalau jambo moja kusherehekea maandiko wiki hii.

2 Nefi 32:8–9

Baba wa Mbinguni ananitaka kusali kila wakati.

Mjaribu hutushawishi tusisali. Fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia watoto kushinda jaribu hili na “kusali kila wakati” (2 Nefi 32:9).

Shughuli za Yakini

  • Chagua kifungu cha maneno kuhusu sala kutoka 2 Nefi 32:8–9, kiandike ubaoni, na ziba kila neno kwa kipande cha karatasi. Waalike watoto kufanya zamu kuondoa karatasi moja baada ya nyingine mpaka watakapobashiri kipi ni kifungu cha maneno.

  • Someni 2 Nefi 32:8–9 kwa pamoja, na waombe watoto kushiriki kile wanachojifunza kuhusu sala kutoka kwenye vifungu hivi. Inamaanisha nini “kusali kila wakati”? (mstari wa 9). Tunawezaje kufanya hili?

  • Nini kinaweza kumfanya mtu asitake kusali? Shiriki uzoefu wakati uliposali japokuwa hukujisikia kufanya hivyo. Je! Ulihisi vipi baada ya hapo? Mwalike mtoto kusoma nusu ya pili ya 2 Nefi 32:8, na wape watoto muda wa kutafakari. Kwa nini Shetani hataki tusali? Ni kwa jinsi gani tunaweza kujikumbusha kusali hata pale tunapokuwa hatujisikii kufanya hivyo?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wahimize watoto kumtafuta mtu—rafiki, ndugu, au mwanafamilia mwingine—wanayeweza kumfundisha jinsi ya kusali.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Watoto ni wachangamfu. Waalike watoto kuigiza hadithi za maandiko na nyimbo. Tumia asili yao ya uchangamfu kuzidisha kujifunza. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.

Chapisha