Mafundisho na Maagano 2021
Julai 12–18. Mafundisho na Maagano 77–80: “Nitawaongoza Muda Wote”


“Julai 12–18. Mafundisho na Maagano 77–80: “Nitawaongoza Muda Wote,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Julai 12–18. Mafundisho na Maagano 77–80,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2021

Picha
Kondoo wakimfuata Yesu

Kwenda Nyumbani, na Yongsung Kim

Julai 12–18

Mafundisho na Maagano 77–80

“Nitawaongoza Muda Wote”

Unapojifunza Mafundisho na Maagano 77–80, tafuta mafungu ya maneno au mistari ambayo inaweza kuwasaidia watoto kuelewa vyema kanuni za injili. Uwe huru kushiriki mistari uliyoipata, hata kama sio sehemu muhimu katika shughuli hapo chini.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto kushiriki vitu walivyo na shukrani navyo. Ni nini wao na familia zao wanafanya kumwonyesha Baba wa Mbinguni kwamba wana shukrani kwa ajili ya baraka Zake?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mafundisho na Maagano 77:2

Mungu aliumba kila kiumbe duniani.

Kujifunza kuhusu vitu Mungu alivyoumba kunaweza kusaidia watoto kuhisi upendo Wake kwa ajili yao.

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto picha za wanyama, pamoja na wadudu na ndege. Unaposoma maneno “wanyama,” “vitu vitambaavyo,” na ndege wa angani” kutoka Mafundisho na Maagano 77:2, watake watoto kuonyesha picha inayohusiana nayo. Shuhudia kwamba Mungu aliumba vitu hivi vyote kwa sababu Yeye anatupenda na anatutaka sisi kuwa wenye furaha (ona pia Mafundisho na Maagano 59:16–20).

  • Imba pamoja na watoto wimbo kuhusu uumbaji wa Mungu, kama vile “My Heavenly Father Loves Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 228–29). Waulize watoto jinsi vitu wanavyoimba kuvihusu huwasaidia kuhisi upendo wa Mungu.

    Picha
    kipepeo juu ya ua

    Mungu aliumba dunia na kila kitu juu yake.

Mafundisho na Maagano 78:6

Ninaweza kushiriki vile nilivyo navyo pamoja na wengine.

Baba wa Mbinguni anatutaka sisi kushiriki baraka zetu kwa uhuru na kila moja wetu ili kwamba tuweze kuwa “sawa katika vitu vya kidunia” na katika “vitu vya mbinguni” (mstari wa 6).

Shughuli Yamkini

  • Kufundisha nini inamaanisha kuwa “sawa katika vitu vya kidunia” (mstari wa 6), wape watoto picha za watu wenye mahitaji (kama vile watu wenye njaa, walioumia, au wenye baridi). Kisha wape watoto wengine vitu ambavyo vitasaidia (kama vile chakula, bandeji, au blanketi). Waalike watoto hawa kushiriki kile walichonacho kuwasaidia watu katika picha. Acha watoto wengine wapate zamu kushiriki. Wasaidie watoto kuelewa kwamba Baba wa Mbinguni anawataka watoto Wake wote kuwa na kile wanachohitaji, na kufanya hivi mara kwa mara anatutaka sisi kushiriki kile tulichonacho na wengine.

  • Soma kwa watoto sentensi zilizo chini ya picha mbili za kwanza za “Sura ya 28: Nabii Joseph Smith Anakwenda Missouri Tena” (Hadithi za Mafundisho na Maagano,108). Waombe watoto kujifanya wanamsaidia mtu fulani kujenga nyumba, kushiriki chakula, au kuhudumia katika njia nyingine. Tunajisikiaje tunaposaidia na kushirikiana? Wasaidie watoto kufikiria vitu ambavyo Yesu Kristo anashiriki pamoja nasi.

Mafundisho na Maagano 78:18

Yesu Kristo Ataniongoza muda wote.

Kama tupo tayari kumwacha Bwana “kutuongoza [sisi] muda wote,”tunaweza “kuwa na furaha kuu,” hata kama kuna vitu “hatuwezi kuvumilia … sasa” (mstari wa 18).

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto washiriki nyakati walipokuwa viongozi, kama vile kuwa mbele ya mstari au kuongoza muziki. Kiongozi anafanya nini? Onyesha picha ya Mwokozi unaposoma kirai kinachofuata kutoka Mafundisho na Maagano 78:18: “Muwe wenye furaha, kwani nitawaongoza muda wote.” Tumia ukurasa wa shughuli ya wiki hii kuwasaidia watoto kufikiria njia tunazoweza kumfuata Mwokozi.

  • Waalike watoto kumfuata Yesu, na waongoze kuzunguka chumba unaposhikilia picha Yake. Unapofanya hivyo, imbeni wimbo pamoja kuhusu kumfuata Yesu Kristo, kama vile “I’m Trying to Be like Jesus” au “(Choose the Right Way” (Kitabu cha nyimbo za Watoto, 78–79, 160). Waache watoto wafanye zamu kushikilia picha na kuwaongoza watoto wengine.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mafundisho na Maagano 77

Ninaweza kupokea majibu kwa maswali yangu kuhusu maandiko.

Kufundisha watoto kuhusu jinsi Joseph Smith alivyotafuta majibu kwa maswali yake inaweza kuwasaidia kujua kwamba Baba wa mbinguni atayajibu wakati wanatafuta mwongozo Wake. Fikiria kushiriki uzoefu wakati ulipopokea majibu kutoka Kwake.

Shughuli Yamkini

  • Soma kwa watoto maneno chini ya picha tatu za kwanza za“Sura ya 27: Nabii Anaendelea na Kazi Yake Licha ya Mateso” (Hadithi za Mafundisho na Maagano,104). Waulize watoto ikiwa wao, kama Joseph, wamewahi kuhisi kwamba hawakuelewa kitu fulani katika maandiko. Waache washiriki uzoefu wao. Joseph alifanya nini kupata majibu? Waeleze watoto kuhusu wakati Baba wa Mbinguni alipokusaidia kuelewa kitu fulani katika maandiko.

  • Watoto unaowafundisha wanaweza kufurahia kusoma baadhi ya mistari katika kitabu cha Ufunuo ambacho Joseph Smith alikuwa na maswali kukihusu. Kisha wangeweza kutazama katika Mafundisho na Maagano 77 kwa ajili ya kile Bwana alichomtaka kuelewa. Chagua mistari michache unayohisi itakuwa yenye maana.

Mafundisho na Maagano 78:3–7

Ninaweza kusaidia “kuendeleza sababu” ya Yesu Kristo.

Katika sehemu ya 78, Bwana alitoa maelekezo muhimu kwa baadhi ya viongozi wa Kanisa ambayo yangewasaidia “kuendeleza sababu” ya Bwana (mstari wa 4). Wasaidie watoto kufikiria kile majukumu yao yanachoweza kuwa katika kuendeleza sababu ya Bwana.

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto wasome Mafundisho na Maagano 78:4. Nini “sababu” ambayo sisi “tuliunga mkono” (tuliyokubali au tuliyochagua kuunga mkono) tulipobatizwa? Watie moyo kutafuta katika kifungu cha maandiko kama haya kwa ajili ya uwezekano wa majibu: Mosia 18:8–10; Mafundisho na Maagano 20:37; Musa 1:39.

  • Eleza kwa watoto kwamba Newel K. Whitney alimiliki duka na kwamba Bwana alimwomba yeye pamoja na wanaume wengine kutumia baadhi ya pesa zao kusaidia malipo kwa ajili ya kazi ya Bwana (ona Mafundisho na Maagano 63:42–43). Waalike watoto wasome Mafundisho na Maagano 78:3–7 na kutafuta sababu ya kwa nini wanaume hawa walitakiwa kufanya hivyo. Jinsi gani tungeweza kujihisi kama tungetakiwa kushiriki kama Newel alivyofanya? Wasaidie watoto kufikiria juu ya njia ambazo watu wanachangia kwenye kazi ya Bwana katika siku hizi, kama vile kulipa zaka na matoleo ya mfungo, kuhudumia katika miito, na kadhalika.

Mafundisho na Maagano 78:19

Ninapaswa kupokea “vitu vyote kwa shukrani.”

Bwana mara nyingi anatubariki zaidi kama tukiwa na shukrani kwa kile ambacho tayari amekwisha tupatia. Jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha wawe wenye shukrani kwa ajili ya baraka zao?

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto wasome Mafundisho na Maagano 78:19 na kutafuta kile Bwana Alichoahidi kwa wale walio na shukrani. Wasaidie watoto waelewe nini maana ya “mara mia moja” pengine kwa kuwaonyesha kitu kidogo na kisha 100 ya kitu kilekile.

  • Imbeni wimbo kuhusu shukrani, kama vile “I am Glad for Many Things”” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto151), au angalieni video “Think to Thank” (ChurchofJesusChrist.org). Wape watoto muda kutengeneza orodha ya vitu walivyo na shukrani navyo. Watie moyo kuorodhesha vitu vingi inavyowezekana katika muda unaowapa.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Fikiria kuwasiliana na wazazi wa watoto unaowafundisha na kupendekeza swali ambalo wangeweza kuwauliza watoto wao kuhusu kitu fulani walichojifunza katika darasa.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Shuhudia juu ya baraka zilizoahidiwa. Wakati unapowataka watoto wa msingi kuishi kanuni fulani, shiriki ahadi ambazo Mungu amezifanya kupitia manabii kwa wale wanaoishi kanuni hiyo. Mfano mmoja wa ahadi ambao ungeweza kushiriki unapatikana katika Mafundisho na Maagano 78:19. (Ona pia Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,35.)

Chapisha