Scripture Stories
Sura ya 28: Nabii Joseph Anakwenda Tena Missouri: Machi–Mei 1832


Sura ya 28

Nabii Joseph Anakwenda Tena Missouri

Machi–Mei 1832

Picha
gari la kukokotwa na maksai
Picha
Joseph anasikia sauti ya Bwana

Joseph Smith alipokea ufunuo ambapo Yesu alisema Watakatifu walikuwa kama watoto Wake wadogo. Walikuwa bado wanajifunza. Yesu alisema wanapaswa kuwa na furaha na wenye shukrani. Yeye angekuwa kiongozi wao.

Picha
Watakatifu wakijenga nyumba

Yesu alisema Alitaka Watakatifu kuwatunza wale ambao walikuwa masikini. Aliwataka kushirikiana na kusaidiana.

Picha
Joseph akiwasalimu Watakatifu wa Missouri

Mara tu baada ya Joseph Smith kupokea ufunuo huu, yeye na baadhi ya marafiki zake walienda tena Missouri. Watakatifu wa Missouri walikuwa na furaha kumwona.

Picha
Joseph anakutana na Watakatifu

Joseph aliwataka Watakatifu kuja kwenye mkutano ili aweze kuwaambia kuhusu ufunuo.

Picha
Yesu akizungumza na Joseph

Katika mkutano Bwana alimpatia Joseph ufunuo mwingine. Yesu alikuwa na furaha kwamba Watakatifu walikuwa wamesameheana. Kwa sababu walikuwa wamefanya hili, Alisema Yeye angewasamehe.

Picha
Watakatifu wakivuna kwenye mashamba

Katika ufunuo huu Yesu pia aliwapa Watakatifu amri mpya. Alisema kwamba Alikuwa amewapa nchi ya Sayuni, na ni lazima wagawane ardhi hiyo kila mmoja. Kila mtu alipaswa kuwa na kile alichohitaji. Bwana pia aliwataka Watakatifu kuboresha vipaji vyao na kuvitumia kwa manufaa ya Kanisa.

Picha
Joseph akiwatembelea Watakatifu

Baada ya mkutano, Joseph alitembelea Watakatifu katika miji mingi. Ilikuwa ni wakati wa furaha kwake. Aliwapenda Watakatifu.

Picha
Joseph anapokea ufunuo

Katika ufunuo mwingine ambao Joseph alipokea wakati alipokuwa Missouri, Bwana alisema kwamba waume wanapaswa kuwatunza wake zao. Wazazi wanapaswa kuwatunza watoto wao.

Picha
Watakatifu wakiwatembelea wajane

Bwana pia alisema Watakatifu wanapaswa kuwatunza wanawake wasiokuwa na waume. Watakatifu lazima pia wawatunze watoto ambao hawana baba au mama.

Picha
Watakatifu kwenye ghala la Askofu

Yesu alisema Watakatifu wanapaswa kutoa chakula na vitu vingine kwa askofu ili kuweka katika ghala. Alisema Askofu anapaswa kutumia kile kilicho katika ghala ili kuwasaidia wale ambao ni masikini.

Picha
Joseph na Askofu Whitney wakisafiri

Baada ya Joseph Smith kumaliza kazi yake Missouri, yeye na Askofu Whitney walianza kurudi Kirtland. Walisafiri kwenye gari la kukokotwa na farasi.

Picha
farasi wakiwa na hofu

Siku moja kitu kiliwatisha farasi na kuwafanya wakimbie kwa kasi.

Picha
Askofu Whitney akiwa amelala chini ardhini

Joseph aliruka kutoka kwenye gari la kukokotwa na farasi, lakini hakuumia. Askofu Whitney aliruka kutoka kwenye gari la kukokotwa na farasi na kuvunja mguu wake.

Picha
Askofu Whitney akiwa amelala kitandani

Joseph Smith na Askofu Whitney walikaa katika nyumba ya wageni. Askofu Whitney alipumzika kwa wiki nne. Joseph alikaa pamoja naye wakati mguu wake ukipona.

Picha
Joseph akiwa amelala kitandani

Wakati walipokuwa katika nyumba ya wageni, mtu aliweka sumu kwenye chakula cha Joseph. Akawa mgonjwa sana.

Picha
Askofu Whitney akimpa Joseph baraka

Joseph akamwomba Askofu Whitney kumpa baraka. Askofu Whitney alitumia nguvu ya ukuhani kumbariki Joseph, naye akapona.

Picha
Askofu Whitney na Joseph wakiomba

Joseph alimshukuru Mungu kwa kumponya. Wakati Joseph na Askofu Whitney walipokuwa na nafuu ya kutosha kusafiri, walikwenda nyumbani kwa familia zao.

Chapisha