Scripture Stories
Sura ya 35: Watakatifu Wanaondoka Jackson County, Missouri: Septemba–Desemba 1833


Sura ya 35

Watakatifu Wanaondoka Jackson County, Missouri

Septemba–Desemba 1833

Picha
nyumba ya majira ya baridi
Picha
Watakatifu wakisalimiana na gavana wa Missouri

Kwa sababu genge la watu wenye fujo katika Jackson County lilikuwa likisababisha matatizo mengi, Watakatifu walijaribu kupata msaada kutoka kwa gavana wa Missouri. William Phelps na Orson Hyde walikwenda kuonana na gavana. Walimwambia kuhusu genge hilo na jinsi nyumba zao zilivyokuwa zimeharibiwa.

Picha
Watakatifu wakiondoka kutoka kwa gavana

Gavana asingeweza kuwasaidia. Aliwaambia wawaombe majaji msaada. Lakini majaji walikuwa marafiki wa lile genge, na hawangeweza kusaida pia.

Picha
genge la watu wenye fujo likivamia duka

Genge la watu wenye fujo liliwashambulia Watakatifu kwa siku sita. Walivunja makazi yao, kuwadhuru wanaume, na kuvunja duka na kurusha kila kitu sakafuni.

Picha
Watakatifu wakifukuzwa majumbani

Genge la watu wenye fujo liliwafanya Watakatifu kukimbia makazi yao. Ilikuwa ni majira ya baridi, na watu wengi walikufa kwa sababu hawakuwa na makazi katika hali ya baridi, na mvua. Watakatifu walienda sehemu nyingine za Missouri ili kulikimbia genge hilo la watu wenye fujo.

Picha
Watakatifu wamekusanyika kuzunguka moto

Watakatifu walikuwa na huzuni. Nyumba zao, mashamba, na maduka yaliharibiwa. Wanyama wao walikuwa wameibiwa. Gavana na majaji hawakuweza kuwasaidia.

Picha
Watakatifu wakitazama mbele kwa imani

Lakini Watakatifu bado walikuwa na imani katika Mungu. Walijua Kanisa la Yesu Kristo lilikuwa la kweli, na walijua kwamba Joseph Smith alikuwa nabii wa Mungu.

Picha
Joseph akiomba

Wakati Watakatifu walipokuwa wakiteswa Missouri, Joseph Smith alikuwa Kirtland, Ohio. Yesu alimpa Joseph ufunuo ulioeleza ni kwa nini Watakatifu katika Missouri walikuwa na matatizo.

Picha
Watakatifu wakizozana wenyewe kwa wenyewe

Yesu alisema baadhi ya Watakatifu hawakuwa wametii amri. Hawakuwa na umoja, kama watu wa Sayuni wanavyopaswa kuwa. Baadhi yao walibishana na kuneneana mambo mabaya. Wengine walikuwa na wivu, na wengine hawakushirikiana na wengine vitu vyao.

Picha
Yesu akija duniani

Licha ya matatizo haya, Yesu alisema aliwapenda Watakatifu na Hataweza kuwasahau. Alisema wanapaswa kufarijika kwa sababu wenye moyo safi siku moja watarudi na kujenga Sayuni. Yesu aliwaambia Watakatifu kujiandaa kwa ajili ya wakati Yeye atakapokuja tena. Wakati Atakapokuja, watu watapendana na kuwa na amani. Wale ambao waliteswa kwa kumfuata Yesu watabarikiwa. Shetani hatakuwa na uwezo wa kuwadanganya watu. Hakutakuwa na kifo kama inavyojulikana leo. Kila mtu atakuwa na furaha.

Chapisha