Watu wa Kuwajua
- Ibrahimu
-
Ibrahimu alikuwa nabii aliyeishi hapo kale. Hadithi ya Ibrahimu ipo katika Agano la Kale na Lulu ya Thamani Kuu.
- Bennett, John C.
-
John C. Bennett alikuwa Meya wa Nauvoo. Yeye alimgeuka Joseph Smith.
- Kapteni Allen
-
Kapteni Allen alikuwa kapteni katika Jeshi la Marekani. Aliwaomba wanaume wa Kanisa kuwa katika Kikosi cha Mormoni.
- Copley, Leman
-
Leman Copley alikuwa muumini wa Kanisa katika Kirtland, Ohio, ambaye hakuwapa ardhi yake waumini wengine.
- Cowdery, Oliver
-
Oliver Cowdery alimsaidia Joseph Smith kutafsiri mabamba ya dhahabu. Alifanya kazi nyingi ili kulisaidia Kanisa.
- Elia
-
Elia alirejesha uwezo maalum wa ukuhani kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery katika Hekalu ya Kirtland.
- Eliya
-
Eliya alikuwa nabii aliyeishi hapo kale. Alirejesha uwezo maalum wa ukuhani kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery katika Hekalu la Kirtland .
- Henoko
-
Henoko alikuwa nabii aliyeishi hapo kale. Yeye alijenga mji wa Sayuni. Hadithi ya Henoko ipo katika Lulu ya Thamani Kuu.
- Gavana Boggs
-
Gavana Boggs alikuwa gavana wa Missouri. Yeye hakuweza kuwasaidia Watakatifu na alitoa amri ya kuwaondoa kutoka jimboni au kuwaua.
- Harris, Martin
-
Martin Harris alimsaidia Joseph Smith kutafsiri mabamba ya dhahabu. Alipoteza kurasa kadhaa za Kitabu cha Mormoni.
- Hyde, Orson
-
Orson Hyde alikuwa Mtume. Aliweka wakfu Nchi Takatifu kwa ajili ya watoto wa Ibrahimu wapate mahali pa kuishi.
- Wahindi
-
Wahindi waliishi katika maeneo yote ya Marekani. Wakati mwingine Wahindi wanaitwa Walamani.
- Yakobo
-
Yakobo alikuwa mmoja wa Mitume Kumi na Wawili wa Yesu. Petro, Yakobo na Yohana, walirejesha Ukuhani wa Melkizedeki kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery.
- Yohana
-
Yohana alikuwa mmoja wa Mitume Kumi na wawili wa Yesu. Petro, Yakobo na Yohana, walirejesha Ukuhani wa Melkizedeki kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery.
- Yohana Mbatizaji
-
Yohana Mbatizaji aliishi wakati Yesu alipoishi duniani. Yohana Mbatizaji alitoa Ukuhani wa Haruni kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery.
- Kimball, Heber C.
-
Heber C. Kimball alikuwa Mtume. Alikwenda misheni huko Uingereza.
- Kimball, Sarah
-
Sarah Kimball alikuwa mshiriki wa Muungano wa kwanza wa Usaidizi wa Akina Mama.
- Kimball, Spencer W.
-
Spencer W. Kimball alikuwa Rais wa 12 wa Kanisa.
- Knight, Newel
-
Newel Knight alikuwa mgonjwa wakati Shetani alipojaribu kumzuia kuomba. Joseph Smith alimponya Newel Knight.
- Walamani
-
Walamani ni uzao wa wana wa Lehi, ambao ni Lamani na Lemueli.
- Melkizedeki
-
Melkizedeki alikuwa nabii aliyeishi hapo kale.
- Wamormoni
-
Wakati mwingine waumini wa Kanisa wanaitwa Wamormoni kwa sababu wanaamini katika Kitabu cha Mormoni.
- Moroni
-
Moroni alikuwa Nabii Mnefi aliyeishi Marekani hapo kale. Alizika mabamba ya dhahabu katika Kilima Kumora.
- Musa
-
Musa alikuwa nabii aliyeishi hapo kale. Aliwaongoza Waisraeli kutoka Misri. Alirejesha uwezo maalum wa ukuhani kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery katika Hekalu la Kirtland.
- Bw. Chandler
-
Bw. Chandler aliuza baadhi ya magombo ya karatasi za kale kwa Watakatifu huko Kirtland. Maandiko ya Ibrahimu yalikuwa kwenye magombo ya karatasi.
- Bw. Hale
-
Bw. Hale alikuwa baba yake Emma Smith.
- Nuhu
-
Nuhu alikuwa nabii aliyeishi miaka mingi iliyopita.
- Page, Hiram
-
Hiram Page alisema alikuwa na jiwe lililompa mafunuo kwa ajili ya Kanisa.
- Partridge, Edward
-
Edward Partridge alikuwa askofu wa kwanza wa Kanisa.
- Petro
-
Petro alikuwa mmoja wa Mitume Kumi na Wawili wa Yesu. Petro, Yakobo na Yohana, walirejesha Ukuhani wa Melkizedeki kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery.
- Phelps, William W.
-
William W. Phelps alisaidia kuanzisha shule katika Jackson County, Missouri.
- Waanzilishi
-
Waanzilishi walikuwa Watakatifu waliovuka uwanda kwenda katika Milima ya Miamba.
- Pratt, Parley P.
-
Parley P. Pratt alienda misheni kuwafundisha Walamani.
- Richards, Willard
-
Willard Richards alikuwa rafiki wa Joseph Smith. Alikuwa pamoja na Joseph katika Jela ya Carthage.
- Rigdon, Sidney
-
Sidney Rigdon alikuwa mmoja wa washauri wa Joseph.
- Smith, Alvin
-
Alvin Smith alikuwa mmoja wa kaka wakubwa wa Joseph Smith. Yeye alifariki. Joseph aliona ono la Alvin akiwa katika ufalme wa selestia wa mbinguni.
- Smith, Emma
-
Emma Smith alikuwa mke wa Joseph Smith. Alikuwa kiongozi wa kwanza wa Muungano wa Usaidizi wa Akina Mama. Alitengeneza kitabu cha nyimbo za dini kwa ajili ya Kanisa.
- Smith, Hyrum
-
Hyrum Smith alikuwa mmoja wa kaka mkubwa wa Joseph Smith. Hyrum aliuawa katika Jela ya Carthage pamoja na Joseph.
- Smith, Joseph
-
Joseph Smith alikuwa nabii wa kwanza na Rais wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Yesu alimpa Joseph Smith mafunuo ambayo yanapatikana katika Mafundisho na Maagano. Joseph aliuawa katika Jela ya Carthage.
- Smith, Joseph Sr.
-
Joseph Smith Mkubwa alikuwa baba yake Joseph Smith.
- Smith, Lucy
-
Lucy Smith alikuwa mama yake Joseph Smith.
- Smith, Samuel
-
Samuel Smith alikuwa kaka mdogo wa Joseph Smith. Alikuwa mmisionari wa kwanza wa Kanisa.
- Snow, Eliza R.
-
Eliza R. Snow alikuwa mshiriki wa Muungano wa wa kwanza wa Usaidizi wa Akina Mama.
- Taylor, John
-
John Taylor alikuwa rafiki wa Joseph Smith. Alikuwa pamoja na Joseph katika Jela ya Carthage. Baadaye alikuwa Rais wa Kanisa.
- Whitmer, David
-
David Whitmer alikuwa shahidi aliyeona mabamba ya dhahabu. Alisaidia kuanzisha Kanisa mnamo 6 Aprili 1830.
- Whitmer, Peter
-
Peter Whitmer alisaidia kuanzisha Kanisa mnamo 6 Aprili 1830.
- Whitney, Newel K.
-
Newel K. Whitney alikuwa askofu wa pili wa Kanisa.
- Williams, Frederick G.
-
Frederick G. Williams alikuwa mmoja wa washauri wa Joseph Smith.
- Young, Brigham
-
Brigham Young alikuwa mmoja wa Mitume Kumi na Wawili. Alikuwa kiongozi wa waanzilishi. Alikuwa Rais wa Kanisa baada ya Joseph Smith.
- Young, Phineas
-
Phineas Young alikuwa kaka wa Brigham Young.