Scripture Stories
Watu wa Kuwajua


Watu wa Kuwajua

Ibrahimu

Ibrahimu alikuwa nabii aliyeishi hapo kale. Hadithi ya Ibrahimu ipo katika Agano la Kale na Lulu ya Thamani Kuu.

Bennett, John C.

John C. Bennett alikuwa Meya wa Nauvoo. Yeye alimgeuka Joseph Smith.

Kapteni Allen

Kapteni Allen alikuwa kapteni katika Jeshi la Marekani. Aliwaomba wanaume wa Kanisa kuwa katika Kikosi cha Mormoni.

Copley, Leman

Leman Copley alikuwa muumini wa Kanisa katika Kirtland, Ohio, ambaye hakuwapa ardhi yake waumini wengine.

Cowdery, Oliver

Oliver Cowdery alimsaidia Joseph Smith kutafsiri mabamba ya dhahabu. Alifanya kazi nyingi ili kulisaidia Kanisa.

Elia

Elia alirejesha uwezo maalum wa ukuhani kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery katika Hekalu ya Kirtland.

Eliya

Eliya alikuwa nabii aliyeishi hapo kale. Alirejesha uwezo maalum wa ukuhani kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery katika Hekalu la Kirtland .

Henoko

Henoko alikuwa nabii aliyeishi hapo kale. Yeye alijenga mji wa Sayuni. Hadithi ya Henoko ipo katika Lulu ya Thamani Kuu.

Gavana Boggs

Gavana Boggs alikuwa gavana wa Missouri. Yeye hakuweza kuwasaidia Watakatifu na alitoa amri ya kuwaondoa kutoka jimboni au kuwaua.

Harris, Martin

Martin Harris alimsaidia Joseph Smith kutafsiri mabamba ya dhahabu. Alipoteza kurasa kadhaa za Kitabu cha Mormoni.

Hyde, Orson

Orson Hyde alikuwa Mtume. Aliweka wakfu Nchi Takatifu kwa ajili ya watoto wa Ibrahimu wapate mahali pa kuishi.

Wahindi

Wahindi waliishi katika maeneo yote ya Marekani. Wakati mwingine Wahindi wanaitwa Walamani.

Yakobo

Yakobo alikuwa mmoja wa Mitume Kumi na Wawili wa Yesu. Petro, Yakobo na Yohana, walirejesha Ukuhani wa Melkizedeki kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery.

Yohana

Yohana alikuwa mmoja wa Mitume Kumi na wawili wa Yesu. Petro, Yakobo na Yohana, walirejesha Ukuhani wa Melkizedeki kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery.

Yohana Mbatizaji

Yohana Mbatizaji aliishi wakati Yesu alipoishi duniani. Yohana Mbatizaji alitoa Ukuhani wa Haruni kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery.

Kimball, Heber C.

Heber C. Kimball alikuwa Mtume. Alikwenda misheni huko Uingereza.

Kimball, Sarah

Sarah Kimball alikuwa mshiriki wa Muungano wa kwanza wa Usaidizi wa Akina Mama.

Kimball, Spencer W.

Spencer W. Kimball alikuwa Rais wa 12 wa Kanisa.

Knight, Newel

Newel Knight alikuwa mgonjwa wakati Shetani alipojaribu kumzuia kuomba. Joseph Smith alimponya Newel Knight.

Walamani

Walamani ni uzao wa wana wa Lehi, ambao ni Lamani na Lemueli.

Melkizedeki

Melkizedeki alikuwa nabii aliyeishi hapo kale.

Wamormoni

Wakati mwingine waumini wa Kanisa wanaitwa Wamormoni kwa sababu wanaamini katika Kitabu cha Mormoni.

Moroni

Moroni alikuwa Nabii Mnefi aliyeishi Marekani hapo kale. Alizika mabamba ya dhahabu katika Kilima Kumora.

Musa

Musa alikuwa nabii aliyeishi hapo kale. Aliwaongoza Waisraeli kutoka Misri. Alirejesha uwezo maalum wa ukuhani kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery katika Hekalu la Kirtland.

Bw. Chandler

Bw. Chandler aliuza baadhi ya magombo ya karatasi za kale kwa Watakatifu huko Kirtland. Maandiko ya Ibrahimu yalikuwa kwenye magombo ya karatasi.

Bw. Hale

Bw. Hale alikuwa baba yake Emma Smith.

Nuhu

Nuhu alikuwa nabii aliyeishi miaka mingi iliyopita.

Page, Hiram

Hiram Page alisema alikuwa na jiwe lililompa mafunuo kwa ajili ya Kanisa.

Partridge, Edward

Edward Partridge alikuwa askofu wa kwanza wa Kanisa.

Petro

Petro alikuwa mmoja wa Mitume Kumi na Wawili wa Yesu. Petro, Yakobo na Yohana, walirejesha Ukuhani wa Melkizedeki kwa Joseph Smith na Oliver Cowdery.

Phelps, William W.

William W. Phelps alisaidia kuanzisha shule katika Jackson County, Missouri.

Waanzilishi

Waanzilishi walikuwa Watakatifu waliovuka uwanda kwenda katika Milima ya Miamba.

Pratt, Parley P.

Parley P. Pratt alienda misheni kuwafundisha Walamani.

Richards, Willard

Willard Richards alikuwa rafiki wa Joseph Smith. Alikuwa pamoja na Joseph katika Jela ya Carthage.

Rigdon, Sidney

Sidney Rigdon alikuwa mmoja wa washauri wa Joseph.

Smith, Alvin

Alvin Smith alikuwa mmoja wa kaka wakubwa wa Joseph Smith. Yeye alifariki. Joseph aliona ono la Alvin akiwa katika ufalme wa selestia wa mbinguni.

Smith, Emma

Emma Smith alikuwa mke wa Joseph Smith. Alikuwa kiongozi wa kwanza wa Muungano wa Usaidizi wa Akina Mama. Alitengeneza kitabu cha nyimbo za dini kwa ajili ya Kanisa.

Smith, Hyrum

Hyrum Smith alikuwa mmoja wa kaka mkubwa wa Joseph Smith. Hyrum aliuawa katika Jela ya Carthage pamoja na Joseph.

Smith, Joseph

Joseph Smith alikuwa nabii wa kwanza na Rais wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Yesu alimpa Joseph Smith mafunuo ambayo yanapatikana katika Mafundisho na Maagano. Joseph aliuawa katika Jela ya Carthage.

Smith, Joseph Sr.

Joseph Smith Mkubwa alikuwa baba yake Joseph Smith.

Smith, Lucy

Lucy Smith alikuwa mama yake Joseph Smith.

Smith, Samuel

Samuel Smith alikuwa kaka mdogo wa Joseph Smith. Alikuwa mmisionari wa kwanza wa Kanisa.

Snow, Eliza R.

Eliza R. Snow alikuwa mshiriki wa Muungano wa wa kwanza wa Usaidizi wa Akina Mama.

Taylor, John

John Taylor alikuwa rafiki wa Joseph Smith. Alikuwa pamoja na Joseph katika Jela ya Carthage. Baadaye alikuwa Rais wa Kanisa.

Whitmer, David

David Whitmer alikuwa shahidi aliyeona mabamba ya dhahabu. Alisaidia kuanzisha Kanisa mnamo 6 Aprili 1830.

Whitmer, Peter

Peter Whitmer alisaidia kuanzisha Kanisa mnamo 6 Aprili 1830.

Whitney, Newel K.

Newel K. Whitney alikuwa askofu wa pili wa Kanisa.

Williams, Frederick G.

Frederick G. Williams alikuwa mmoja wa washauri wa Joseph Smith.

Young, Brigham

Brigham Young alikuwa mmoja wa Mitume Kumi na Wawili. Alikuwa kiongozi wa waanzilishi. Alikuwa Rais wa Kanisa baada ya Joseph Smith.

Young, Phineas

Phineas Young alikuwa kaka wa Brigham Young.

Chapisha