Sura ya 5
Joseph Smith na Oliver Cowdery
Februari–Aprili 1829
Joseph na Emma Smith waliishi katika shamba dogo karibu na Harmony, Pennsylvania. Baba yake Joseph alikuja kuwatembelea. Walikuwa na furaha kumwona. Baba yake Joseph alikuwa mtu mwema.
Yesu alimpa Joseph ufunuo kwa ajili ya baba yake. Ufunuo ulieleza jinsi ambavyo watu wangeweza kumsaidia Yesu. Wanapaswa kumpenda Yesu. Wanapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kufundisha injili. Wanapaswa kuwapenda na kuwasaidia watu wengine.
Watu waonataka kumsaidia Yesu wanapaswa pia kuomba na kuwa na imani. Yesu alisema watu wanaomsadia watabarikiwa.
Baba yake Joseph alikwenda nyumbani na kujaribu kufanya mambo ambayo Yesu alimwambia kufanya. Alishiriki injili na wengi wa wana familia yake.
Ilimbidi Joseph afanye kazi katika shamba lake. Pia alihitaji kutafsiri mabamba ya dhahabu. Ilikuwa kazi kubwa mno kwake kufanya peke yake, hivyo alisali na kumwomba Baba wa Mbinguni kwa ajili ya usaidizi.
Baba wa Mbinguni alijibu maombi ya Joseph. Alimtuma mtu mmoja aliyeitwa Oliver Cowdery kwa Joseph. Oliver alitaka kujua kuhusu mabamba ya dhahabu. Joseph alimwambia kuhusu malaika Moroni, mabamba, na Kitabu cha Mormoni.
Oliver alimwamini Joseph na kusema angesaidia kutafsiri mabamba ya dhahabu. Wakati Joseph akisoma maneno kwa sauti, Oliver aliyaandika kwenye karatasi. Joseph na Oliver walifanya kazi kwa bidii.
Yesu aliwafundisha Joseph na Oliver mambo mengi. Alisema wanapaswa kutafuta hekima na uzima wa milele, si utajiri. Alisema pia wanapaswa kujifunza juu ya Mungu na kuwasaidia watu kujifunza injili. Wanapaswa kuwa waaminifu na kufanya mambo mema. Ikiwa wangefanya hivyo, wangeweza kuishi pamoja na Baba wa Mbinguni milele.
Yesu alisema Oliver anapaswa daima kuwa rafiki wa Joseph na kumsaidia katika nyakati ngumu. Yesu pia alisema Oliver angeweza kujifunza kutafsiri kama Joseph. Roho Mtakatifu angemsaidia Oliver kutafsiri ikiwa Oliver alikuwa na imani ya kutosha.
Oliver alijaribu kutafsiri. Alidhani ingekuwa rahisi, lakini hakuweza.
Yesu alisema Oliver hakuwa ameomba msaada wa Mungu katika njia sahihi. Yesu alimwambia Joseph Smith jinsi Oliver na watu wote wanavyoweza kupata msaada kutoka kwa Mungu.
Wakati watu wanapohitaji msaada, wanapaswa kufikiri kwa makini kuhusu nini cha kufanya. Wanapaswa kuamua kile wanachofikiri ni jambo sahihi kufanya.
Kisha wanapaswa kumwuliza Mungu ikiwa ni sahihi. Kama ni sahihi, watajisikia vizuri katika mioyo yao. Watajua ni sahihi.
Kama si sahihi, hawatajisikia vizuri katika mioyo yao.
Oliver hakujaribu kutafsiri Kitabu cha Mormoni tena. Badala yake, aliandika maneno wakati Joseph akiyatafsiri. Yesu alisema Oliver angebarikiwa kwa kumsaidia Joseph.