Scripture Stories
Sura ya 30: Ufunuo kuhusu Vita: Desemba 25 1832


Sura ya 30

Ufunuo kuhusu Vita

Desemba 25, 1832

Picha
nyumba ya majira ya baridi
Picha
Watakatifu wakiwa na wasiwasi

Watu wengi walikuwa wakibatizwa katika Kanisa. Injili iliwafanya wawe na furaha, lakini walikuwa na wasiwasi kuhusu mambo yaliyokuwa yanatokea duniani.

Picha
Jengo likianguka

Matetemeko ya ardhi na vita vilikuwa vikitokea katika sehemu nyingi.

Picha
watu wakitofautiana

Mambo ya kusikitisha pia yalikuwa yakitokea Marekani. Baadhi ya watu hawakutaka kuwa sehemu ya nchi. Walitaka kuwa na viongozi wao wenyewe.

Picha
Joseph anapokea ufunuo

Mnamo Siku ya Krismasi 1832, Yesu alimpa Joseph Smith ufunuo kuhusu vita.

Picha
Watu wakipigana wakati wa Vita ya Wenyewe kwa Wenyewe

Yesu alisema watu nchini Marekani wangepigana vita ya wenyewe kwa wenyewe. Unabii huu ulitimizwa wakati Vita ya Wenyewe kwa Wenyewe ya Marekani ilipoanza miaka 30 baadaye.

Picha
askari

Yesu pia alifunua kwamba kutakuwa na vita katika maeneo mengine yote ya dunia. Watu wengi watakufa, na kutakuwa na huzuni ya kutisha. Yesu alisema Watakatifu wanapaswa kuwa waaminifu katika nyakati hizi ngumu.

Picha
Joseph Smith akitafakari

Joseph Smith alisikitika kujua kwamba kutakuwa na vita vingi hivyo. Alijua kwamba kama watu watatii amri za Mungu, wasingeweza kupigana na kuwa na vita.

Chapisha