Sura ya 24
Wazazi Wanapaswa Kuwafundisha Watoto Wao
Novemba 1831
Baadhi ya wazee katika Kanisa walitaka kujua mapenzi ya Bwana kwao, hivyo walikwenda kwa Nabii Joseph Smith.
Mafundisho na Maagano 68, kichwa cha habari cha sehemu
Joseph aliomba kwa ajili ya mwongozo. Jibu la Bwana lilijumuisha kanuni muhimu kuhusu jinsi ya kuwa wazazi wazuri.
Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao kuhusu Yesu na kuwasaidia kukuza imani Kwake.
Wazazi wanapaswa kufundisha watoto wao jinsi ya kutubu.
Yesu alisema watoto wanapaswa kubatizwa wanapokuwa na umri wa miaka minane. Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao injili kabla ya kubatizwa.
Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao kuhusu kipawa cha Roho Mtakatifu. Wazazi wanapaswa pia kuwafundisha watoto wao jinsi ya kuomba na jinsi ya kumsikiliza Roho Mtakatifu.
Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao kujua na kutii amri za Mungu na kuwa waumini wazuri wa Kanisa.
Wazazi na watoto wanaofuata mafundisho ya Yesu wanaweza kuwa na furaha ya kudumu kama familia.