Scripture Stories
Sura ya 24: Wazazi Wanapaswa Kuwafundisha Watoto Wao: Novemba 1831


Sura ya 24

Wazazi Wanapaswa Kuwafundisha Watoto Wao

Novemba 1831

Picha
gari la kukokotwa na maksai
Picha
Joseph akiomba

Baadhi ya wazee katika Kanisa walitaka kujua mapenzi ya Bwana kwao, hivyo walikwenda kwa Nabii Joseph Smith.

Mafundisho na Maagano 68, kichwa cha habari cha sehemu

Picha
familia ikisoma maandiko

Joseph aliomba kwa ajili ya mwongozo. Jibu la Bwana lilijumuisha kanuni muhimu kuhusu jinsi ya kuwa wazazi wazuri.

Picha
wazazi wakiwafundisha watoto

Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao kuhusu Yesu na kuwasaidia kukuza imani Kwake.

Picha
mama akimfariji mtoto

Wazazi wanapaswa kufundisha watoto wao jinsi ya kutubu.

Picha
mwanamume akimbatiza mwanamke

Yesu alisema watoto wanapaswa kubatizwa wanapokuwa na umri wa miaka minane. Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao injili kabla ya kubatizwa.

Picha
familia ikiomba pamoja

Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao kuhusu kipawa cha Roho Mtakatifu. Wazazi wanapaswa pia kuwafundisha watoto wao jinsi ya kuomba na jinsi ya kumsikiliza Roho Mtakatifu.

Picha
familia ikisoma pamoja

Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao kujua na kutii amri za Mungu na kuwa waumini wazuri wa Kanisa.

Picha
familia yenye furaha

Wazazi na watoto wanaofuata mafundisho ya Yesu wanaweza kuwa na furaha ya kudumu kama familia.

Chapisha