Sura ya 19
Ujio wa Pili wa Yesu Kristo
Baadhi ya watu huko Kirtland, Ohio, hawakutaka kujifunza injili. Baadhi hata walisema uongo kuhusu Watakatifu ili kujaribu kuwazuia wengine kujifunza kuhusu injili.
Mafundisho na Maagano 45, kichwa cha habari cha sehemu
Yesu alimwambia Joseph Smith kuwa Yeye angerudi duniani tena hivi karibuni. Kabla ya Yeye kuja, kila mtu duniani lazima aisikie Injili. Watakatifu wanapaswa kuwa wamisionari wema na kufanya kazi kwa bidii ili kushiriki injili.
Wakati Yesu alipoishi duniani, Aliwaambia Mitume Wake kile kitakachotokea kabla ya Yeye kurudi tena.
Yesu aliwaambia Mitume Wake kwamba hekalu la Yerusalemu lingeharibiwa. Wayahudi watatawanyika kwenye mataifa mengi, na wengi wao watauawa. Kutakuwa na vita nyingi. Watu hawatapendana, na watageuza mioyo yao kutoka kwa Mungu. Kutakuwa na magonjwa ya kutisha, maradhi, na matetemeko ya ardhi. Jua litakuwa giza, mwezi utakuwa kama damu, na nyota zitaanguka.
Tukio moja muhimu katika maandalizi kwa ajili ya kurudi kwa Yesu duniani ni urejesho wa Kanisa Lake. Yesu alisema injili iliyorejeshwa itakuwa kama nuru katika giza.
Mambo mengi ambayo Yesu alizungumza kuyahusu tayari yametokea. Mambo mengine yanaanza kutokea, na mengine yatatokea katika siku zijazo.
Wakati mambo haya yatakapotokea, watu wenye haki watajua Yesu anakuja karibuni. Watamtaka Yeye aje. Wayahudi wengi watarudi Yerusalemu. Wataisikia injili.
Watakatifu wenye haki watajenga mji mpya wa Sayuni, ambapo watakuwa salama. Hawatapigana wao kwa wao. Watakuwa na furaha na kuimba nyimbo za shangwe. Watu ambao si wenye haki hawataweza kwenda Sayuni.
Yesu atakuja duniani katika wingu angavu. Watu wenye haki watamwona. Watu wote wenye haki waliokufa watafufuliwa. Watakutana na Yesu mawinguni na kuja duniani pamoja Naye.
Yesu atakuja Yerusalemu. Atasimama juu ya mlima pale, na utagawanyika mara mbili. Mbingu na nchi zitatikisika. Watu waovu wataangamizwa.
Watu katika Yerusalemu watamwona Yesu na kuuliza, “Je, haya majeraha katika mikono na miguu yako ni ya nini?” Atasema: “Mimi ni Yesu ambaye alisulubiwa. Mimi ni Mwana wa Mungu.” Ndipo watu watakapolia kwa sababu ya uovu wao na kuomboleza kwa sababu Yesu alikuwa ameteswa.
Watu wenye haki watakuwa na furaha tele kumwona Yesu. Dunia nzima itakuwa ni mali yao. Shetani hataweza kuwajaribu. Watoto wao watakua bila dhambi. Yesu ataishi pamoja nao kwa miaka 1,000 na atakuwa Mfalme wao.
Yesu alimwambia Joseph Smith kuwatuma wamisionari ili wawaambie watu kutubu na kujiandaa kwa ajili ya Ujio wa Pili. Yesu alisema Watakatifu pia wanapaswa kujiandaa. Wanapaswa kuomba, kufunga, na kufundishana amri.
Yesu aliwaahidi Watakatifu kwamba kama wangekuwa karibu Naye, Angekuwa karibu nao. Alisema wanapaswa kuomba, na Yeye aliahidi kwamba Mungu angewajibu.
Watakatifu wanapaswa kufanya kila kitu wanachoweza ili kumsaidia Yesu. Wakati watu wanapomsaidia Yesu, wanakuwa kama Yeye. Ndipo watakuwa tayari kwa Ujio Wake wa Pili.