Sura ya 51
Endaumenti za Kwanza
Mei 1842
Picha
Hekalu la Nauvoo
Picha
Hekalu la Nauvoo
Yesu alimwahidi Joseph Smith kwamba Angewapa Watakatifu baraka maalum. Baraka hii inaitwa endaumenti. Endaumenti inatolewa hekaluni. Ni wanaume na wanawake ambao wanatii amri za Mungu ndio pekee wanaoweza kupokea endaumenti.
Picha
Joseph akifundisha kuhusu hekalu
Baadaye, Joseph Smith alifanya mkutano na baadhi ya wanaume na wake zao. Aliwafundisha mambo ambayo wangeweza kufanya hekaluni. Kisha endaumenti zilitolewa kwao wote.
Picha
hekalu la siku za leo
Waumini wa Kanisa ambao wanatii amri za Mungu wanaweza kwenda hekaluni na kupokea baraka maalum ya endaumenti. Kama sehemu ya endaumenti, wanafanya maagano na Mungu, na Yeye anafanya maagano pamoja nao.