Scripture Stories
Sura ya 45: Magenge Zaidi ya watu wenye fujo katika Missouri: 1838–1839


Sura ya 45

Magenge Zaidi ya watu wenye fujo katika Missouri

1838–1839

Picha
wanandoa katika gari la kukokotwa na maksai
Picha
Joseph akiwa na ramani za ujenzi

Watakatifu wengi walikuwa wakiishi Far West, Missouri, ikiwa ni pamoja na Joseph Smith. Watu walijenga makazi na shule na walikuwa na furaha.

Picha
Magenge ya watu wenye fujo yakikusanyika

Lakini Watakatifu hawakuwa na amani kwa muda mrefu. Tena, watu wengine katika Missouri walianza kuwaletea matatizo.

Picha
genge la watu wenye fujo likipanga kuwaumiza Watakatifu.

Genge la watu wenye fujo lilikutana ili kupanga njia za kuwaumiza Watakatifu.

Picha
genge la watu wenye fujo likiwakamata Watakatifu

Genge la watu wenye fujo lilifanya mambo mengi mabaya. Waliwafukuza Watakatifu nje ya makazi yao.

Picha
genge la watu wenye fujo likiharibu makazi

Walichoma makazi yao na kuharibu mashamba yao.

Picha
genge la watu wenye fujo likimpiga mwanamume

Waliwapiga wanaume na kuwaweka baadhi yao jela.

Picha
mwanamume akimuumiza mwanamke

Magenge ya watu wenye fujo yaliwaumiza baadhi ya wanawake.

Picha
Watakatifu wakimwomba msaada Gavana Boggs

Watakatifu walimwomba msaada Gavana Boggs wa Missouri. Lakini watu wengine walikuwa wakimwambia gavana uongo kuhusu Watakatifu, na yeye hakuwasaidia.

Picha
Gavana Boggs akizungumza na watu wake

Matatizo kati ya Watakatifu na magenge ya watu wenye fujo yaliendelea kuwa makubwa. Akidhani kuwa Watakatifu walikuwa wa kulaumiwa kwa matatizo haya, Gavana Boggs aliwaambia baadhi ya askari kuwaua Watakatifu kama hawataondoka Missouri.

Picha
genge la watu wenye fujo likiwashambulia Watakatifu

Baadhi ya Watakatifu waliishi katika mji ulioitwa Haun’s Mill. Siku moja genge la watu wenye fujo lilikuja na kuwashambulia.

Picha
genge la watu wenye fujo likirusha risasi kwenye nyumba ya magogo

Baadhi ya Watakatifu walikimbilia msituni. Wengine walikimbilia kwenye jengo la magogo kwa ajili ya ulinzi. Genge la watu wenye fujo lilipiga risasi kupitia kwenye nyufa za kuta. Kisha genge la watu wenye fujo liliingia kwenye jengo na kupiga risasi nyingi zaidi.

Picha
Watakatifu wakikwepa risasi

Genge liliwaua watu 17 katika Haun’s Mill na kujeruhi wengine 13. Baadhi ya watoto walipigwa risasi na kuuawa.

Picha
genge la watu wenye fujo likiwaibia Watakatifu

Kisha genge la watu wenye fujo liliiba kwenye makazi na kwenye magari ya kukokotwa na maksai ya Watakatifu.

Picha
askari wakitaka kumuua Joseph

Baadaye baadhi ya askari walimteka Joseph Smith na viongozi wengine wa Kanisa. Askari waliambiwa wampige risasi Joseph na rafiki zake.

Picha
askari wakikataa kumuua Joseph

Lakini kiongozi mmoja wa askari hakutii. Alisema itakuwa ni kosa la jinai kumpiga risasi Joseph na wengine.

Picha
Joseph na rafiki zake wakiwa katika minyororo

Kesi ilipangwa dhidi ya Joseph na rafiki zake. Kabla na wakati wa kesi, waliwekwa gerezani katika mji wa Richmond, Missouri. Walinzi waliwafunga kwa minyororo. Joseph na rafiki zake walilala kwenye sakafu yenye baridi.

Picha
walinzi wakicheka

Walinzi walikuwa wakatili sana kwa wafungwa. Waliapa na kusimulia hadithi mbaya. Walisimulia jinsi walivyowaibia na kuwaua Watakatifu. Walisimulia jinsi walivyowaumiza wanawake na watoto. Usiku mmoja walicheka na kujivuna kwa masaa kadhaa.

Picha
Joseph akiwakemea walinzi waovu

Joseph alichukia kile walichokuwa wakikisema. Hakutaka kusikia lolote zaidi, hivyo alisimama na kuwaamuru kunyamaza. “Kimya,” alisema. “Katika jina la Yesu Kristo … nawaamuru kutulia; sitaishi dakika nyingine na kusikia lugha kama hiyo. Sitisheni maongezi kama hayo, au la ninyi au mimi tufe sasa hivi!” Walinzi waliingiwa na hofu na kumwomba Joseph samahani. Walikaa katika kona na walikuwa kimya usiku wote.

Chapisha