Scripture Stories
Sura ya 58: Kiongozi Mpya kwa ajili ya Kanisa: Julai–Agosti 1844


Sura ya 58

Kiongozi Mpya kwa ajili ya Kanisa

Julai–Agosti 1844

Picha
Hekalu la Nauvoo
Picha
Watakatifu wakizungumza pamoja

Baada ya Nabii Joseph Smith kuuawa, Kanisa halikuwa na Rais. Watakatifu hawakuwa na uhakika ni nani aliyepaswa kuwa kiongozi wao.

Picha
Mitume wakitumikia misheni

Wengi wa Mitume walikuwa mbali kwenye misheni.

Picha
Sidney Rigdon akiondoka Nauvoo

Sidney Rigdon alikuwa mshauri wa Joseph Smith. Lakini hakuwa amemtii Bwana na alikuwa ameondoka Nauvoo.

Picha
Sidney Rigdon akirejea Nauvoo

Wakati Sidney Rigdon aliposikia kwamba Joseph Smith alikuwa amefariki, alirudi Nauvoo. Alitaka kuwa kiongozi wa Kanisa.

Picha
Mitume wakirejea kutoka misheni

Mitume waliokuwa mbali katika misheni pia walirudi Nauvoo waliposikia juu ya kifo cha Joseph. Brigham Young alikuwa kiongozi wa Mitume. Alisema Bwana alikuwa amewapa mitume mamlaka ya kuongoza Kanisa hadi Rais mpya atakapochaguliwa.

Picha
Sidney Rigdon akizungumza kwa sauti

Waumini wa Kanisa walikuwa na mkutano. Kwanza Sidney Rigdon alizungumza nao na kusema alipaswa kuwa kiongozi wa Kanisa.

Picha
Brigham Young akijitokeza kama Joseph

Kisha Brigham Young alizungumza na kusema Mitume walipaswa kuongoza Kanisa. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye. Sauti ya Brigham Young iikuwa kama sauti ya Joseph Smith, na kwa baadhi ya watu alionekana kama Joseph Smith. Watakatifu walijua kwamba Mungu aliwachagua Mitume ili kuongoza Kanisa, na wote walipiga kura ya kuwakubali Mitume kama viongozi wao. Sidney Rigdon alikasirika. Alirudi nyumbani kwake na kuanzisha kanisa lake mwenyewe. Hakuwa tena muumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za Mwisho.

Chapisha