Scripture Stories
Sura ya 20: Vipawa vya Roho: Machi 8 1831


Sura ya 20

Vipawa vya Roho

Machi 8, 1831

Picha
ubatizo
Picha
Joseph anapokea ufunuo

Joseph Smith alipokea mafunuo mengi ambayo yalifundisha juu ya Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu ni Roho anayemsaidia Baba wa Mbinguni na Yesu. Roho Mtakatifu hana mwili wa nyama na mifupa.

Picha
mtoto akipokea Kipawa cha Roho Mtakatifu

Kupitia nguvu ya Roho Mtakatifu, Mungu hutoa vipawa maalum kwa waumini wa Kanisa. Hivi huitwa vipawa vya Roho, au vipawa vya kiroho. Kila Mtakatifu ana angalau kipawa kimoja cha roho. Waumini wa kanisa wanapaswa kujifunza kuhusu vipawa vyao na kuvitumia ili kusaidiana. Yesu alimwambia Joseph Smith baadhi ya vipawa hivi.

Picha
muumini akitoa ushuhuda wake

Baadhi ya Watakatifu wamepewa kipawa cha kujua kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu. Wanajua Yeye alikufa kwa ajili yetu. Watakatifu wengine wanapewa kipawa cha kutambua na kuamini shuhuda za kweli za watu wengine kuhusu Yesu.

Picha
kiongozi akifundisha watu wake

Baadhi ya Watakatifu wanapewa kipawa cha kuwa viongozi.

Picha
mwanamke akiomba

Baadhi ya Watakatifu wanapewa kipawa cha kujua tofauti kati ya roho wa haki na wa uovu. Roho za haki zinatumwa na Mungu na hutufanya tujisikie vizuri. Roho za uovu zinatumwa na Shetani na huleta hisia mbaya.

Picha
mtu akifundisha kutoka kwenye maandiko

Baadhi ya Watakatifu hupewa kipawa cha hekima. Kipawa hiki kinawasaidia kufanya maamuzi mazuri na kutumia vizuri maarifa ambayo Baba wa Mbinguni huwapa. Baadhi ya Watakatifu hupewa kipawa cha maarifa. Wale walio na kipawa hiki wanapaswa kuwafundisha wengine na kuwasaidia kufanya maamuzi yenye hekima.

Picha
mwanamume akimbariki mtoto

Baadhi ya Watakatifu wanapewa kipawa cha imani ya kuponywa. Wengine hupewa kipawa cha kuponya watu wagonjwa. Roho Mtakatifu huwapa baadhi ya Watakatifu kipawa cha kufanya miujiza. Miujiza huonyesha uwezo wa Mungu.

Picha
mtu akizungumza na Wenyeji wa Amerika

Baadhi ya Watakatifu wanapewa kipawa cha kuzungumza kwa lugha wasizozijua.

Picha
Joseph akiona ono la Hekalu la Salt Lake

Baadhi ya Watakatifu wanapewa kipawa cha unabii. Kipawa hiki kinawasaidia kujua na kuelewa mambo yaliyotokea katika siku za nyuma, mambo yanayotokea sasa, na mambo ambayo yatatokea katika siku zijazo.

Picha
mtu akihubiri

Baadhi ya Watakatifu wamepewa vipawa vingi. Watakatifu wote wanapaswa kutumia vipawa vyao kuwatumikia na kuwabariki wengine.

Picha
askofu anakutana na dada

Askofu anaweza kujua ni vipawa gani kila Mtakatifu anacho. Anajua ni nani watakuwa walimu wazuri. Anajua ni Watakatifu gani wanampenda Mungu na kutii amri.

Picha
msichana mdogo akiwa amepiga magoti katika kuomba

Watakatifu wenye haki wanapaswa kufanya kazi na kuomba ili kupewa vipawa wanavyohitaji. Vipawa hivi vyote vinatoka kwa Mungu.

Chapisha