Scripture Stories
Sura ya 13: Joseph na Emma: Julai 1830


Sura ya 13

Joseph na Emma

Julai 1830

Picha
ubatizo
Picha
Emma na Joseph

Joseph na Emma Smith waliishi katika shamba dogo huko Pennsylvania. Walipendana na kufanya kazi kwa bidii ili kusaidiana.

Picha
Joseph na Emma

Joseph na Emma walivumilia magumu mengi. Walikuwa na mtoto wa kiume, lakini alifariki. Walihuzunika sana.

Picha
Joseph akipanda mbegu

Joseph alikuwa na wasiwasi juu ya familia yake. Walikuwa masikini, na alitaka kuwatunza. Alihitaji kupanda mazao ili familia yake iweze kupata chakula.

Picha
Joseph akifundisha

Joseph pia alikuwa na wasiwasi kuhusu Kanisa. Baadhi ya Watu waliendelea kuleta matatizo kwa Watakatifu, na baadhi ya viongozi wa Kanisa iliwabidi wajifiche mbali nao.

Picha
Joseph akisema kwa heri kwa Emma

Wakati mwingine ilimbidi Joseph aondoke nyumbani ili kuwasaidia Watakatifu. Joseph alihuzunika kuondoka, na Emma alikuwa na wasiwasi wakati alipokwenda mbali.

Picha
Joseph akipokea faraja kutoka kwa Mungu

Joseph aliomba ili kujua kile alichopaswa kufanya. Yesu alimwambia asiwe na hofu juu ya watu waliokuwa wakijaribu kumdhuru. Yesu alisema Joseph alipaswa kuwa na subira katika mateso yake. Alisema daima angemsaidia Joseph.

Picha
Watakatifu wakimpa Joseph chakula

Yesu alisema Joseph alipaswa kupanda mazao yake na kisha kwenda kuwasaidia Watakatifu katika maeneo mengine. Yesu pia alimwambia asiwe na wasiwasi juu ya chakula, nguo, au fedha. Watakatifu wangempa kile alichohitaji.

Picha
Emma akiwafundisha wanawake wengine

Yesu alimpa Joseph Smith ufunuo kwa ajili ya Emma. Yesu alisema Emma Smith alikuwa mwanamke wa kipekee. Alikuwa amemchagua ili afanye kazi muhimu.

Picha
Emma akimfariji Joseph

Yesu alisema Emma alipaswa kumfariji Joseph wakati alipokuwa na matatizo. Alipaswa kumsaidia kuwa na furaha na si kuwa na wasiwasi.

Picha
Emma akifundisha kutoka kwenye maandiko

Yesu alisema Emma alipaswa kuwafundisha Watakatifu na kuwasaidia kujifunza maandiko. Alisema Roho Mtakatifu angemsaidia kujua nini cha kufundisha.

Picha
Emma akijifunza nyumbani

Yesu pia alisema Emma alipaswa kutumia muda wake ili kujifunza. Alipaswa kujifunza na kuandika mambo mengi.

Picha
Emma akitafuta kwenye vitabu

Yesu alimwomba Emma kuchagua nyimbo kwa ajili ya Watakatifu kuimba. Nyimbo zingechapishwa katika kitabu cha nyimbo.

Picha
watakatifu wakiimba

Baba wa Mbinguni anapenda kuwasikia watu wenye haki wakiimba. Nyimbo zao ni maombi Kwake, na maombi haya yatajibiwa kwa baraka.

Picha
Joseph na Emma

Yesu alimwambia Emma kuwa mnyenyekevu na kumpenda mumewe. Alimwambia awe na furaha kwa sababu ya baraka ambazo zingemjia Joseph.

Picha
Emma Smith

Yesu alimwaambia Emma kuwa na furaha na kushangilia. Alimwambia pia ashike maagano yake. Ikiwa angefanya hivyo, angepokea baraka kubwa na kuweza kurudi kuishi pamoja Naye mbinguni.

Picha
Watakatifu kutoka nchi nyingi

Yesu alisema kwamba mambo aliyomwelezea Emma Smith ni kwa ajili ya watu wote.

Chapisha