Sura ya 13
Joseph na Emma
Julai 1830
Joseph na Emma Smith waliishi katika shamba dogo huko Pennsylvania. Walipendana na kufanya kazi kwa bidii ili kusaidiana.
Joseph na Emma walivumilia magumu mengi. Walikuwa na mtoto wa kiume, lakini alifariki. Walihuzunika sana.
Joseph alikuwa na wasiwasi juu ya familia yake. Walikuwa masikini, na alitaka kuwatunza. Alihitaji kupanda mazao ili familia yake iweze kupata chakula.
Joseph pia alikuwa na wasiwasi kuhusu Kanisa. Baadhi ya Watu waliendelea kuleta matatizo kwa Watakatifu, na baadhi ya viongozi wa Kanisa iliwabidi wajifiche mbali nao.
Wakati mwingine ilimbidi Joseph aondoke nyumbani ili kuwasaidia Watakatifu. Joseph alihuzunika kuondoka, na Emma alikuwa na wasiwasi wakati alipokwenda mbali.
Joseph aliomba ili kujua kile alichopaswa kufanya. Yesu alimwambia asiwe na hofu juu ya watu waliokuwa wakijaribu kumdhuru. Yesu alisema Joseph alipaswa kuwa na subira katika mateso yake. Alisema daima angemsaidia Joseph.
Yesu alisema Joseph alipaswa kupanda mazao yake na kisha kwenda kuwasaidia Watakatifu katika maeneo mengine. Yesu pia alimwambia asiwe na wasiwasi juu ya chakula, nguo, au fedha. Watakatifu wangempa kile alichohitaji.
Yesu alimpa Joseph Smith ufunuo kwa ajili ya Emma. Yesu alisema Emma Smith alikuwa mwanamke wa kipekee. Alikuwa amemchagua ili afanye kazi muhimu.
Yesu alisema Emma alipaswa kumfariji Joseph wakati alipokuwa na matatizo. Alipaswa kumsaidia kuwa na furaha na si kuwa na wasiwasi.
Yesu alisema Emma alipaswa kuwafundisha Watakatifu na kuwasaidia kujifunza maandiko. Alisema Roho Mtakatifu angemsaidia kujua nini cha kufundisha.
Yesu pia alisema Emma alipaswa kutumia muda wake ili kujifunza. Alipaswa kujifunza na kuandika mambo mengi.
Yesu alimwomba Emma kuchagua nyimbo kwa ajili ya Watakatifu kuimba. Nyimbo zingechapishwa katika kitabu cha nyimbo.
Baba wa Mbinguni anapenda kuwasikia watu wenye haki wakiimba. Nyimbo zao ni maombi Kwake, na maombi haya yatajibiwa kwa baraka.
Yesu alimwambia Emma kuwa mnyenyekevu na kumpenda mumewe. Alimwambia awe na furaha kwa sababu ya baraka ambazo zingemjia Joseph.
Yesu alimwaambia Emma kuwa na furaha na kushangilia. Alimwambia pia ashike maagano yake. Ikiwa angefanya hivyo, angepokea baraka kubwa na kuweza kurudi kuishi pamoja Naye mbinguni.
Yesu alisema kwamba mambo aliyomwelezea Emma Smith ni kwa ajili ya watu wote.