Scripture Stories
Sura ya 34: Mungu Anawaonya Watu wa Sayuni: Julai–Agosti 1833


Sura ya 34

Mungu Anawaonya Watu wa Sayuni

Julai–Agosti 1833

Picha
nyumba ya majira ya baridi
Picha
Watakatifu wakijenga maduka Missouri

Mungu aliwaamuru Watakatifu zaidi kwenda Jackson County, Missouri. Watu wapya walifika huko karibu kila wiki, na walijenga nyumba, maduka na kiwanda cha uchapishaji.

Picha
watu wenye hasira

Watakatifu katika Missouri walikuwa na amani na furaha kwa muda. Hata hivyo, ghafla matatizo yakaibuka. Baadhi ya Watakatifu walikuwa wakaidi na wakatili. Baadhi yao walibishana na viongozi wao. Watu wengine walioishi huko walianza kuwa na wasiwasi kuhusu Watakatifu wengi waliokuwa wakihamia katika eneo hilo. Watu hawa waliwataka Watakatifu kuondoka.

Picha
genge la watu wenye fujo likiwa limekusanyika dhidi ya Watakatifu

Genge la watu wenye hasira lilikutana. Walituma baadhi ya watu kuwaambia viongozi wa Kanisa kuwa Watakatifu lazima waondoke Jackson County. Lakini viongozi walijua kwamba Mungu aliwataka kujenga mji wa Sayuni katika Jackson County. Waliwaambia watu kwamba Watakatifu wasingeweza kuondoka.

Picha
genge la watu wenye fujo likiharibu kiwanda cha uchapishaji

Wanaume katika genge hilo walikuwa na hasira sana. Walivunja na kuingia ndani ya kiwanda cha uchapishaji cha Watakatifu na kukiharibu.

Picha
genge la watu wenye fujo likiwa limejiandaa kupaka lami na kumwaga manyoya

Kisha, genge liliwakamata Askofu Partridge na Charles Allen na kuweka lami na manyoya kwenye ngozi zao. Genge pia liliwapiga baadhi ya Watakatifu wengine.

Picha
genge la watu wenye fujo likiwa na bunduki

Siku tatu baadaye, washiriki wa genge walipita mjini na kufyatua bunduki zao kwenye majengo. Waliwaambia Watakatifu mambo mabaya kwa sauti kubwa na kusema wangemchapa mtu yeyote watakayemshika. Walichoma mazao na kubomoa nyumba, maghala, na maduka.

Picha
Olivery Cowdery akielekea Kirtland

Oliver Cowdery alikuwa mmoja wa viongozi wa Kanisa katika Missouri. Alitumwa kwenda Kirtland kumwona Joseph Smith.

Picha
Joseph akimsalimu Oliver

Wakati Oliver alipowasili Kirtland, alimwambia Joseph kile kilichokuwa kikitendeka Jackson County. Watakatifu huko walitaka kujua cha kufanya.

Picha
Watakatifu wakileta chakula ghalani

Joseph alimwambia Oliver kuhusu baadhi ya mafunuo aliyopokea. Bwana alikuwa amefunua kuwa Watakatifu wanapaswa kujenga hekalu katika Sayuni. Hekalu lingelipiwa kutoka kwenye zaka za watu. Yesu alimwambia Joseph kwamba Sayuni ingekuwa kubwa ikiwa Watakatifu wangekuwa watiifu. Lakini Watakatifu wangeadhibiwa ikiwa hawakuwa watiifu.

Picha
kundi la watu wakipiga kura

Yesu alisema Watakatifu wanapaswa kutii sheria za nchi. Wanapaswa kuwapigia kura watu waadilifu kuwa viongozi wa nchi. Wakati watu waovu wanapokuwa viongozi, watu wanasikitika.

Picha
familia ikingojea genge la watu wenye fujo liondoke

Bwana aliwaamuru Watakatifu kutii maneno Yake yote. Alisema hawapaswi kuwaogopa maadui zao. Badala yake, Watakatifu wanapaswa kuwasamehe maadui zao. Hawapaswi kupigana na adui zao isipokuwa Mungu amewaamuru kupigana. Bwana alisema ya kwamba Yeye angewaadhibu watu waovu.

Picha
Watakatifu wakiwekea viunzi majengo

Wiki chache baadaye, Yesu alisema Watakatifu katika Sayuni wangekuwa na matatizo kwa muda kwa sababu hawakutii amri. Hata hivyo, Yesu aliahidi kwamba siku moja angewasaidia Watakatifu kujenga Sayuni.

Chapisha