Scripture Stories
Sura ya 54: Mungu na Malaika: Februari–Aprili 1843


Sura ya 54

Mungu na Malaika

Februari–Aprili 1843

Picha
Hekalu la Nauvoo
Picha
mtu akizungumza na Joseph

Siku moja mtu mmoja aliyesema alikuwa amemwona malaika alikuja kumwona Joseph Smith. Mtu huyo alimwambia Joseph jinsi malaika alivyokuwa amevaa. Joseph alisema kuwa mtu huyo hakuwa amemwona malaika kwa sababu malaika hawavai jinsi ambavyo mtu huyo alivyokuwa ameeleza.

Picha
mtu akionyesha hisia za hasira kwa Joseph

Mtu huyo alikasirika sana. Aliamuru moto ushuke kutoka mbinguni umchome Nabii na nyumba yake. Lakini mtu huyo hakuwa na nguvu za Mungu, na hakuna moto ulioshuka kutoka mbinguni.

Picha
Joseph anaona ono la malaika

Yesu alimpa Joseph Smith ufunuo kuhusu malaika. Yesu alisema kwamba malaika ni watu ambao wameishi duniani, wakafa, na kufufuka. Wana miili ya nyama na mifupa.

Picha
Mtu akitazama mbinguni

Yesu alisema Shetani anajaribu kuwalaghai watu. Wakati mwingine anafanya watu wafikiri kuwa yeye ni malaika. Anajaribu kuwashawishi watu kufanya mambo mabaya. Lakini watu wenye haki wanaweza kujua wakati Shetani anapojaribu kuwalaghai.

Picha
malaika wanaishi na Mungu.

Baadaye, Joseph Smith aliwaambia Watakatifu kweli zingine kuhusu mbinguni. Alisema kwamba malaika hawaishi katika sayari kama dunia. Badala yake, wanaishi na Mungu. Joseph pia alisema kuwa watu mbinguni watajua kila kitu walichojifunza duniani.

Picha
malaika akiwa ameshikilia sheria za Mbinguni

Joseph Smith alisema kwamba sheria zote za Mungu zilitengenezwa mbinguni kabla ya kuja kwetu duniani. Kuna baraka kwa kila sheria. Ni lazima tutii sheria ili kupokea baraka.

Picha
Yesu akiwa na mwili wa nyama na mifupa

Joseph Smith aliwaambia Watakatifu kuhusu Yesu Kristo na Baba wa Mbinguni. Yesu anafanana kama mwanadamu na ana mwili wa nyama na mifupa.

Picha
Baba wa Mbinguni akiwa na mwili wa nyama na mifupa.

Baba wa Mbinguni pia ana mwili wa nyama na mifupa. Yeye anaishi katika sehemu nzuri, na inayong`aa.

Picha
Joseph akitazama mbinguni

Joseph Smith pia alisema Roho Mtakatifu ni roho. Roho Mtakatifu hana mwili wa nyama na mifupa.

Chapisha