Scripture Stories
Sura ya 37: Viongozi wa Ukuhani: Februari–Machi 1835


Sura ya 37

Viongozi wa Ukuhani

Februari–Machi 1835

Picha
nyumba ya majira ya baridi
Picha
Joseph akizungumza

Joseph Smith aliwaomba wanaume wa Kambi ya Sayuni pamoja na wengine kuja kwenye mkutano muhimu katika Kirtland, Ohio. Joseph aliwaambia wanaume kwamba Yesu alitaka mitume kumi na wawili waitwe ili kusaidia kuongoza Kanisa.

Picha
Oliver Cowdery, David Whitmer, na Martin Harris

Bwana alikuwa amemwambia Oliver Cowdery, David Whitmer, na Martin Harris kuchagua Mitume. Kwenye mkutano, Oliver, David, na Martin walibarikiwa na Urais wa Kwanza wa Kanisa. Kisha wakaomba pamoja na kuchagua wanaume wema kumi na wawili.

Picha
Urais wa Kwanza wakiwatawaza Mitume

Wanaume kumi na wawili walitawazwa kuwa Mitume. Kuitwa kwa Mitume ilikuwa ni moja ya matukio muhimu zaidi katika urejesho wa Kanisa la Bwana.

Picha
Mitume Kumi na Wawili

Mitume ni viongozi muhimu sana katika Kanisa. Wanajua kwamba Yesu ni Mwokozi wetu. Wanafundisha injili ulimwenguni kote.

Picha
washiriki wa Sabini

Baada ya siku chache, wanaume wengine walichaguliwa kuwa viongozi katika Kanisa. Waliitwa Sabini. Sabini waliwasaidia Mitume.

Picha
Mitume Kumi na Wawili katika mkutano

Siku moja Mitume Kumi na Wawili walikuwa katika mkutano. Walikuwa wakijitayarisha kwenda misheni, na walitaka usaidizi wa Baba wa Mbinguni.

Picha
Joseph na Mitume wakiwa wamepiga magoti katika maombi

Mitume walimwomba Joseph Smith kuomba kwa ajili ya ufunuo ili kuwasaidia katika misheni zao. Yesu alimpa Joseph na Mitume ufunuo mkuu ambao ndani yake aliwaambia kuhusu ukuhani.

Mafundisho na Maagano 107, kichwa cha habari cha sehemu

Picha
akina kaka wenye ukuhani wakitoa baraka

Ukuhani ni uwezo wa Mungu. Ni uwezo mkuu zaidi duniani. Mungu anatoa ukuhani kwa watu waadilifu. Wanaume ambao wana ukuhani wanaweza kuruhusiwa kuhubiri injili, kufanya ibada, na kuwa viongozi katika Kanisa.

Picha
Wenye Ukuhani wa Melkizedeki

Kuna ukuhani wa aina mbili katika Kanisa. Moja ni ukuhani wa Melkizedeki, ambao pia huitwa ukuhani mkuu zaidi. Rais wa Kanisa, washauri wake, Mitume Kumi na Wawili, na Sabini wote wana Ukuhani wa Melkizedeki.

Picha
Joseph akizungumza na Urais wa Kwanza

Rais wa Kanisa ni Nabii wa Mungu. Yeye anawaambia watu yale ambayo Yesu anataka wafanye. Nabii ana washauri ambao humsaidia. Nabii na washauri wake ni Urais wa Kwanza wa Kanisa.

Picha
Makuhani wakuu katika Ukuhani wa Melkizedeki.

Makuhani wakuu pia wana Ukuhani wa Melkizedeki. Viongozi wengi katika vigingi na kata ni makuhani wakuu. Hawa ni pamoja na marais wa vigingi, Maaskofu, na wajumbe wa baraza kuu.

Picha
wazee katika Ukuhani wa Melkizedeki

Wanaume ambao wametawazwa kama wazee pia wana Ukuhani wa Melkizedeki. Wazee wanapaswa kuwafundisha waumini wa Kanisa na kuwachunga.

Picha
wazee wakiondoka kwenda misheni

Wazee pia huitwa kwenda kwenye misheni kufundisha injili kwa watu ulimwenguni kote.

Picha
Wenye Ukuhani wa Melkizedeki wakitoa baraka

Wanaume wote ambao wana Ukuhani wa Melkizedeki wanaweza kubariki watu. Wanaweza pia kuwapa watu Roho Mtakatifu.

Picha
Wenye Ukuhani wa Haruni wakibariki sakramenti

Ukuhani mwingine ni Ukuhani wa Haruni, ambao pia unaitwa ukuhani mdogo. Ukuhani wa Haruni unajumuisha ofisi za askofu, kuhani, mwalimu, na shemasi. Makuhani wanaweza kubatiza watu, kubariki sakramenti, na kuwasaidia wazee.

Picha
Waalimu wa nyumbani wakimtembelea muumini

Walimu huandaa sakramenti. Wanafanya mafundisho ya nyumbani na kusaidia waumini wa Kanisa kuishi maisha mema.

Picha
shemasi akipitisha sakramenti

Mashemasi wakipitisha sakramenti. Wao pia hukusanya sadaka ya mfungo na kumsaidia askofu.

Picha
Joseph akielekeza

Yesu alisema watu wote ambao wana ukuhani wanapaswa kujifunza yale Mungu anayotaka wafanye. Ikiwa watafanya kazi kwa bidii, Baba wa Mbinguni atawabariki.

Chapisha