Sura ya 47
Watakatifu Wanaondoka Missouri
Msimu wa Baridi 1839
Wakati Joseph Smith alipokuwa jela, mengi ya majukumu ya kuongoza Watakatifu yaliwekwa juu ya Brigham Young, mmoja wa Mitume. Alifanya mkutano ili kuwaambia Watakatifu kwamba ni lazima waanze kujiandaa ili kuondoka Missouri. Wengi wa Watakatifu walikuwa masikini na hawakuwa na magari ya kukokotwa na maksai au farasi. Wanaume katika mkutano walisema wangewasaidia Watakatifu masikini kuhama.
Watakatifu walianza kuondoka Missouri mnamo Februari 1839, wakati ilipokuwa baridi kali. Waliambiwa kwamba watu katika jimbo la Illinois wanaweza kuwa marafiki kwao, hivyo walisafiri maili 200 kuelekea magharibi mwa Illinois. Wengi wao walikwenda katika mji wa Quincy, ambapo watu walikuwa wakarimu na waliwapa malazi, chakula, na ajira.
Gavana Boggs na rafiki zake walifurahia kuona Watakatifu waliondoka Missouri.