Scripture Stories
Sura ya 6: Joseph na Oliver Wanapewa Ukuhani: Mei 1829


Sura ya 6

Joseph na Oliver Wanapewa Ukuhani

Mei1 829

Picha
mabamba ya dhahabu
Picha
Joseph akimwelekeza Oliver

Joseph Smith na Oliver Cowdery walikuwa wakitafsiri Kitabu cha Mormoni. Walisoma juu ya ubatizo na walitaka kujua mengi zaidi kuhusu hilo.

Picha
Joseph na Oliver wakiomba

Joseph na Oliver waliamua kumwomba Mungu. Walikuwa na imani kwamba Yeye angewasaidia kujifunza ukweli. Mnamo 15 Mei 1829, walikwenda msituni na kuomba.

Picha
Yohana Mbatizaji akiwatokea Joseph na Oliver

Mjumbe wa mbinguni alikuja kwa Joseph na Oliver. Alikuwa ni Yohana Mbatizaji, aliyembatiza Yesu zamani. Mwanga mkali ulimzunguka kote.

Picha
Yohana Mbatizaji akitunukia Ukuhani wa Haruni

Yohana Mbatizaji alikuwa amekuja kuwatunukia Joseph na Oliver Ukuhani wa Haruni. Ukuhani ni uwezo wa Mungu. Ukuhani wa Haruni unajumuisha mamlaka ya kubatiza watu.

Picha
Joseph akimbatiza Oliver

Yohana Mbatizaji aliwaambia Joseph na Oliver wabatizane. Joseph alimbatiza Oliver, na kisha Oliver akambatiza Joseph. Walishuka chini ya maji walipobatizwa.

Picha
Yohana Mbatizaji akimbatiza Yesu

Zamani, Yohana Mbatizaji alikuwa amembatiza Yesu kwa njia hiyo hiyo. Yesu alikuwa ameshuka chini ya maji pale alipobatizwa.

Picha
Joseph na Oliver

Joseph na Oliver walijawa na Roho Mtakatifu baada ya kubatizwa. Roho Mtakatifu aliwaambia Kanisa la kweli la Yesu Kristo punde lingekuwepo duniani tena.

Picha
Joseph na Oliver pamoja na wengine

Joseph na Oliver waliwaambia marafiki zao wema kuwa walikuwa wamebatizwa. Pia waliwaambia kuhusu ukuhani. Lakini Joseph na Oliver hawakuwaambia watu wengine mara moja. Walijua kwamba baadhi ya watu wasingewaamini na wangewaletea matatizo.

Picha
Petro, Yakobo, na Yohana wakitunukia Ukuhani wa Melkizedeki

Baadaye, wajumbe wengine watatu wa mbinguni walikuja. Walikuwa Petro, Yakobo na Yohana, ambao walikuwa Mitume watatu wa mwanzo wa Yesu. Petro, Yakobo na Yohana waliwapa Joseph Smith na Oliver Cowdery Ukuhani wa Melkizedeki. Huu pia unaitwa ukuhani “mkubwa.”

Picha
Baraka za Ukuhani

Mara baada ya ukuhani kurejeshwa, wanaume waadilifu wangeweza kupewa mamlaka ya kusaidia kufanya kazi ya Mungu duniani. Wanaume wenye Ukuhani wa Melkizedeki wanaweza kuwa viongozi wa Kanisa. Wanaweza kutoa baraka kwa watu. Wanaweza pia kuwapa watu kipawa cha Roho Mtakatifu. Urejesho wa ukuhani ni baraka kubwa.

Chapisha