Scripture Stories
Sura ya 50: Watakatifu katika Nauvoo: Januari–Julai 1841


Sura ya 50

Watakatifu katika Nauvoo

Januari–Julai 1841

Picha
Hekalu la Nauvoo
Picha
Joseph akiomba

Watakatifu walikuwa wanajenga Nauvoo kuwa mji mzuri. Mji ulikua haraka wakati waumini wapya wa Kanisa walipokusanyika huko kutoka Uingereza na maeneo mengine. Yesu alimpa Joseph Smith ufunuo muhimu kuhusu kile Watakatifu walichopaswa kufanya katika Nauvoo.

Picha
Watakatifu wakijenga hekalu Nauvoo

Yesu alimwambia Joseph Smith kuandika barua akiwaambia wafalme wote na viongozi duniani kuhusu injili iliyorejeshwa. Yesu pia alisema Watakatifu walipaswa kujenga hekalu katika Nauvoo. Aliwataka kuleta dhahabu, fedha, vyuma vingine, na aina nyingi za mbao nzuri ili kujenga hekalu.

Picha
Yesu Kristo

Yesu alisema Angekuja hekaluni. Huko Angetoa Ufunuo kuhusu ukuhani. Pia Angerejesha ibada na kufunua maarifa zaidi.

Picha
waumini wakifanya ubatizo kwa ajili ya wafu

Yesu alimwambia Joseph kuwa Watakatifu wangeweza kubatizwa kwa ajili ya watu ambao wamekufa. Yesu alisema Watakatifu walipaswa kujenga kisima cha ubatizo ndani ya hekalu ambapo wangeweza kubatizwa kwa ajili ya wafu.

Picha
Hyrum akitoa baraka ya patriaki

Yesu pia alifunua kwamba Hyrum Smith, kaka yake Joseph, alipaswa kuwa patriaki wa Kanisa. Kama patriaki, Hyrum angetoa baraka maalum kwa waumini wa Kanisa.

Picha
Brigham Young akizungumza

Yesu pia alimpa Joseph Smith ufunuo kuhusu Brigham Young. Yesu alisema alijua kuwa Brigham alifanya kazi kwa bidii kwa ajili ya Kanisa. Alikuwa ameacha nyumba na familia yake mara nyingi ili kutumikia misheni.

Picha
Brigham akiihudumia familia yake

Yesu alimwambia Brigham Young kwamba alipaswa kukaa na familia yake na kuwapa matunzo maalum.

Chapisha