Scripture Stories
Sura ya 15: Misheni kwa Walamani: Septemba 1830


Sura ya 15

Misheni kwa Walamani

Septemba 1830

Picha
ubatizo
Picha
Oliver Cowdery

Yesu alitaka watu wengi zaidi kusikia juu ya injili. Alitaka baadhi ya Watakatifu waende misheni. Alimwita Oliver Cowdery kwenda misheni kwa Wahindi wa Kiamerika. Wahindi hawa pia waliitwa Walamani kwa sababu baadhi yao walikuwa uzao wa Walamani katika Kitabu cha Mormoni.

Picha
Yesu akizungumza na Mnefi

Yesu alitaka Walamani wasome Kitabu cha Mormoni. Alikuwa amewaahidi manabii wengi kwamba Walamani wangepata Kitabu cha Mormoni. Sasa ilikuwa ni wakati wa kutimiza ahadi hiyo.

Picha
Yesu akizungumza na Walamani

Kitabu cha Mormoni kinawaelezea Walamani kuhusu mababu zao walioishi mamia ya miaka iliyopita. Kinawaambia kuhusu ahadi muhimu ambazo Yesu aliwaahidi. Kinawasaidia kuamini katika Yesu. Kinawafundisha kutubu na kubatizwa.

Picha
wanaume wa Kanisa

Baadhi ya wanaume walitaka kwenda na Oliver Cowdery kuhubiri injili kwa Walamani. Bwana alisema watatu kati ya wanaume hao wangeweza kwenda.

Picha
wamisionari wakiwafundisha Wenyeji wa Amerika

Kwanza wamisionari walikwenda kwa baadhi ya makabila katika New York. Wamisionari waliwapa watu Kitabu cha Mormoni, lakini ni wachache wao tu waliweza kusoma.

Picha
wamisionari wakiwasalimia Wenyeji wa Amerika

Kisha wamisionari walikwenda kuhubiri kwa baadhi ya Walamani huko Ohio. Hawa watu walikuwa na furaha kusikia kuhusu Kitabu cha Mormoni na kujifunza juu ya mababu zao.

Picha
Wamisionari wakiondoka wakiwa juu ya farasi

Wamisionari waliondoka Ohio na kwenda katika mji mmoja ulioitwa Independence katika Jackson County, Missouri.

Picha
Wenyeji wa Amerika wakisoma kutoka kwenye Kitabu cha Mormoni

Kulikuwa na Walamani wengi katika Missouri. Wamisionari waliwahubiria Injili na kuwapa Kitabu cha Mormoni. Walikuwa na furaha tele na waliwashukuru wamisionari kwa ajili ya kitabu.

Picha
watu wakiwaambia wamisionari kukaa mbali nao

Watu wengine katika Missouri hawakuamini injili ya urejesho wala Kitabu cha Mormoni. Waliwaambia wamisionari kukaa mbali na Wahindi.

Picha
wamisionari wakiondoka Missouri

Watu walisema askari wangewafukuza wamisionari ikiwa hawakuondoka. Wakiwa wamehuzunika, wamisionari walikwenda kuwafundisha watu wengine huko Missouri.

Picha
Parley P. Pratt akizungumza na Joseph

Mmoja wa wamisionari aliitwa Parley P. Pratt. Alikwenda Ohio kumwaambia Joseph Smith kile walichofanya. Parley alisema misheni yao ilikuwa nzuri na walikuwa wamefundisha Injili kwa watu wengi.

Chapisha