Scripture Stories
Sura ya 9: Uanzishaji wa Kanisa la Yesu Kristo: Aprili 6 1830


Sura ya 9

Uanzishaji wa Kanisa la Yesu Kristo

Aprili 6, 1830

Picha
ubatizo
Picha
Joseph anapokea ufunuo

Joseph Smith alikuwa akiishi katika mji wa Fayette katika jimbo la New York. Yesu alimwambia Joseph ilikuwa ni wakati wa Kanisa Lake la Kweli kuwepo tena duniani. Alimwambia Joseph kuanzisha Kanisa hilo.

Picha
Joseph akiwapa maelekezo viongozi wa Kanisa

Mnamo Aprili 6, 1830, Joseph alifanya mkutano wa kuanzisha Kanisa. Oliver Cowdery, Hyrum Smith, Samuel Smith, David Whitmer, na Peter Whitmer walikuja kumsaidia. Wote walikuwa wamekwisha batizwa. Watu wengine pia walikuja kwenye mkutano.

Picha
Joseph akimtawaza mzee

Wanaume hao waliomba kwa Baba wa Mbinguni. Joseph alimtawaza Oliver kuwa mzee katika Kanisa. Kisha Oliver akamtawaza Joseph.

Picha
Joseph akibariki sakramenti

Joseph na Oliver walibariki sakramenti. Wakawapa watu.

Picha
Joseph akiwathibitisha waumini

Joseph na Oliver waliweka mikono yao juu ya kichwa cha kila mwanamume ili kumthibitisha kuwa muumini wa Kanisa la Yesu Kristo na kumpa kipawa cha Roho Mtakatifu.

Picha
mtu akitoa ushuhuda

Joseph na Oliver waliwatawaza baadhi ya wanaume wengine kwenye ukuhani. Watu hawa walikuwa na furaha tele. Walisema walimpenda Mungu na kuelezea jinsi Yeye alivyowabariki.

Picha
Joseph anapokea ufunuo

Yesu alitoa ufunuo kwa Joseph Smith katika mkutano. Yesu alisema Joseph alikuwa nabii. Nabii wa kweli huongea kwa ajili ya Yesu. Wakati nabii anapoongea kwa ajili ya Yesu, waumini wa Kanisa wanapaswa kumsikiliza na kumtii.

Picha
Joseph akimbatiza mama yake

Baada ya mkutano, watu wengi walibatizwa, wakiwemo mama na baba yake Joseph Smith. Siku nzuri iliyoje! Kanisa la Yesu Kristo lilikuwa duniani tena.

Chapisha