Scripture Stories
Sura ya 2: Ono la kwanza la Joseph Smith: 1820


Sura ya 2

Ono la Kwanza la Joseph Smith

1820

Picha
kijana Joseph akiwa amepiga magoti
Picha
Joseph Smith, Mkubwa

Joseph Smith na familia yake walimwamini Mungu. Walisoma Biblia pamoja. Wazazi wa Joseph waliwafundisha watoto wao kuwa wema.

Picha
Joseph akihudhuria kanisani

Kulikuwa na makanisa mengi sehemu aliyoishi Joseph. Watu wote walitofautiana juu ya kanisa gani lilikuwa sahihi. Joseph hakujua ni kanisa gani la kujiunga nalo. Alitaka kujua ni Kanisa gani lilikuwa la kweli la Yesu Kristo.

Picha
Joseph akisoma Biblia

Siku moja wakati Joseph alipokuwa na umri wa miaka 14, alisoma katika Biblia kwamba tunapaswa kumwomba Mungu wakati tunapotaka kujua kitu. Joseph aliamua kuomba na kumwuliza Mungu ni kanisa gani angejiunga nalo.

Picha
Joseph akiwa amepiga magoti

Katika siku nzuri ya majira ya kuchipua, Joseph alikwenda msituni karibu na nyumba yake. Alipiga magoti na kuomba kwa sauti. Alikuwa na imani ya kwamba Baba wa Mbinguni angejibu maombi yake.

Picha
Joseph akiwa ameshikilia kichwa chake

Shetani hakutaka Joseph aombe. Alijaribu kumzuia Joseph na kufanya giza kumzunguka. Joseph alikuwa na hofu na hakuweza kuzungumza.

Picha
Joseph akiwa amepiga magoti kuomba

Lakini Joseph hakukoma kuomba. Shetani asingeweza kumzuia.

Picha
Baba wa Mbinguni na Yesu

Kisha Joseph alipata ono. Aliona mwanga wenye mng’aro mzuri, uliomzunguka kote. Aliwaona Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wakisimama juu yake angani. Baba wa Mbinguni alimwonyesha Yesu na akasema, “Huyu ni Mwanangu Mpendwa. Msikilize Yeye!”

Picha
Yesu

Joseph alimwuliza Yesu ni kanisa gani angejiunga nalo. Yesu alimwambia Joseph asijiunge na kanisa lolote kwani yote yalikuwa si sahihi. Hakuna hata moja lililokuwa kanisa Lake. Alimwambia Joseph mambo mengine mengi. Kisha ono likamalizika.

Picha
Joseph na mama yake

Wakati Joseph aliporudi nyumbani, mama yake alimuuliza kama alikuwa sawa. Joseph alisema alikuwa sawa. Kisha akamwambia mama yake kuwa alikuwa ameona ono. Alimwambia kile alichojifunza katika ono lake.

Picha
kiongozi wa dini akimkemea Joseph

Joseph pia aliwaambia baadhi ya watu katika mji kuhusu ono lake. Watu hawakumwamini. Walisema alikuwa anasema uongo, na wakawa na hasira na wakawa wakatili kwake.

Picha
Joseph akidhihakiwa

Joseph daima alisema ukweli kuhusu ono lake. Alijua alikuwa amewaona Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Alijua kwamba hakuna kanisa lolote duniani lililokuwa la kweli.

Chapisha