Scripture Stories
Sura ya 10: Muujiza wa Kwanza katika Kanisa: Aprili 1830


Sura ya 10

Muujiza wa Kwanza katika Kanisa

Aprili 1830

Picha
ubatizo
Picha
watu wakihudhuria mkutano wa kanisa

Mkutano uliofuata wa Kanisa ulikuwa siku ya Jumapili, Aprili 11, 1830. Mbali na waumini wa Kanisa, watu wengine wengi walihudhuria mkutano huo.

Picha
Oliver akifundisha Injili

Oliver Cowdery alifundisha injili ya Yesu Kristo. Baadhi ya watu walimwamini Oliver na walitaka kujiunga na Kanisa. Walibatizwa baada ya mkutano.

Picha
Newel Knight

Shetani hakutaka watu wajiunge na Kanisa, hivyo alijaribu kuwafanya baadhi yao wajisikie vibaya. Mmoja wa watu hawa alikuwa mtu mmoja aliyeitwa Newel Knight.

Picha
Newel Knight akiombwa kutoa sala

Joseph alimwomba Newel kusali katika mkutano, na Newel alisema angefanya hivyo.

Picha
Newel Knight akihangaika kuomba

Lakini Shetani hakutaka Newel aombe. Wakati Newel alipokwenda kwenye mkutano, alisema alikuwa na hofu ya kuomba kwa sauti.

Picha
Newel Knight akijaribu kuomba

Asubuhi iliyofuata, Newel Knight aliingia Msituni ili aweze kuomba peke yake. Newel alijaribu kuomba, lakini tena Shetani hakumtaka aombe, na hakuweza kuzungumza. Akawa mgonjwa na mwenye hofu, na akaenda nyumbani.

Picha
Joseph akimbariki Newel

Mke wa Newel alikuwa na wasiwasi juu ya mume wake na akamwomba Joseph Smith kusaidia. Joseph alitumia ukuhani kumbariki Newel na kumfukuza Shetani nje. Baada ya baraka, Newel alijisikia vizuri. Baadaye alibatizwa.

Chapisha