Scripture Stories
Sura ya 1: Joseph Smith na Familia Yake: 1805–1820


Sura ya 1

Joseph Smith na Familia Yake

1805–1820

Picha
kijana Joseph akiwa amepiga magoti
Picha
Joseph Smith akiwa mvulana mdogo

Joseph Smith alizaliwa tarehe 23 Desemba 1805. Familia yake iliishi katika jimbo la Vermont huko Marekani. Baba yake Joseph Smith pia aliitwa Joseph. Jina la mama yake lilikuwa Lucy.

Picha
Joseph na ndugu zake

Joseph alikuwa na kaka watano na dada watatu.

Picha
Familia ya Joseph wakifanya kazi

Mama na baba wa Joseph walikuwa watu wema. Waliwapenda watoto wao na walifanya kazi kwa bidii ili kuwatunza.

Picha
Joseph kitandani

Wakati Joseph alipokuwa kijana mdogo, alikuwa na uvimbe mbaya sana kwenye mguu wake. Madaktari walijaribu kutibu mguu wake, lakini hawakuweza.

Picha
Hyrum akiwa amekaa pembeni mwa kitanda cha Joseph

Hyrum Smith alikuwa mmoja wa kaka wakubwa wa Joseph. Alimpenda Joseph na alisikitika kwamba mguu wa Joseph ulimuuma sana. Aliketi karibu na kitanda cha Joseph na kumsaidia ajisikie vizuri.

Picha
Lucy Mack Smith pamoja na Joseph

Madaktari walitaka kuukata mguu wa Joseph, lakini mama yake hakuwaruhusu. Hivyo madaktari waliamua kukata sehemu ya mfupa. Joseph alijua mguu wake ungeuma wakati madaktari watakapoukata, lakini alikuwa na imani kwamba Baba wa Mbinguni angemsaidia.

Picha
Joseph na mama yake

Madaktari walimtaka Joseph kunywa mvinyo kidogo ili maumivu yasiwe makali sana. Joseph alikataa kunywa mvinyo. Joseph alimwomba mama yake kwenda nje kwa sababu hakumtaka aone madaktari wakikata kwenye mguu wake.

Picha
Madaktari wakifanyia upasuaji mguu wa Josesph

Joseph alimwomba baba yake amshikilie wakati madaktari wakikata kwenye mguu wake. Waliondoa sehemu mbaya za mfupa. Hii iliumiza sana, lakini Joseph alikuwa jasiri. Baada ya siku nyingi, mguu wake ulikuwa vizuri.

Picha
nyumba ya magogo

Wakati Joseph alipokuwa na umri mkubwa, familia yake ilihamia jimbo la New York. Waliishi katika nyumba ya magogo kwenye shamba karibu na Palmyra.

Picha
Lucy Mack Smith akifua nguo

Familia ya Joseph ilikuwa masikini. Walifanya kazi kwa bidii kulipia shamba. Wavulana walimsaidia baba yao kupanda mazao na kutunza mifugo. Wasichana walifanya kazi na mama yao.

Picha
Joseph akivuta fimbo na kaka yake

Joseph alikuwa mtoto mzuri. Alikuwa na furaha na alipenda kucheka na kuburudika.

Chapisha