Scripture Stories
Sura ya 7: Mashahidi Wanaona Mabamba ya Dhahabu: 1829–1830


Sura ya 7

Mashahidi Wanaona Mabamba ya Dhahabu

1829–1830

Picha
mabamba ya dhahabu
Picha
Joseph na Oliver

Joseph Smith na Oliver Cowdery walimaliza kutafsiri Kitabu cha Mormoni. Yesu alitaka watu wasome kitabu. Pia aliwataka wajue kwamba Joseph alikuwa amesema ukweli kuhusu mabamba ya dhahabu.

Picha
Martin Harris, Oliver Cowdery, na David Whitmer

Yesu alichagua watu wengine watatu kuona mabamba ya dhahabu na kuwa mashahidi kwamba yalikuwa halisi. Watu hawa walikuwa Martin Harris, Oliver Cowdery, na David Whitmer.

Picha
malaika na mabamba ya dhahabu

Joseph aliwachukua mashahidi watatu kwenda nao msituni, ambako waliomba. Malaika alikuja na kuwaonyesha mabamba ya dhahabu. Yesu aliwataka mashahidi watatu kuwaambia watu mambo waliyoyaona.

Picha
Joseph, Martin, Oliver na David

Joseph Smith alikuwa na furaha tele. Mashahidi watatu wangewaambia watu juu ya mabamba ya dhahabu, na watu wengi wangeamini kwamba Joseph alisema ukweli.

Picha
mashahidi wanane

Yesu alimwambia Joseph kuonyesha mabamba kwa mashahidi wengine wanane. Wanaume wanane walishika mabamba ya dhahabu katika mikono yao na kuona maandishi kwenye mabamba.

Picha
mashahidi wakiandika barua

Mashahidi wote waliandika juu ya mabamba ya dhahabu. Walisema waliyaona mabamba, na walishuhudia kwamba mabamba yalikuwa halisi. Maneno ya mashahidi yako katika Kitabu cha Mormoni.

Picha
Joseph akimkabidhi Moroni mabamba ya dhahabu

Baada ya Joseph Smith kutafsiri mabamba na mashahidi kuyaona, Joseph hakuyahitaji tena. Malaika Moroni alitokea, na Joseph akamrudishia mabamba ya dhahabu.

Picha
kuchapisha Kitabu cha Mormoni

Baada ya Joseph kumaliza kutafsiri Kitabu cha Mormoni, alikipeleka kwa mchapishaji. Joseph hakuwa na fedha za kumlipa mchapishaji. Martin Harris alikuwa na fedha za kutosha, na katika ufunuo aliombwa kuzitoa ili kumlipa mchapishaji.

Picha
watu waovu

Shetani hakutaka Kitabu cha Mormoni kichapishwe. Hakutaka watu wakisome. Watu waovu walijaribu kuzuia uchapishaji.

Picha
mtu akiiba kurasa za kitabu

Mtu mmoja alikwenda kwenye kiwanda cha uchapishaji Jumapili na kuiba baadhi ya kurasa za Kitabu cha Mormoni. Alichapisha kurasa katika gazeti mpaka pale watu wengine walipomzuia kuziiba.

Picha
mpiga chapa akiwa na kitabu kilichokamilika

Watu waliojaribu kuzuia uchapishaji hawakufanikiwa kwa sababu wale ambao ni waovu hawawezi kuzuia kazi ya Yesu. Baada ya miezi mingi, uchapishaji wa Kitabu cha Mormoni ulikamilika.

Chapisha